JK apingwa kortini kugombea urais 2010

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,037
22,728
Na Makumba Mwemezi - Majira

RAIS Jakaya Kikwete amewekewa pingamizi kortini kugombea urais mwaka huu kwa madai ya matumizi mabaya ya madaraka na ufujaji wa fedha za umma katika safari zake za nje.

Hayo yameelezwa na Mwalimu Mstaafu na Mkazi wa Dar es Salaam, Bw. Paul Mhozya ambaye amefungua kesi katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam kupinga mgombea huyo katika uchaguzi wa Oktoba 31, mwaka huu.

Akizungumza na Majira jana, Bw. Mhozya alisema amefungua pingamizi hilo chini ya hati ya dharura akiitaka mahakama kulisikiliza mapema kabla kampeni kuanza, hivyo akaishauri CCM kuteua mgombea mbadala mapema, badala ya kusubiri uamuzi wa mahakama.


Katika hati ya mashtaka yenye sababu kumi za kuiomba mahakama imuengue Rais Kikwete kwenye kinyang'anyiro cha urais Bw. Mhozya anasema, rais ametumia nafasi aliyopewa kwa mambo binafsi, amekiuka katiba na kuvunja haki za binaadamu pamoja na matumizi holele ya fedha za watanzania kwa mambo yake mwenyewe.

Gazeti la The Citizen toleo la jana lilimkariri Bw. Mhozya kuwa aliwahi kufungua kesi ya kikatiba kama hiyo mwaka 1993 dhidi ya Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi kuwa alivunja katiba kwa kuruhusu Zanzibar kujiunga na Jumuiya ya Kiislamu (OIC), lakini ikatupwa na Jaji Barnabas Samatta kuwa mamlaka ya kumwondoa rais madarakani yalikuwa mikononi mwa bunge peke yake, chini ya kifungu cha 46A cha katiba.

Bw. Mhozya alisema amefikia uamuzi wa kufungua kesi hiyo kutokana na ujeuri uliooneshwa na Rais Kikwete katika miaka mitano ya uongozi wake, hivyo ni vema akazuiwa kuurudia kwa kumzuia asirudi madarakani.

Alisema anayo orodha ndefu ya mambo mabaya aliyofanya Rais Kikwete wakati wa uongozi wake, ambayo anatarajia kuyatumia kama ushahidi na uthibitisho wa malalamiko aliyopeleka mahakamani, ambayo anaamini yatakubaliwa na kumwondoa kwenye kinyang'anyiro.

"Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi (NEC), Jaji Lewis Makame alikwishasema kuwa tume iko tayari kupokea pingamizi dhidi ya mgombea yoyote kwa maslahi ya umma na kuwa itachukua hatua stahili, ninasubiri kauli ya mahakama na ninaamini itasikiliza hoja zangu na kuzifanyia kazi," alisema.

Alisema kuwa yeye kama Mtanzania anayo mamlaka chini ya ibara ya 30 (3) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufungua kesi dhidi ya uvunjaji wa ibara yoyote ndani ya katiba hasa zinazohusu haki za binaadamu.

Ibara ya 30 (3) inasema "Mtu yeyote anayedai kuwa sharti lolote katika Sehemu hii ya Sura hii au katika sheria yoyote inayohusu haki yake au wajibu kwake limevunjwa, linavunjwa au inaelekea litavunjwa na mtu yeyote popote katika Jamhuri ya Muungano, anaweza kufungua shauri katika Mahakama Kuu"

Bw. Mhozya anasema pamoja na kuwa Rais ana kinga kisheria lakini Kikwete hana kinga ya kuwekewa pingamizi kama mgombea kwa sasa, ndio maana akaamua kufungua kesi hii wakati huu badala ya kusubiri atakaposhinda na kuwa rais, kwani atakuwa na uwezo wa kutumia kinga yake.

