JK awaambia wanaoishi UGhaibuni wasisahau nyumbani!

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
wakuu mbali ya kupiga kelele sanahapajamvini tujitahidi kujituma ili tuweze kuwasaidia ndugu zetu wanyumbani.

na kujiletea maendeleo yetu na jamii zetu. mengi muuungwana katukumbusha hapo chini


Muishio ughaibuni msisahau Tanzania - JK
2007-10-25 10:05:52
Na Maura Mwingira, Paris


Rais Jakaya Kikwete amewakumbusha watanzania wote wanaoishi nje kutosahau kuendeleza walikozaliwa na kuwaendeleza ndugu zao ambao wamewaacha nyumbani.

Rais alitoa wito huo wakati akiongea na watanzania wanaoishi nchini Ufaransa.

Alisema tofauti ya wao kuishi ?majuu? itajidhihirisha kwa kuboresha maisha ya jamii yao, ikiwa ni pamoja na kujenga makazi bora.

Aliwataka pia kukumbuka kuwekeza nyumbani na kuwavutia wawekezaji na watalii kuja Tanzania, lakini pia aliwataka wasiogope kurudi ?Bongo? pale watakapoona maisha ya ughaibuni yamewashinda.

Akifafanua kuhusu uboreshaji wa miundombinu, Rais aliwaeleza watanzania hao hatua ambazo zinachukuliwa na serikali za kulifufua shirika la Ndege la Tanzania (Air Tanzania).

Hata hivyo, amewakumbusha kuwa Tanzania bado ni nchi maskini sana ambayo wastani wa Pato la mtu kwa mwaka ni Dola za Marekani 370 kwa mwaka, hivyo wasitarajie miujiza itakayoibadili nchi hiyo haraka haraka na kuwa nchi yenye pepo kama zilivyo nchi zilizoendelea.

Alisisitiza kuwa hata Roma au miji mingine maarufu duniani haikujengwa mara moja, lakini pamoja na changamoto mbalimbali serikali imejipanga vema kuwaletea hali bora ya maisha nafuu wananchi wake.

Kuhusu hali ya kisiasa, demokraria, utawala bora na vita dhidi ya rushwa, Rais alisema kuwa kwa ujumla hali ya kisiasa ni shwari sana, na kwamba hali ya siasa imekuwa hai (active) na kwamba uhuru wa kidemokrasia umeshamiri sana, jambo alilosema ni zuri.

Rais pia aliwaambia Watanzania hao kuwa serikali haitakuwa tayari kuwasaidia watanzania wanaoishi nje ya nchi ambao watajiingiza katika vitendo vya uvunjaji wa sheria za nchi wanazoishi.

Aliwataka kuzingatia kanuni, sheria na taratibu za wenyeji wao na hasa kwa vile hakuna aliyewalazimisha kwenda huko, bali walikwenda kwa hiari yao wenyewe.

?Lakini wakikusingizia umeiba ili hali wewe hukuiba na ikathibitishwa hukuiba basi hapo serikali itakutetea kwa hali na mali,? alisema.

SOURCE: Nipashe
 
...sawa bro kikwete nitajitahidi kutuma school feekwa binamu wangu ili asome!
 
Hilo ndilo muhimu, kila anayejiweza kidogo akisaidia kusomesha ndugu mmoja ama wawili, atakuwa ametoa mchango wa maana. Zamani watu walikuwa wanasaidia ndugu kwa kuwaleta mjini, kukaa nao mpaka wanapata kazi. Siku hizi kazi ni tatizo, nafikiri msaada wa maana ni kwenye elimu.

Pia wasomi wengi hawajengi kwao, kiasi kuwa inakuwa ngumu hata kurudi likizo maana hata watoto watashangaa kuona baba anayetamba Dar huku kwao hata kibanda hakuna? Nawasifu ndugu zetu wa Kilimanjaro na Rungwe kwa hili.

Mtu ukijenga kwenu, utapata nguvu ya kurudi likizo mara nyingi na vijana wa huko wilayani watakuwa japo wana role model wa kumwangalia juu ya kujiendeleza through elimu.
 
Hivi anaweza kutueleza serikali ya Tanzania huwa inatoa msaada gani kwa wananchi. Wengi sana waishio nje hawataki hata kukanyaga balozi zetu kwa kufahamu kwamba unless you know somebody; huwa hawana msaada wowote, labda uwe Ridh**** etc.
 
wakuu mbali ya kupiga kelele sanahapajamvini tujitahidi kujituma ili tuweze kuwasaidia ndugu zetu wanyumbani.

na kujiletea maendeleo yetu na jamii zetu. mengi muuungwana katukumbusha hapo chini


Muishio ughaibuni msisahau Tanzania - JK
2007-10-25 10:05:52
Na Maura Mwingira, Paris


Rais Jakaya Kikwete amewakumbusha watanzania wote wanaoishi nje kutosahau kuendeleza walikozaliwa na kuwaendeleza ndugu zao ambao wamewaacha nyumbani.

Rais alitoa wito huo wakati akiongea na watanzania wanaoishi nchini Ufaransa.

Alisema tofauti ya wao kuishi ?majuu? itajidhihirisha kwa kuboresha maisha ya jamii yao, ikiwa ni pamoja na kujenga makazi bora.

Aliwataka pia kukumbuka kuwekeza nyumbani na kuwavutia wawekezaji na watalii kuja Tanzania, lakini pia aliwataka wasiogope kurudi ?Bongo? pale watakapoona maisha ya ughaibuni yamewashinda.

Akifafanua kuhusu uboreshaji wa miundombinu, Rais aliwaeleza watanzania hao hatua ambazo zinachukuliwa na serikali za kulifufua shirika la Ndege la Tanzania (Air Tanzania).

