Ibrah
JF-Expert Member
- Mar 22, 2007
- 2,729
- 528
Hakuna kitu kinachoniumiza katika maisha yetu ya kila siku katika nchi yetu tukufu ya Tanzania kama maisha duni waliyonayo Watanzania. Bahati mbaya sana, kila kunapokucha ni heri ya jana- hali ya maisha inaziodi kuwa mbaya kadiri siku zinavyosonga mbele!
Ajabu ni kuwa takwimu zinazotolewa kila wakati zinaonyesha kuwa kipato cha Watanzania kimepanda na kuashiria kuwa maisha yamekuwa bora. Ukweli ni kuwa Maisha ya Watanzani wengi ni duni mno; kila siku iendayo kwa Mungu hali inazidi kuwa mbaya zaidi na ule msemo wa kila kukicha heri ya jana unajidhirisha!
Hebu tafakari mabadiliko ya bei hizi bidhaa hizi muhimu tangu mwaka 2005:-
Sukari
Mwaka 2005, wakati JK anakabidhiwa nchi na mtangulizi wake Mkapa kilo moja ya sukari ilikuwa shilingi mia tano 500/- leo hii miaka mitano tu bei ya sukari imepanda mara tatu zaidi na kufikia shilingi 1,500/-!
Mkate
Mwaka 2005, wakati Mh JK anachukua nchi; bei ya mkate wa kawaida wa Super Loaf, ilikuwa shilingi 300/- leo hii mkate huo huo unauzwa shilingi 700/-!
Orodha ni ndefu mno na unaweza kuongeza na kuongeza. Hii ni tofauti kabisa na kauli mbiu ya Rais wetu JK wakati akipigania kura na ahadi kemkem na kauli mbiu maarufu "Maisha bora kwa kila Mtanzania"
Maisha bora sasa imekuwa maisha balaa kwa kila Mtanzania! Watawala wetu waulizwapo kuhusu ahadi ya JK ya Maisha bora hutugeuzia kibao na kujibu ati Maisha bora hayaji kwa kukaa tu! Hivi ni kweli Watanzania tumekaa tu kusubiria hayo maisha bora? Mbona Watawala mnatudhihaki?
Tukilinganisha hali za Maisha ya Watanzania katika awamu hizi mbili- awamu ya 3 na awamu ya 4 utaona kuwa Awamu hii imechangia sana kudunisha maisha ya Watanzania kwa kiwango kikubwa sana ingawa ni awamu ambayo ina nafasi nzuri sana ya kuboresha maisha kuliko awamu iliyopita maana Mkapa aliwaachi misingi imara ya kiuchumi na namna yha kudhibiti mfumuko wa bei ambao ni kisu kilakali kwenye vifua vya Watanzania wengi. Awamu ya JK ina neema kubwa ya kukuzsanya mapato mengi zaidi kuliko awamu iliyotangulia lakini ni kama vile Utawala wa JK umevaa suruali yenye mifuko iliyotoboka!
Kwa kuangalia maisha ya Watanzania na matumizi makubwa ya Watawala wa Awamu ya 4- safari nyingi, Warsha na Semina tele tunaona kuwa JK ametusaliti sana Watanzania maana ni marafiki zake na ndugu zao ndo wanaofaidi hayo Maisha bora mabayo kwa Watanzania wengi ni maisha balaa!
TUTAFAKARI!
Ajabu ni kuwa takwimu zinazotolewa kila wakati zinaonyesha kuwa kipato cha Watanzania kimepanda na kuashiria kuwa maisha yamekuwa bora. Ukweli ni kuwa Maisha ya Watanzani wengi ni duni mno; kila siku iendayo kwa Mungu hali inazidi kuwa mbaya zaidi na ule msemo wa kila kukicha heri ya jana unajidhirisha!
Hebu tafakari mabadiliko ya bei hizi bidhaa hizi muhimu tangu mwaka 2005:-
Sukari
Mwaka 2005, wakati JK anakabidhiwa nchi na mtangulizi wake Mkapa kilo moja ya sukari ilikuwa shilingi mia tano 500/- leo hii miaka mitano tu bei ya sukari imepanda mara tatu zaidi na kufikia shilingi 1,500/-!
Mkate
Mwaka 2005, wakati Mh JK anachukua nchi; bei ya mkate wa kawaida wa Super Loaf, ilikuwa shilingi 300/- leo hii mkate huo huo unauzwa shilingi 700/-!
Orodha ni ndefu mno na unaweza kuongeza na kuongeza. Hii ni tofauti kabisa na kauli mbiu ya Rais wetu JK wakati akipigania kura na ahadi kemkem na kauli mbiu maarufu "Maisha bora kwa kila Mtanzania"
Maisha bora sasa imekuwa maisha balaa kwa kila Mtanzania! Watawala wetu waulizwapo kuhusu ahadi ya JK ya Maisha bora hutugeuzia kibao na kujibu ati Maisha bora hayaji kwa kukaa tu! Hivi ni kweli Watanzania tumekaa tu kusubiria hayo maisha bora? Mbona Watawala mnatudhihaki?
Tukilinganisha hali za Maisha ya Watanzania katika awamu hizi mbili- awamu ya 3 na awamu ya 4 utaona kuwa Awamu hii imechangia sana kudunisha maisha ya Watanzania kwa kiwango kikubwa sana ingawa ni awamu ambayo ina nafasi nzuri sana ya kuboresha maisha kuliko awamu iliyopita maana Mkapa aliwaachi misingi imara ya kiuchumi na namna yha kudhibiti mfumuko wa bei ambao ni kisu kilakali kwenye vifua vya Watanzania wengi. Awamu ya JK ina neema kubwa ya kukuzsanya mapato mengi zaidi kuliko awamu iliyotangulia lakini ni kama vile Utawala wa JK umevaa suruali yenye mifuko iliyotoboka!
Kwa kuangalia maisha ya Watanzania na matumizi makubwa ya Watawala wa Awamu ya 4- safari nyingi, Warsha na Semina tele tunaona kuwa JK ametusaliti sana Watanzania maana ni marafiki zake na ndugu zao ndo wanaofaidi hayo Maisha bora mabayo kwa Watanzania wengi ni maisha balaa!
TUTAFAKARI!