JK apata mshituko juu ya ongezeko la bei ya vyakula; aagiza serikali kuingilia kati

Hivi wachumi wanaomzunguka ****** pale magogoni wana kazi gan? Dah bora BEN kuliko huyu mtu...hata kiberiti kushusha bei hawawezi kweli?????????????:A S 13::A S 13:


Ba martha nikwambie kuna ki dada pale magogoni kwa jk pale ambako huwa kanampa ushauri wa maswala ya uchumi......nimekasahau jina lakini kapo hivi kafupi na huwa kananyoa kipara mara nyingi....sijui ka nane kale...mimi kwa kukaona tu nikasema alipaswa kuwa muandaa makongamano na semina za hapa na pale au kuwa hata mc kwenyematukiio makubwa pale ikulu maana kanafiti sana au kuandaa booking za ndege za jk .......lakini maswala ya uchumi huyu hawezi kabisa...hata CV yake inaonyesha yaani hakusoma uchumi yaani basi tu.....ndo watu kama haka ka binti jk anategema kupata ushauri na ndio maana anakuja na madudu kama haya.......
 
huyu nae jk akili zake fupi..yaani yeye anaona leo kupanda kwa gharama za maisha, wakati wenye akili waliliona hili mwaka mmoja tu tangu aupate urais(2006), licha ya CDM kumkumbusha lakini wapi....duh nimeamini jamaa alikuwa kwenye usingizi mzito, naona kaamshwa baada ya lile agizo la uingereza kwamba apunguze safari za nje....muheshiwa karibu nyumbani!!

Mtazamo wa Kikwete katika masuala ya uchumi naweza kumlinganisha na Idd Amin kwa hoja moja ya kiuchumi ifuatayo. Idd Amin alipoona hali ngumu ya uchumi na watu wanataka pasa akaagiza kuchapa pesa nyingi ili watumishi na wanajeshi walipwe. Hali kadhalika Kikwete baada ya kuona watu wananja na mfumuko wa bei kupaa anaagiza kusambaza akiba ya vyakula ya taifa kwenye soko ili kushindana na mfumuko wa bei.

Inaonyesha dhahiri mfumo wa uchumi na mambo yanayosababisha mfumuko wa bei hajui ila kujaza zaidi vyakula mitaani. Sidhani kama vyakula vinakosekana mitaani, ila kuna mambo yanayochangia mfumuko huo na hivyo washauri wa mambo ya uchumi hawamsaidii na kesho hao hao watamgeuzia kibao. Kikwete amedanganywa mengi hata kufungua hoteli ndani ya hifadhi ya barabara na kesho yake inabomolewa lakini bado hajifunzi tu.
 
..angekuwa anajitegemea, at least kwa chakula, angejua kuwa huku mitaani mambo ni magumu.

..najua wengine mtaleta hoja ya washauri, lakini huwezi kumdanganya mtu ambaye ana uwezo wa kuhakiki hicho unachomshauri.
 
Huyu mchumi wa ajabu sana.......hayo mahindi atakayoyaachia yataishia kwa BAKHRESSA....nadhani hajui hata maana ya hiyo SGR....ni kwa ajili ya kukimu wakati wa NJAA ambao unakuja....yeye alitakiwa kufanya haya:
  1. Kushusha VAT ya mafuta toka 18% mpaka 10%
  2. Kuondoa VAT kwenye LUKU
  3. Kufuta kodi zote katika sukari inayozalishwa nchini

Ndugu afanye hayo kwa ushauri wa Mkuro?
if you are a fool, you must make a friendship with bright people!!
Kikwete ni mjinga, kaamua kuwa karibu na wajinga!!!
Wajinga hao wameshindwa kutafuta vyanzo vingine vya mapato badala yake wameamua kulea rushwa kwa kuongeza kodi kwenye mishahara na nishati!!!
just take a simple crip of housing taxes .............. eneo hili naweza kudiriki kusema halijaguswa kabsaaaaaaaaaaaaaaa!!!
 
Mchakachuaji,
Rais wetu mgonjwa halafu unaweka heading hiyo. Umetushtua kidogo. Maagizo/ Ushauri wake huo una walakini. Haoni kutokuwa na kodi kwenye mafuta ya taa kunavyochangia uchakachuaji kwenye mafuta mengine?
mkuu hapo me sikubaliani na wewe hivi ushasahau kwamba wale ndugu zetu waliopo vijijini hawana umeme?na nishati yao kubwa ni vibatari na taa zinazotumia mafuta ya taa.hebu tuwahurumie maana bakora walizochapwa zinatosha.
muhimu ni EWURA kufanya kazi yake waache ubabaishaji tatizo rushwa inatumaliza nchii hii.
 
