JK in MTWARA...Stay tuned!!

Sizinga

Platinum Member
Oct 30, 2007
9,101
6,027
Huyu bwana anafanya kampen kesho mjini Mtwara...Tutegemee tena Meli kubwa mpya na ya kisasa,mzee wa ahadi!,nitashangaa sana akiacha kutoa hii ahadi. STAY TUNED, Naisubiri hiyo kesho. Nitawajulisha yatakayojili.
 
Kivuko cha Kilambo mpakani na Msumbiji kilizama zaidi ya mwaka na nusu,tafadhali afikishiwe habari hii ili watu wanaovusha magari kuelekea Msumbiji wapate nafuu.Gari ndogo kwa sasa inavushwa kwa laki mbili na nusu kwa kutumia njia mabayo ni ya hatari mno.Ninazo picha ila sielewi namna ya kuzi attach.
Ikiwa atatimiza ahadi hii atakuwa amewasaidia mno wafanyabiashara.
 
Kinana ameshawambia kuwa watanzania wanapenda kusikia ahadi na kushangilia. Mnataka asiahidi? :tonguez:
Watanzania hawataki watekelezaji wa ahadi bali wanataka watu wa kuwaahidi tuuu na kutudanganya.....Sikiliza BBC umsikie Kinana alivyosema:llama:!!
 
Huyu bwana anafanya kampen kesho mjini Mtwara...Tutegemee tena Meli kubwa mpya na ya kisasa,mzee wa ahadi!,nitashangaa sana akiacha kutoa hii ahadi. STAY TUNED, Naisubiri hiyo kesho. Nitawajulisha yatakayojili.

Usisahau kutuwekea you tube ukionyesha umati utaokuwepo pale atapohutubia.
 
Bila kusahau ahadi ya kivuko pale Kivukoni ya Mtwara (soko la samaki,pweza etc)... Kuelekea Ng'ambo na ahadi ya Bandari mji mkongwe wa Mikindani... Lol!
 
Kila leo CCM wanatembea sehemu zote za nchi sasa kutafuta kura za kuiba na wale ambao wanaogopa CCM itawatembelea usiku kuuliza kura. Tukiogopa kupiga kura tunarudisha vizazi vyote vijavyo. CCM haina majibu na kama kuna mtu yeyote anaona hili swala tofauti inawezekana amehamia leo TZ. Nchi inapata shida bila sababu yeyote, kwa kifupi haya ni maswali; kwanini nchi ina struggle kupata maji sehemu nyingi? Solution ya matatizo la huduma za afya mahospitalini? Solution za maswala ya uchumi? Kitu cha kushangaza Kikwete na Wabunge wa CCM wanawadanganya wale wanaodanganyika kwamba wanamajibu mengine ya haya matatizo. Ni muhimu tuchague viongozi wengine ili waleta ideas nyingine mpya kwa nchi yetu ya Tanzania. We do not deserve this poverty. Wizi wa fedha na ushirikina nchini ndio mafanikio ya Kipindi cha kwanza cha Kikwete, akipewa kipindi kingine ataleta sifa gani kwa nchi?
 
Inshu siyo ahadi inshu ni nani atakuwa mmiliki wake, au ndo itakuwa vitega uchumi wake? huyu mzee mjanja anataka akitoka kila sehemu kuliko na ziwa kuna mali yake. Uchumi utakuwa chini ya JK serikali itakuwa haina la kusema zaidi ya kukubaliana na Jk&Co + Familia. Subirini muone, tunauza nchi bila kujua, itakuwa kugumu sana kuwatoa hawa jamaa kama tutawaamini na ahadi zao.

Angalia hiyo Highway ya serengeti mwenye faida nayo kubwa ni JK wengine tulie tu, hakuna la maana zaidi ya kuendelea kujineemesha na mali za nchi hii bila kujali watanzania wote.
 
dah jamaa wamesombwa na magari ..kwa sasa uwanja etlist umejaa..kiaina
 
Back
Top Bottom