Indume Yene
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 2,950
- 711
Rais JK amemteua balozi T. Manongi kuziba nafasi iliyokuwa ya balozi Ombeni Umoja wa Mataifa. Ninakuwa na wasiwasi na huu uteuzi hasa baada ya Mama Migiro kutembelea ikulu juzi tu halafu msaidizi wake anapelekwa tena huko...just curious.
kuna kama kalaana fulani aisee na hiyo email, inakera sanaHivi Ikulu bado inatumia email ya yahoo tu jamani?
Hivi kuna mtu anajali hili kama swala la national security?
Mie sijaelewa hapo panaposema Mwakilishi wa kudumu!!!Ina maana hadi kifo kimtenganishe na hicho cheo?
Mie sijaelewa hapo panaposema Mwakilishi wa kudumu!!!Ina maana hadi kifo kimtenganishe na hicho cheo?
Hata mimi najiulizaga hivyo hivyo!
Kwa nini aitwe "mwakilishi wa kudumu"? Picha ninayopata mimi ni kwamba atadumu huko UN mpaka atakapokufa!!
I suspect imekuwa convention siku nyingi hata wenyewe ukiwauliza wanaweza kushindwa kukuelezea.
Mi naona wanatofautisha tu kati ya "Balozi" (ambaye naye strangely ni Muwakilishi wa Kudumu) na "Muwakilishi wa Kudumu" (ambaye naye almost always ni balozi by rank) kwa maana ya kwamba balozi anapeleka credentials kwa Head of State na Muwakilishi wa Kudumu ni kwa UN organizations au NATO/EU na kwa hivo hapeleki hati kwa Mkuu wa Nchi.
Tatizo ni neno "kudumu" linapotumika kwa huyo mwakilishi.
Kudumu maana yake ni kuendelea kuishi au kuwepo kwa muda wote.
Katika umoja wa mataifa nadhani uanachama wetu labda ndiyo wa kudumu lakini si hao watu au huyo mtu anayetuwakilisha. Yeye huwa hadumu.
Wanapotumia "mwakilishi wa kudumu" kumuelezea mtu atakayetuwakilisha huko wanazua utata kidogo.
NB: Halafu hiyo "muwakilishi" ni Kiswahili cha wapi hicho? Maana Kamusi ya Kiswahili Sanifu ya Oxford toleo la pili iliyochapishwa mwaka 2012 na kamusi ya TUKI chapa ya tano iliyotolewa mwaka 2010 zote zina "mwakilishi"....
Hiyo habari ya "Muwakilishi wa Kudumu" inazama katika historia ya diplomasia.Kulikuwa na wawakilishi wa kutumwa mara moja.Rais/ mfalme anamtuma muwakilishi kwenda kwenye nchi fulani kwa sababu maalum, ama kutuma ujumbe fulani ama kuhudhuria kikao fulani.
Zilipokuja habari za kuwa na haja ya kuwa na ubalozi, na kuwa na balozi ambaye badala ya kutumwa kwa mara moja, anakaa kabisa katika mji wa nchi ya kigeni kama muwakilishi wa serikali yake, hapo ndipo pakatokea habari ya "muwakilishi wa kudumu".
Muwakilishi wa kudumu haina maana kwamba hatoki mpaka kifo.
Hivi Ikulu bado inatumia email ya yahoo tu jamani?
Hivi kuna mtu anajali hili kama swala la national security?