Not_Yet_Uhuru
JF-Expert Member
- Oct 11, 2010
- 1,304
- 431
JK ametoboa jinsi viongozi wa CCM wanavyoowamaliza Watanzania....kwa kuwafanya 'malofa' na kuwaibia haki ya kupata viongozi wasio na dira, mafisadi. JK akihutubia katika Miaka 35 ya Chama Cha Mafisadi, Kirumba Mwanza mchana huu, ameweka wazi 'ujinga wa watanzania' na hasa kudanganywa katika kufanya maamuzi katika kupiga Kura, pale alipofikia hatua ya kurejea kauli ya kudhalilisha aliyowahi kuitamka aliyewahi kugombea Jimbo la Ukonga, Marehemu Ukiwaona Dito wa Muzuzuri (Ditopile), pale aliposema kuwa tatizo la watanzania ni 'ULOFA WAO' maana huwa wanakubali kupelekwa kukesha guest, wanaacha wake au waume zao na watoto majumbani wamelala, mwishowe wanagawiwa sh. 1,000 au 2,000 tu na vipapatio vya kuku, wanakubali kuwapigia kura viongozi wabovu, waliooza. JK kasisitiza kuwa Dito alikuwa 'mkweli', kuwaambia watanzania kuwa 'malofa', aliwapasha ukweli! Pamoja na yote hayo, JK alizidi kuwafumbua macho wasikilizaji na Watanzania wote kuwa kwa kauli aliyotoa Dito ya kuwa 'Malofa', wapiga kura walikasirika, walimkimbia ktk mikutano yake, alikosa kura ktk chaguzi zote zilizofuata....!
Na yeye JK kwa kafikia kuhalalisha kuwa Dito 'aliwapasha ukweli' Watanzania kuwa ni 'MALOFA', tunalo la kubisha?? Naomba kuwasilisha!
PAMOJA DAIMA! (Source: Tiibisii)
Na yeye JK kwa kafikia kuhalalisha kuwa Dito 'aliwapasha ukweli' Watanzania kuwa ni 'MALOFA', tunalo la kubisha?? Naomba kuwasilisha!
PAMOJA DAIMA! (Source: Tiibisii)