Alisema katika kipindi cha uongozi wake rais amefanya safari za ughaibuni zisizo za lazima nyingi kwa fedha za umma, jambo ambalo limesababisha wananch wengi kuishi maisha ya taabu na umaskini mkubwa, huku akidai kuwa urais ni suala binafsi, akisema kuwa ndio maana alimteua mwanawe kumtafutia wadhamini.

Alisema sheria inaitaka NEC kutoa muda wa ziada kwa chama ambacho mgombea wake amekufa au ameshindwa kuendelea kukiwakilisha, ili chama hicho kiweze kuteua mgombea mwingine, hivyo anaamini kuwa baada ya pingamizi hilo kukubaliwa mahakamani, NEC itawaamuru CCM kufanya hivyo kwa kuwaongezea muda.

"Sasa kwa vile sheria inasema NEC itawaongezea muda wa kuteua mgombea mwingine, mimi nashauri wakateua kabisa mgombea mwingine na kumshauri niliyemwekea pingamizi kujitoa, hii itaepusha kupoteza muda pindi pingamizi likikubaliwa, hakuna jinsi," alisema Bw. Mhozya.


Alisema yeye anahofia zaidi mustakabali wa nchi na vizazi vijavyo kuliko anavyohofia maisha yake, hivyo pamoja na vitisho anavyopata bado hataogopa kusimamia ukweli na kuwafichua waovu kama anavyofanya.

"Nimetoka mahakamani leo (jana), nilikwenda kuwaona makarani wa wanipatie 'samansi'(hati ya kuhudhuria mahakamani iliyo na tarehe ya kusikilizwa kesi) lakini walisema bado haijatoka naamini itatoka hivi karibuni ili tukasikilizwe. Matatizo yapo na nilikwisha yazoea," alisema Bw. Mhozya.
 
Bravo bwana Mhozya, nafikiri katika Watanzania 30m wenye upeo wewe umeliona hili, asante sana
 
Part of mafioso plot ?? (Referring yule kigagula aliesema hakutakuwa na uchaguzi mwaka huu)
 
sio hilo tu ..pia ashitakiwe kwa kuwaficha wezi wa mabilioni ya EPA, sheria gani inayoruhusu mwizi arudishe tu pesa alizoiba then basi.?

what abt meremeta...? what abt richmond ...?the list is endless...!

SAY NO TO KIWETE...! ENUF IS ENUF..!
 
Wrong stepping. Kazi ya kumuengua mgombea ni ya Tume ya Uchaguzi na si mahakama.
 
Kumbe sio Mtikila peke yake anayeyaona haya na kuyasema hadharani hata kama kwa kufanya hivyo kutahatarisha pumzi yake?
Congrats.
 
Safi sana mzee kwa kutukomboa sisi tusiojua namana ya kutumia haki zetu kwa kutokujua hata katiba inafananaje, wala sheria za nchi hii zinasemaje juu ya haki za raia. Kama kweli uraisi si jambo binafsi, iweje kikwete aseme et alimtuma mtoto wake kumtafutia wadhamini kwa sababu eti ni jambo la kifamilia. Bravo Mhozya tupo tunakuunga mkono. Ule utabiri wa nabii Isaya kuhusu Taifa la Tanzania unaweza kutimia mwaka huu. Nabii Isaya anasema Mungu hapendezwi na tabia ya viongozi wachache kutumia madaraka yao kujinufaisha wao na familia zao wakati wananchi waliowengi wanateseka na umasikini uliokithiri, wajane wananyang'anywa haki zao, yatima wanateseka hakuna wakuwaangalia.
:hippie:
 
Tatizo hapa hamna kesi, hatujaonyeshwa sharti lililovunjwa na huyu bwana akiambiwa ahakikishie mahakama ni jinsi gani safari za JK zinafuja mali ya umma ni vigumu sana kuonyesha, hasa kwa sababu ni vigumu kuchanganua kwa uhalisi safari za raisi zinafanya kazi gani hata zile tangible tu, ukiachilia mbali zile intangible ambazo ndiyo kabisa kuzi quantify ni vigumu.