Navyo fahamu, Rais wetu alishawahi kuwa waziri wa fedha,alishakuwa pia waziri wa nishati, nilitegemea wizara alizozipitia zingefanya vizuri katika uongozi wake, kwa kuwa anazifahamu vizuri. lakini naona ndo zinaongoza kwa kufanya vibaya. alishakuwa pia waziri wa mambo ya nchi za nje, je Rais wake alikuwa anasafiri hivyo kama yeye?
Lazima tukubali sasa kuwa tuna Rais tatizo.
 
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, ameshtushwa kupanda kwa bei ya vyakula na gharama za maisha mijini.Kutokana na hali hiyo, Rais Kikwete ameagiza chakula cha akiba cha taifa kuingizwa katika masoko ya mijini hasa jiji la Dar es Salaam mara moja ili kupunguza bei ya chakula katika masoko ya miji na kupunguza makali na gharama ya maisha kwa wananchi.<br />
<br />
Rais Kikwete ameagiza kuwa kazi hiyo ya kuingilia soko na kupunguza bei ya chakula kwa wananchi iwe kazi ya nyongeza na ya kudumu ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika pamoja na Wakala wa Akiba ya Chakula ya Taifa (NFRA).<br />
<br />
Amesema kuwa miji ya Tanzania ina masikini wengi na malalamiko makubwa ya masikini hao ni bei kubwa ya chakula na kuwa ni wajibu wa Serikali kuchukua hatua za makusudi kuwapunguzia wananchi gharama hizo za maisha kwa kuingiza chakula cha bei nafuu katika masoko ya mijini.<br />
<br />
Rais alitoa maagizo hayo wakati alipotembelea maghala ya NFRA mjini Dar es Salaam kama mwendelezo wa ziara zake na Wizara mbalimbali na taasisi za wizara hizo.<br />
<br />
Rais Kikwete amesema kuwa kama hatua za kuingilia soko zingechukuliwa tangu Oktoba mwaka jana wakati bei ya mahindi ilipokuwa sh. 300 kwa kilo mjini Dar es Salaam, bei hiyo isingepanda na kufikia sh. 430 kwa bei ya sasa. <br />
<br />
“Hii ndiyo kazi yetu kuanzia sasa yaani kuhakikisha kuwa tunaingilia soko, kuingiza chakula cha kutosha na hasa mahindi kwa sababu hiki ndicho chakula kikuu cha Watanzania na kuhakikisha kuwa tunaishusha bei hiyo ya mahindi hadi sh. 300 katika kipindi kifupi iwezekanavyo,” Rais amewaambia maofisa wa Wizara na Wakala huo.<br />
<br />
Amesema kuwa lazima viongozi waelewe kuwa hata mijini kuna upungufu wa chakula. <br />
<br />
“Tafsiri ya njaa ni kama mji haupati chakula cha kutosha basi kuna njaa, Hivyo tujipe mamlaka ya kuingiza haraka soko ili kuwalinda wananchi kwa sababu hatuwezi kuwaacha wananchi mikononi mwa wafanyabiashara binafsi wa chakula ambacho kichocheo chao kikubwa ni faida,” amesema Rais Kikwete.<br />
<br />
Amesema hiyo sasa ni kazi yao ya kila siku yaani kufuatilia masoko na kuhakikisha kuwa kinakuwepo chakula cha kutosha kupunguza bei. <br />
Amewaagiza viongozi kucheza na soko la Dar es Salaam ili kuhakikisha kuwa bei zinakwenda chini haraka iwezekanavyo.<br />
<br />
Amesema kuwa siyo busara kwa mahindi kubakia maghalani kusubiri njaa wakati bei za vyakula zinapanda sana. Nyie mna wajibu wa kulilisha taifa hili.<br />
<br />
Source: Dar leo<br />
My take ina maana yeye anakaa tu magogoni bila kujua changamoto zinazowakabili wananchi wake? huyu baba Rizione One day yes
<br />
<br />
Hii mada mahali pake ni kule kwenye biashara. Hapa wengine wanatukana na kukejeli bila kujadili kilichosemwa.
Kwa ujumla kuingiza chakula cha hifadhi kwa lugha nzuri ni kuwa serikali imetangaza kusubsidizy chakula. Hii ina athari kubwa saana kwa serikali yenyewe, wafadhili na wakulima.
Mazao yanapouzwa kwa bei kubwa inamaana mkulima yule anaelima kwa mikakati na yeye ananufaika. Lakini km kikifika kipindi cha mkulima kunufaika basi bei inapunguzwa, vipi kuhusu mahitaji ya kilimo? Hawa jamaa wamekuwa wakijinadi kutoa ruzuku kwa wakulima lakini ruzuku zile hazitoshelezi chochote. Pia hii dhana ya kusubsidizy wananchi wa Dar (sawa ndio soko kubwa) wale ambao mahitaji kwao si chakula hasa watu masikini wananufaika vipi?
Hoja ya serikali kutoa ruzuku kwa lugha nzuri ni tete. Nchi yetu ni km boarderless inamaana kuna conrtol za namna gani kuzuia mazao haya yasiuzwe nje na kuhakikisha mkulima anaendelea kunufaika na kilimo chake pale akitaka kuuza nje. Iliwahi kunukuliwa kuwa, wakulima wa Rukwa wanaomba kuuza mazao yao Malawi kwa kuwa hayanunuliwi na yanawaozea.
Pia sera ya ruzuku kwenye chakula si sera ya wafadhili, nchi imejiandaaje kupambana na hili wakati bajeti yetu ni tegemezi?
Suluhisho la mfumuko wa bei ni kuongeza uzalishaji wa chakula na kuhakikisha kuna miundombinu ya kueleweka huku pia tukivutia uwekezaji kwenye kilimo.
 
