magistergtz
JF-Expert Member
- Dec 17, 2011
- 282
- 56
Kauli ya jk kuwa mawazili alowatimua wanawajibika kwa makosa yasio yao, bali ya watendaji walio chini yao inaudhi. Zaidi ya kuudhi inatia wasiwasi kama jk anaelewa wajibu wa mawaziri wake.
Wajibu wa mawaziri ni kuongoza na kusimamia watendaji walio chini yao. ,Huu ndo wajibu wa kiongozi yeyote ile. Kwa kifupi kazi ya kiongozi ni. kuhakikisha walio chini yake wanafanya kazi kwa mujibu wa taratibu zalizopo. Watendaji wakiharibu na kiongozi hachukui hatua yoyote, ina maana huyo kiongozi kashindwa majukumu yake na anastahili kuwajibishwa sawa na mtendaji aloharibu.
Hivo basi kauli ya jk kuwa mawaziri wameponzwa na fitna na madudu ya watendaji yenye lengo la kuwasafisha mawaziri ni potoshi. Mawaziri wamekosea na wameshindwa kutimiza wajibu waloapa kuutimiza. Walistahili kufukuzwa.
Je, kama hawana makosa ni umbea na fitna tu iweje awafukuze??????
Mawaziri 6 walotimuliwa walistahili na inabidi washtakiwe kwa kutotimiza wajibu. Kauli za kuwasafisha zinaashiria jk hakuwa na utashi bali alichukua hatua kwa shinikizo tu.
Wajibu wa mawaziri ni kuongoza na kusimamia watendaji walio chini yao. ,Huu ndo wajibu wa kiongozi yeyote ile. Kwa kifupi kazi ya kiongozi ni. kuhakikisha walio chini yake wanafanya kazi kwa mujibu wa taratibu zalizopo. Watendaji wakiharibu na kiongozi hachukui hatua yoyote, ina maana huyo kiongozi kashindwa majukumu yake na anastahili kuwajibishwa sawa na mtendaji aloharibu.
Hivo basi kauli ya jk kuwa mawaziri wameponzwa na fitna na madudu ya watendaji yenye lengo la kuwasafisha mawaziri ni potoshi. Mawaziri wamekosea na wameshindwa kutimiza wajibu waloapa kuutimiza. Walistahili kufukuzwa.
Je, kama hawana makosa ni umbea na fitna tu iweje awafukuze??????
Mawaziri 6 walotimuliwa walistahili na inabidi washtakiwe kwa kutotimiza wajibu. Kauli za kuwasafisha zinaashiria jk hakuwa na utashi bali alichukua hatua kwa shinikizo tu.