Hata hivyo, amewakumbusha kuwa Tanzania bado ni nchi maskini sana ambayo wastani wa Pato la mtu kwa mwaka ni Dola za Marekani 370 kwa mwaka, hivyo wasitarajie miujiza itakayoibadili nchi hiyo haraka haraka na kuwa nchi yenye pepo kama zilivyo nchi zilizoendelea.

Alisisitiza kuwa hata Roma au miji mingine maarufu duniani haikujengwa mara moja, lakini pamoja na changamoto mbalimbali serikali imejipanga vema kuwaletea hali bora ya maisha nafuu wananchi wake.

Kuhusu hali ya kisiasa, demokraria, utawala bora na vita dhidi ya rushwa, Rais alisema kuwa kwa ujumla hali ya kisiasa ni shwari sana, na kwamba hali ya siasa imekuwa hai (active) na kwamba uhuru wa kidemokrasia umeshamiri sana, jambo alilosema ni zuri.

Rais pia aliwaambia Watanzania hao kuwa serikali haitakuwa tayari kuwasaidia watanzania wanaoishi nje ya nchi ambao watajiingiza katika vitendo vya uvunjaji wa sheria za nchi wanazoishi.

Aliwataka kuzingatia kanuni, sheria na taratibu za wenyeji wao na hasa kwa vile hakuna aliyewalazimisha kwenda huko, bali walikwenda kwa hiari yao wenyewe.

?Lakini wakikusingizia umeiba ili hali wewe hukuiba na ikathibitishwa hukuiba basi hapo serikali itakutetea kwa hali na mali,? alisema.

SOURCE: Nipashe

ANA WAZIMU HUYU JK
 
Hivi anaweza kutueleza serikali ya Tanzania huwa inatoa msaada gani kwa wananchi. Wengi sana waishio nje hawataki hata kukanyaga balozi zetu kwa kufahamu kwamba unless you know somebody; huwa hawana msaada wowote, labda uwe Ridh**** etc.

Dua,

Wewe si upo UK, mbona Balozi (mama Majaar) ana msaada jamani? Ni makosa kulaumu balozi zote kwa pamoja, kuna wafanyakazi wa baadhi ya balozi wanajitahidi, hqao tuwapongeze na wale wanaonyanyasa Watanzania wenzao ndio tuwaandame.

Kawaambia Watanzania wakamwone kila alhamisi ya kwanza ya mwezi, nasikia mpaka sasa
ni wachache wanaoenda, hii ina maana hatuna shida.
 
Dua,

Wewe si upo UK, mbona Balozi (mama Majaar) ana msaada jamani? Ni makosa kulaumu balozi zote kwa pamoja, kuna wafanyakazi wa baadhi ya balozi wanajitahidi, hqao tuwapongeze na wale wanaonyanyasa Watanzania wenzao ndio tuwaandame.

Kawaambia Watanzania wakamwone kila alhamisi ya kwanza ya mwezi, nasikia mpaka sasa
ni wachache wanaoenda, hii ina maana hatuna shida.

Mimi sikutaja ni balozi wa nchi gani, ninaongelea experience yangu binafsi katika balozi za Tanzania pamoja na habari ambazo ndizo watanzania wengi wanasema tunapokuwa na mawasiliano. Kweli UK balozi anafanya hivyo lakini hiyo ofisi ni one out of how many? Kinachotakiwa ni kutokuwa na malalamiko katika ofisi zaidi ya 50%. UK inawezekana watu bado wana ile ya kudhania hawawezi kupewa msaada mara wanapokwenda pale lakini elewa kitu kimoja WTZ wenye matatizo wamekata tamaa na hawataki hata kwenda huko. Uliza kwa nini? TABIA ILIYOKUWA IMEJENGEKA - HAWATHAMINIWI.

Mimi nikiwa na shida wala sisubiri hiyo alhamisi ataniona ofisini kwake asubuhi na mapema kwa sababu najua haki zangu.
 
...sawa bro kikwete nitajitahidi kutuma school feekwa binamu wangu ili asome!

inaleta matumaini kwa kuungana na mheshimiwa pale anapoomba jambo kwa wanachi wake, baadala ya kupinga kila kitu anachosema (angalau saa nyingine tunatofautiana) hadi kuonekana hakuna hope ndipo life ekspektansi inaposhuka, watoto wa miaka 20 kuonekana kama vizee bana !
 
Hilo ndilo muhimu, kila anayejiweza kidogo akisaidia kusomesha ndugu mmoja ama wawili, atakuwa ametoa mchango wa maana. Zamani watu walikuwa wanasaidia ndugu kwa kuwaleta mjini, kukaa nao mpaka wanapata kazi. Siku hizi kazi ni tatizo, nafikiri msaada wa maana ni kwenye elimu.

Pia wasomi wengi hawajengi kwao, kiasi kuwa inakuwa ngumu hata kurudi likizo maana hata watoto watashangaa kuona baba anayetamba Dar huku kwao hata kibanda hakuna? Nawasifu ndugu zetu wa Kilimanjaro na Rungwe kwa hili.

Mtu ukijenga kwenu, utapata nguvu ya kurudi likizo mara nyingi na vijana wa huko wilayani watakuwa japo wana role model wa kumwangalia juu ya kujiendeleza through elimu.

Maneno mazuri hayo, kujenga taifa itakuwa vizuri tukishare tasks na serikali hasa pale inapotuomba wananchi tusaidie pale tunapoweza !

Kuwa karibu na serikali kwa kushirikiana kimawazo, things n.k kuteleta maendeleo na kujenga imani kwa vizazi vijavyo !
 
Back
Top Bottom