Wewe unapenda sana chai.
jiulize umeifanyia nini serikali na siyo ikufanyie nini?[/QUOTE]

Mkuu huo msemo huo kwenye red ulipata umaarufu sana pale hayati J.F.Kennedy rais wa zamani wa Marekani alipoutumia kuwauliza vijana wa Marekani.Lakini siyo kwamba ndiyo uko-applicable everywhere everyday,kwa kuwa hata wakati Kennedy anasema hayo bado serikali ilikuwa na majukumu yake inayotimiza kwa raia!!!

Kama raia tuna wajibu wetu lakini tuna haki zetu pia na moja ni kuiuliza na kuikosoa serikali iliyopo madarakani tunapoona haitendi kulingana na taratibu na sheria ambazo zinaipasa itende.
 
Mtazamo wa Kikwete katika masuala ya uchumi naweza kumlinganisha na Idd Amin kwa hoja moja ya kiuchumi ifuatayo. Idd Amin alipoona hali ngumu ya uchumi na watu wanataka pasa akaagiza kuchapa pesa nyingi ili watumishi na wanajeshi walipwe. Hali kadhalika Kikwete baada ya kuona watu wananja na mfumuko wa bei kupaa anaagiza kusambaza akiba ya vyakula ya taifa kwenye soko ili kushindana na mfumuko wa bei.

Inaonyesha dhahiri mfumo wa uchumi na mambo yanayosababisha mfumuko wa bei hajui ila kujaza zaidi vyakula mitaani. Sidhani kama vyakula vinakosekana mitaani, ila kuna mambo yanayochangia mfumuko huo na hivyo washauri wa mambo ya uchumi hawamsaidii na kesho hao hao watamgeuzia kibao. Kikwete amedanganywa mengi hata kufungua hoteli ndani ya hifadhi ya barabara na kesho yake inabomolewa lakini bado hajifunzi tu.

Na asisahau mwaka huu kanda ya ziwa hakuna kabisa chakula. atagawa chakula chote mpaka wahanga wa ukame watakosa. hali itakuwa tete sana kanda ya ziwa. akijisahau chakula akawapelekea wakwere kwa kuwa anataka kuwapa unafuu wa maisha, huku usukumani hakuna kabisa mvua, hapo itakula kwake.
 
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, ameshtushwa kupanda kwa bei ya vyakula na gharama za maisha mijini.
Huyu jamaa yeye ni kushituka tu utadhani anaishi dunia nyingine, nadhani anajifanya haya matatizo ni mapya na ameyagundua katika hizi ziara zake , hapo anataka ku win mind za waswahili ili waone kawasema kweli say bandari, elimu etc wanajifanyia mambo bila yeye kujua etc. usanii huu sijui kama tutafika ngoja tuwaachie uvsisiem wajaribu tukiwa tunaangalia jahazi linakoelekea.
 
Hivi ule mradi wa kukataa mashangingi wa WM Pinda umeishia wapi?

Njia muafaka ni kuuza MASHANGINGI YOYE ya serikali na kununua Volkswagen Passat haya ndi yanafilisi uchumi wetu na yanatumika kwa maslahi binafsi ya wakubwa na familia zao.
 
Mbadala wa mapato haya?

1. Dowans - >90bil
2. Meremeta - Unknown
3. Radar - Unknown
4. Ndege ya rais - Unknown
5. Mashangingi - Faida yake ni ipi?
6. Mabilion yanyopotea kila siku kwenye mikataba ya kizembe
7. Mabilion ya malipo ya wafanyakazi hewa kila mwaka
8. Mabilion ya miradi isiyo na tija na ikiishia kufa baada ya mda mfupi
9. Mabilion yanayochotwa benki na kuwekwa kwenye kampeini za siasa mf. Mama Salima budget ipi hugharamia safari zake na magari ya serikali anayotumia
10. Mabilioni yanayopotea kila kila siku kwenye halmashauri, hizi ni kodi za watanzania wanolia leo hii - Serikali ina taarifa, nini kinafanyika
11..........
12..........
13.............
14................