System yenyewe haina transparency, evidence yote iko classified hata ile isiyostahili, rais yuko juu ya sheria halafu yeye ndiye anayechagua majaji wote na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi. Unategemea nini ?

Kesi inaweza kuburudisha watu, kuonyesha watu walivyochoka na kutoa msukumo wa kumpinga JK, lakini haina legal merit.

Legal merit, which is quite different from merit period. The law is an a.s.s.

It is not what happenned, it is what you can prove happenned.
 
Tatizo hapa hamna kesi, hatujaonyeshwa sharti lililovunjwa na huyu bwana akiambiwa ahakikishie mahakama ni jinsi gani safari za JK zinafuja mali ya umma ni vigumu sana kuonyesha, hasa kwa sababu ni vigumu kuchanganua kwa uhalisi safari za raisi zinafanya kazi gani hata zile tangible tu, ukiachilia mbali zile intangible ambazo ndiyo kabisa kuzi quantify ni vigumu.

System yenyewe haina transparency, evidence yote iko classified hata ile isiyostahili, rais yuko juu ya sheria halafu yeye ndiye anayechagua majaji wote na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi. Unategemea nini ?

Kesi inaweza kuburudisha watu, kuonyesha watu walivyochoka na kutoa msukumo wa kumpinga JK, lakini haina legal merit.

Legal merit, which is quite different from merit period. The law is an a.s.s.

It is not what happenned, it is what you can prove happenned.




NDG Kiranga ujue sheria haipo juu ya MUNGU, huo ndio mwanzo tu wa mpango wa Mungu kuikomboa nchi hii kutoka kwa utawala huu, MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Tatizo hapa hamna kesi, hatujaonyeshwa sharti lililovunjwa na huyu bwana akiambiwa ahakikishie mahakama ni jinsi gani safari za JK zinafuja mali ya umma ni vigumu sana kuonyesha, hasa kwa sababu ni vigumu kuchanganua kwa uhalisi safari za raisi zinafanya kazi gani hata zile tangible tu, ukiachilia mbali zile intangible ambazo ndiyo kabisa kuzi quantify ni vigumu.

System yenyewe haina transparency, evidence yote iko classified hata ile isiyostahili, rais yuko juu ya sheria halafu yeye ndiye anayechagua majaji wote na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi. Unategemea nini ?
Kesi inaweza kuburudisha watu, kuonyesha watu walivyochoka na kutoa msukumo wa kumpinga JK, lakini haina legal merit.

Legal merit, which is quite different from merit period. The law is an a.s.s.

It is not what happenned, it is what you can prove happenned.

Mkuu hilo linajulikana tunasubili tu mahakama itamke kwamba nayo hii ni kesi ya kisiasa, tumeiozea!
Lakini Bravo kwa huyu mzee, umefanya vyema.. kwani kwa sasa Tanzania ilikuwa imefikia hatua ya kwenda kisangoma sangoma hasa baada ya shekh Yahaya kuwatishia nyau waliokuwa na nia ya kumpinga JK kwamba watakufa! na kweli wote wakaogopa! Kwa mzee kama huyu kuamua kabisa kumfungilia kesi halali.. ni hatua njema kabisa ambayo japo haita fika mbali lakini itasikika na itaendelea fungua masikio ya walio wengi.
 
Sawa namtakia kila la kheri ila niseme ataweka historia. Kwa UFUPI anapoteza muda hakuna kitu hapa. Najua sitaeleweka ila ndio hivyo.
 
Kiranga umesema yanayonikera kila siku, huwezi kuwa na NEC yenye meno inayotokana na rais mwenyewe kuteua, kama Takukuru ilivyo! mfumo wa mahakama ulivyo nk. Hawa jamaa inabidi sasa wawe wanaapishwa bungeni wala siyo rais jamani.

Anyway, kesi ni nzuri ila mwisho wa siku haitakuwa na maana.
 
