bemg
JF-Expert Member
- Apr 25, 2010
- 2,799
- 642
Napenda kupendekeza katika Baraza jipya la Mawaziri Jk usiache kumpa Dr.Festus Limbu wizara ya Fedha ili uchumi wetu uwe stable na shilingi yetu iwe na thamani kama kipindi cha Mkapa.Ni mtu ambaye ni kwenye uchumi makini naalionyesha anaweza kwenye wizara ile kipindi cha Rais Mkapa akiwa Naibu Waziri wa fedha.Uzuri wake ni kwamba siyo fisadi, amekulia malezi ya mafundisho ya neno la Mungu na hapendi kujilimbikizia mali yeye binafsi au ndugu zake au rafiki zake kama tunavyoona wengine wanapopewa dhamana ya taifa wanakula fastafasta.Anapenda kusimamia ukweli na kile kinachopatikana kifanye kazi stahili kwa watu wote bila kujali itikadi.
Ni jambo nzuri mawaziri na manaibu wake wakawa na hofu ya Mungu ili waone huruma ya maisha magumu kwa watanzania na waweze kusimamia kwa uwazi na ukweli mali za umma.Waache tamaa ya utajiri maana mwisho wake ni kujiangamiza roho zao.
Nawasilisha
Ni jambo nzuri mawaziri na manaibu wake wakawa na hofu ya Mungu ili waone huruma ya maisha magumu kwa watanzania na waweze kusimamia kwa uwazi na ukweli mali za umma.Waache tamaa ya utajiri maana mwisho wake ni kujiangamiza roho zao.
Nawasilisha