Mundali
JF-Expert Member
- Sep 16, 2010
- 749
- 164
Mheshimiwa JK,
Mnamo mwezi June, 2010 pale Dodoma wakati kikao cha bajeti kikiendelea, ulitutangazia watanzania nia njema ya serikali yako ya kunusuru ulichoita hasara waliyopata wafanyabiashara ya mazao na sekta ya utalii kutokana na mtikisiko wa uchumi duniani. Mpango huo mliupa jina "Stimulus Package".
Serikali yako kwa upendo iliokuwa nao kwa wafanyabiashara wale (na si wakulima) mliamua kuwagawia fedha kwa hasara walizosadikika kuzipata. Makampuni yaliyofaidika yamebaki kuwa siri ya serikali yako.
Kwa angalizo tu kipindi hicho ilikuwa ni miezi minne kabla ya wewe kuingia kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu. Ulitenga kiasi cha shilingi 1.3 trilioni kwa mpango (zawadi?) huo. Mimi mtanzania raia wa kuzaliwa sina nchi nyingine ninayoifahamu zaidi ya mama Tanzania, nauliza je,
1. Kipi ni muhimu kati ya wafanyabiashara wachache waliopata hasara ya mtikisiko wa uchumi wa dunia, ama watanzania wote wanaopata hasara kutokana na janga la Giza na kupanda kwa bei za mafuta?
2. Serikali yako iliweza vipi kujibana na kupata shilingi trilioni 1.3 katika bajeti ya 2010/2011 ya stimulus package, ikashindwa kujibana katika bajeti ya 2011/2012 kupata pesa kama hizo kununulia mitambo ya umeme?
3. Mbona trilioni 1.3 zilipatikana mapema kabla ya October 2010?
4. Kuna uhusiano wowote kati ya stimulus package na miezi takribani mitatu ya helikopta tatu kupzunguka nawe nchi nzima katika kampeni zako?
5. Uliweza kuajiri askari wapya zaidi ya 5000 na kununua magari ya maji ya kuwasha na zana nyingine za kutushikisha adabu tukipinga matokeo haramu, kwa mwaka huo wa 2010 pekee, uwezo huo uliutoa wapi mheshimiwa sana?
NAOMBA MAJIBU TAFADHALI MR. PRESIDENT
Mnamo mwezi June, 2010 pale Dodoma wakati kikao cha bajeti kikiendelea, ulitutangazia watanzania nia njema ya serikali yako ya kunusuru ulichoita hasara waliyopata wafanyabiashara ya mazao na sekta ya utalii kutokana na mtikisiko wa uchumi duniani. Mpango huo mliupa jina "Stimulus Package".
Serikali yako kwa upendo iliokuwa nao kwa wafanyabiashara wale (na si wakulima) mliamua kuwagawia fedha kwa hasara walizosadikika kuzipata. Makampuni yaliyofaidika yamebaki kuwa siri ya serikali yako.
Kwa angalizo tu kipindi hicho ilikuwa ni miezi minne kabla ya wewe kuingia kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu. Ulitenga kiasi cha shilingi 1.3 trilioni kwa mpango (zawadi?) huo. Mimi mtanzania raia wa kuzaliwa sina nchi nyingine ninayoifahamu zaidi ya mama Tanzania, nauliza je,
1. Kipi ni muhimu kati ya wafanyabiashara wachache waliopata hasara ya mtikisiko wa uchumi wa dunia, ama watanzania wote wanaopata hasara kutokana na janga la Giza na kupanda kwa bei za mafuta?
2. Serikali yako iliweza vipi kujibana na kupata shilingi trilioni 1.3 katika bajeti ya 2010/2011 ya stimulus package, ikashindwa kujibana katika bajeti ya 2011/2012 kupata pesa kama hizo kununulia mitambo ya umeme?
3. Mbona trilioni 1.3 zilipatikana mapema kabla ya October 2010?
4. Kuna uhusiano wowote kati ya stimulus package na miezi takribani mitatu ya helikopta tatu kupzunguka nawe nchi nzima katika kampeni zako?
5. Uliweza kuajiri askari wapya zaidi ya 5000 na kununua magari ya maji ya kuwasha na zana nyingine za kutushikisha adabu tukipinga matokeo haramu, kwa mwaka huo wa 2010 pekee, uwezo huo uliutoa wapi mheshimiwa sana?
NAOMBA MAJIBU TAFADHALI MR. PRESIDENT