Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,316
- 33,125
MGOMBEA urais kwa tiketi ya CCM Jakaya Kikwete jana aliendelea kumwaga ahadi kwenye kampeni zake mkoani Lindi, huku akibainisha kuwa tayari ameanza kutekeleza ahadi ya kugawa vyandarua viwili kila kaya aliyoitoa hivi karibuni.
Akizungumza kwenye uwanja wa Nyangao Jimbo la Mtama, Kikwete alisema ahadi ya kugawa vyandarua hivyo, imeanza kutekelezwa mkoani Lindi.
Hivi karibuni niliahidi kugawa vyandarua viwili kila kaya, ahadi hiyo tumeanza kuitekeleza kwa wakazi wa Mkoa wa Lindi ambako tumepeleka vyandarua 145,968,alisema na kuendelea:
Watu wanasema sana kwamba rais anatembea sana na mimi nasema, kama ningekaa Dar es Salaam na kuangalia uzuri wa mke wangu, Watanzania wangekufa.
Nisingetembea ningefahamiana wapi na Bushi hata anipe vyandarua bilioni 5.2 ? alihoji.
Kikwete alitaja faida zingine za ziara zake nje ya nchi kuwa ni pamoja na kufahamiana na serikali ya Marekani ambayo imeahidi kuipa Tanzania msaada wa vitabu vya sayansi.
Vitabu 800,000 ya masomo ya sayansi wameshatupatia na mwakani wataendelea kutupa vitabu vingine milioni 2.4, alisema.
Alieleza kuwa mbali na msaada wa vitabu, serikali yake ijayo ina mpango maalumu wa miaka mitano kujenga nyumba za walimu ili kuwawekea mazingira mazuri ya kazi.
Tunapanga pia kuajiri walimu 19,000 ambao tutawagawanya watano kila shule za sekondari za kata, alisema Kikwete na kuongeza kwamba serikali yake pia ina mpango wa kuboresha Hospitali ya Taifa Muhimbili na kujenga hospitali nyingine ili kusaidiana kukabiliana na changamoto za kuuwahudumia Watanzania.
Pia tuna mpango wa kuhamisha Chuo Kikuu cha Muhimbili kutoka mahala kilipo n kukipeleka Mlonganzila ambako pia tutajenga hospitali nyingine kubwa itakayoshirikiana na Muhimbili. Lengo letu ni kupunguza tatizo la kupeleka wagongwa nje ya nchi na kuwaleta wagonjwa kutoka nje kuja kutibiwa hapa, alisema Kikwete.
Akizungumzia suala la afya kwa wakazi wa Jimbo la Mtama, Kikwete alisema ana mpango wa kuipandisha hadhi Hospitali ya Nyangao ili iwe na hadhi ya Hospitali Teule na Hospitali ya Mandawa iliyoko Lindi vijijini kuwa hospitali ya wilaya.
Awali Kikwete aliwataka wananchi kuichagua CCM akieleza mambo matatu aliyosema ndio kigezo cha chama hicho kuendelea kutawala.
Nawaombeni Watanzani tuichague CCM kwa sababu tatu muhimu:Moja hakuna chama bora kuliko CCM kwa muundo, sera na mipango. Vipo vyama 18 lakini wengine ni photocopy, vinajaribu kutuiga na hii ni haki yao kwani ukichelewa kuzaliwa unapaswa kuwaiga waliokutangulia, alisema na kuendelea:
Sababu ya pili ya kuwatakeni muichagua CCM ni kwamba imeongoza nchi hii vizuri. Nchi imetulia ndiyo ni maskini lakini mambo yamebadilika sana ikilinganishwa na wakati wa uhuru.
Pia sisi ni waaminifu.Tukiahidi tunatekeleza. Mwaka 2005 tuliahidi amani na utulivu natumefanya.
chanzo: Gazeti la Mwananchi