Tatizo hapa hamna kesi, hatujaonyeshwa sharti lililovunjwa na huyu bwana akiambiwa ahakikishie mahakama ni jinsi gani safari za JK zinafuja mali ya umma ni vigumu sana kuonyesha, hasa kwa sababu ni vigumu kuchanganua kwa uhalisi safari za raisi zinafanya kazi gani hata zile tangible tu, ukiachilia mbali zile intangible ambazo ndiyo kabisa kuzi quantify ni vigumu.

System yenyewe haina transparency, evidence yote iko classified hata ile isiyostahili, rais yuko juu ya sheria halafu yeye ndiye anayechagua majaji wote na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi. Unategemea nini ?

Kesi inaweza kuburudisha watu, kuonyesha watu walivyochoka na kutoa msukumo wa kumpinga JK, lakini haina legal merit.

Legal merit, which is quite different from merit period. The law is an a.s.s.

It is not what happenned, it is what you can prove happenned.

Kazi ni ngumu kuanzisha. Lakini kwa kuwa jamaa keshaanza, nakwambia watajitokeza wengi tu kumuunga mkono na kumsaidia katika mambo ya kisheria na kuweka bayana vifungu vya katiba vilivyovunjwa na Rais alipokuwa madarakani. Tutasikia mengi mwaka huu. Hapo ndo utabiri wa Sheik Yahya utakapotimia, kwamba itaundwa serikali ya mseto, na uchaguzi utaahirishwa. Tusubiri tuone.
 
Tatizo hapa hamna kesi, hatujaonyeshwa sharti lililovunjwa na huyu bwana akiambiwa ahakikishie mahakama ni jinsi gani safari za JK zinafuja mali ya umma ni vigumu sana kuonyesha, hasa kwa sababu ni vigumu kuchanganua kwa uhalisi safari za raisi zinafanya kazi gani hata zile tangible tu, ukiachilia mbali zile intangible ambazo ndiyo kabisa kuzi quantify ni vigumu.

System yenyewe haina transparency, evidence yote iko classified hata ile isiyostahili, rais yuko juu ya sheria halafu yeye ndiye anayechagua majaji wote na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi. Unategemea nini ?

Kesi inaweza kuburudisha watu, kuonyesha watu walivyochoka na kutoa msukumo wa kumpinga JK, lakini haina legal merit.

Legal merit, which is quite different from merit period. The law is an a.s.s.

It is not what happenned, it is what you can prove happenned.

Unasema hamna kesi wakati kesi imekwisha kuwa filed una maana gani? Si usubiri kwanza mentioning and hearing ndipo uweze kubashiri hukumu yake!!
 
Hakuna haja ya kumharibia Rais wetu, Huko nje nasikia amepata kufahamiana na watu wengi sasa nchi yetu inafahamika sana Marekani, hata Obama ameshatujua Tanzania hivyo ataudhamini Tukienda Kukopa, Hakuna wa kutunyima maana tumeshajitangaza vyakutosha kuwa sisi ni aroro apweche. Sasa kama asingeenda hizo safari tungepata wapi wa kutukopesha? Hata hivyo vyandarua vilivyozua kashfa huko Temeke ni matokeo ya Hizo safari hata Bill klinton kaja mpaka Ntwara kuangalia kama matumizi ya fedha zake yameenda sawia au la japo niliona kile kituo cha afya kama changa la macho vile!!!!!!:bowl::bowl::bowl::bowl::bowl::bowl::bowl::bowl::tape:
 
Chukua tano mwalimu, na uongeze kipengele cha afya , JK afya yake ni mgogoro kwani anazimika zimika majukwaani, ushahidi upo.Endeleza mapambano mkuuu,mpaka kieleweke
 
tusitegemee matokeo chanya kwenye kesi hii ............lakini nampa hongera kwa kutubutu na kujaribu kuchukua hatua. wengi wa watanzania tunatabia ya kutochukua hatua hata pale inapowezekana
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom