The Planner
JF-Expert Member
- Dec 1, 2010
- 357
- 118
Siku zote wahenga hunena, panapofuka moshi kuna moto, Nimeanza kwa msemo huu nikijaribu kuoanisha na jinsi mambo yanavyokwenda katika kipindi hiki kifupi baada ya uchaguzi. Migomo imeanza kushika kasi karibu katika maeneo mengi kuanzia vyuo vikuu, wafanyakazi wa reli, wachimba mchanga huko mbeya, ukiangalia hapa ni kwamba kuna mambo hayaendi sawa kwa wasomi, wafanyakazi na wananchi wa kawaida. JK this is not a good sign, hawa watu wanafanya migomo na maandamano kuexpress hisia zao, lakini time will come wataona migomo haiwasaidii, itakuwa hatari sana kupambana na watu waliokata tamaa, hawa huwa hawana cha kupoteza.,Nawasilisha!