Wakuu, ukiwa ndani ya mtumbwi huwezi kukaa kimya unapoona mmoja wenu yuko busy anatoboa mtumbwi katikati ya mto. Madhara yake wote mnayajua.
Yapo mengi yanayoonyesha kuwa kinachofanyika ni kusaidia upinzani;
1. Inakuwaje matukio makubwa na mazito yanatokea na kiongozi anakaa kimya tu bila ya kutoa kauli yoyote? Inahitaji rasilimali gani? Neno, kauli ina nguvu kubwa kiutawala. Au ni style ya upepo, utapita?
2. Inakuwaje Mawaziri wanaachwa wajipiganie na kudhalilika wakati ungeweza kuepusha haya kwa kuyawekea msimamo mapema: Nchimbi, Mwakyembe na wezi wa mafuta na shaba waliotoroshwa ki-mizengwe.
3. Inakuwaje kilio cha watu wa Nchi yako, kupunguza safari za nje, ukubwa wa misafara, unapuuza?
4. Unapata muda saa ngapi wa kutuliza akili na ku-concentrate kushughulikia matatizo yanayolikabli Taifa wakati muda wote uko safari?
5. Ni kweli imeshindikana kuwashushulikia wezi na wabadhirifu wa mali za umma?
6. Kuna ugumu gani kuzifanyia kazi hoja muhimu, hata kama zimetoka upinzani, iwapo zina maslahi kwa Taifa?
7. Huko Zanzibar, CUF pia ni chama shiriki katika kutawala. Hoja zao zinasikilizwa au mpaka wapande jangwani na kufanya mikutano ya hadhara? Kwa nini wanapuuzwa na kupewa majina ya kudhalilisha?
8. Unamkumbuka muasisi wa Perestroita?
Yapo mengi mengine, unawapa tabu wenzio kujitetea muda wote wakati mengine yangeweza kufanyiwa kazi.
Yapo mengi yanayoonyesha kuwa kinachofanyika ni kusaidia upinzani;
1. Inakuwaje matukio makubwa na mazito yanatokea na kiongozi anakaa kimya tu bila ya kutoa kauli yoyote? Inahitaji rasilimali gani? Neno, kauli ina nguvu kubwa kiutawala. Au ni style ya upepo, utapita?
2. Inakuwaje Mawaziri wanaachwa wajipiganie na kudhalilika wakati ungeweza kuepusha haya kwa kuyawekea msimamo mapema: Nchimbi, Mwakyembe na wezi wa mafuta na shaba waliotoroshwa ki-mizengwe.
3. Inakuwaje kilio cha watu wa Nchi yako, kupunguza safari za nje, ukubwa wa misafara, unapuuza?
4. Unapata muda saa ngapi wa kutuliza akili na ku-concentrate kushughulikia matatizo yanayolikabli Taifa wakati muda wote uko safari?
5. Ni kweli imeshindikana kuwashushulikia wezi na wabadhirifu wa mali za umma?
6. Kuna ugumu gani kuzifanyia kazi hoja muhimu, hata kama zimetoka upinzani, iwapo zina maslahi kwa Taifa?
7. Huko Zanzibar, CUF pia ni chama shiriki katika kutawala. Hoja zao zinasikilizwa au mpaka wapande jangwani na kufanya mikutano ya hadhara? Kwa nini wanapuuzwa na kupewa majina ya kudhalilisha?
8. Unamkumbuka muasisi wa Perestroita?
Yapo mengi mengine, unawapa tabu wenzio kujitetea muda wote wakati mengine yangeweza kufanyiwa kazi.