Not_Yet_Uhuru
JF-Expert Member
- Oct 11, 2010
- 1,304
- 431
Hakika, Tumeyapokea maneno ya JK kuhusu dhamira yake ya kuleta mchakato wa mabadiliko ya Katiba kwa tahadhari, isiwe tena ghiliba za kisiasa kama ilivyokwishatokea ktk utekelezaji wa tume za majaji Nyalali na Kisanga kuhusu katiba hiyo hiyo. Tunayajua yaliyokwishatokea Tanzania toka miongo mitatu iliyopita.
Hii ya JK itakuma maamuzi yaliyokamilika kama atawang'oa kabisa hawa watu wawili ktk utawala wake yaani Jaji Werema-mwanasheria mkuu na Celina Kombani-Waziri wa sheria na katiba ambao wameshalionyesha taifa kwa kauli zao kuwa hawako njia moja na JK na Pinda.
Hawa watu wawili ni hatari na watakuwa vikwazo na kamwe hawatamsaidia JK na watanzania kufikia lengo la Katiba mpya. Wana muono finyu, hawana lengo na ni wavivu wa fikra kuhusu dira, matakwa na future ya taifa na watanzania na hawafai kuwepo tena serikalini. Tunaomba wawajibishwa mapema.
Naomba kuwasilisha, tulijadili.
Hii ya JK itakuma maamuzi yaliyokamilika kama atawang'oa kabisa hawa watu wawili ktk utawala wake yaani Jaji Werema-mwanasheria mkuu na Celina Kombani-Waziri wa sheria na katiba ambao wameshalionyesha taifa kwa kauli zao kuwa hawako njia moja na JK na Pinda.
Hawa watu wawili ni hatari na watakuwa vikwazo na kamwe hawatamsaidia JK na watanzania kufikia lengo la Katiba mpya. Wana muono finyu, hawana lengo na ni wavivu wa fikra kuhusu dira, matakwa na future ya taifa na watanzania na hawafai kuwepo tena serikalini. Tunaomba wawajibishwa mapema.
Naomba kuwasilisha, tulijadili.