Z..............................................................................................................................................
 
Hapo ndipo tunapoona upeo wake mdogo wa kufikiri.Yeye anadhani tu kuingiza chakula cha akiba ndio kutapunguza mfumuko wa bei.Kuna factors nyingi sana zinachangia,mfano bei ya mafuta.Mfumuko wa bei unachangiwa zaidi na bei ya mafuta.Akiweza kudhibiti bei ya mafuta,mfumuko na utapungua.Lakini kwa sababu hana hata idea hizi,basi tujue tu inakula kwetu kwa sana tu mpaka 2015.Inatia huruma kuwa na kiongozi ambaye ana mawazo duni kama huyu wa sasa.

Nafikiri tunaopaswa kuwakalia kooni ni hao washauri wake wa uchumi. Nashindwa kuelewa wanamshauri kitu gani hao mbu**** kenge hawa, yaani leo ndo wamempa taarifa za nini kinaendelea huko kwenye masoko? Aibu!! Wasomi wetu jamani mnatia aibu ninyi!!!
 
Huyu jamaa yeye ni kushituka tu utadhani anaishi dunia nyingine, nadhani anajifanya haya matatizo ni mapya na ameyagundua katika hizi ziara zake , hapo anataka ku win mind za waswahili ili waone kawasema kweli say bandari, elimu etc wanajifanyia mambo bila yeye kujua etc. usanii huu sijui kama tutafika ngoja tuwaachie uvsisiem wajaribu tukiwa tunaangalia jahazi linakoelekea.

Akili ya Kikwete ni kumaliza akiba ya chakula ya taifa kipindi cha mavuno ambapo chakula hupatikana kwa wingi, je, kitakapokuja kipindi cha njaa na akiba ya chakula ya taifa amemaliza atafanya nini?
Nadhani atapata kisingizio cha upungufu wa chakula ili aendeleze safari zisizoisha kupitisha bakuli kuomba chakula kutoka mataifa mbalimbali ambapo matumizi ya safari yake yatakuwa zaidi ya chakula atakachokwenda kukopa. Mzigo kwa walipa kodi.
 
Mungu wangu ! Si nyie mliniambia ati huyu jamaa ana digree ya Uchumi chuo kinuu ? Je ni kweli au utani ???
 
Hapana...unaposhusha kodi bei hupungua na watu hufanya manunuzi zaidi....kutokana na unafuu wa bei...watu watanunua zaidi(in terms of volumes) na wigo wa kodi kupanda....simple economics...kwa vile VAT sio production cost

Hii falsafa bado ni ngumu kwa JK plz can you make it more simple.........................I dont think if he is aware that VAT is not part of production cost....
 
Kumbukeni hizi statement.............................


  1. Sijui kwa nini watu wa Tanzania ni maskini..........
  2. DOWANS siwajui na wala sitaki kuwafahamu...
Kwa haya simshangai JK kwa kusema kuwa alikuwa hajui kuwa maisha ni magumu na bidhaa muhimu zimepanda bei sana...........Inaonekana mambo mengi anastuliwa kama msinziaji..........
 
Haaa haaa haaaa!! Mwenzenu msiniumize mbavu bure!!!!

Eti Jakaya Kikwete kapatwa na MSHTUKO juu ya kupanda kwa gharama ya maisha nchini; eeehheeeee ndio tuseme kawasili lini huko kutoka Ughaibuni au kwenye sayari nyingine huko katika Taifa la Kusadikika???

Jamani kwa hili wananchi kute nchini kwa sauti moja tunasema CHADEMA asanteni saaaaaaaaaaaaaaaana kwa namna ambavyo maandamano yenu hivi sasa yaanza kutunufaisha kwa kutekelezwa kwa maagizo yenu hatua kwa hatua nchini.

Chonde tungeeni moto huo na elimu zaidi juu ya haki zetu kote nchini; mijini na vijijini ili tuelewe fika namna ya kuwashika hawa mafisadi kuwajibika kwetu kwa wakati na namna tupendavyo sisi.

Hakika kumbe lugha ya maandamano ndioyo pekee lugha inayoeleweka kwa serikali ya kifisadi chini ya Kikwete.
 
Kikwete alipoamrisha kushusha bei ya sukari alichunguza kwanza kinachosababisha sukari kupanda bei?
Kama sukari imepanda bei viwandani, retail merchandize itashushwa bei kwa utaratibu upi?
Je alisha waamrisha VAT kupunguza kiwango cha kodi ya uzalishaji pamoja na mengine yanayosababisha mfumuko wa bei ili sukari iteremke bei?
Kwani ni kiinimacho tu.
 
Back
Top Bottom