JK anawaonaje 'Red Shirts' wa Thailand wanaodai haki?

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233

Ukifuatiliua vizuri historia ya Thailand utaona kuwa hali iliyofikiwa sasa hivi inatokana na uminywaji wa haki wa muda mrefu uliofanywa na watawala mbali mbali, hali ya rushwa kubwa (grand corruption) iliyoshamiri kutokana na vyombo husika kuchukua hatua stahili.

Hali hii imeleta tofauti kubwa ya maisha kati ya 'walionacho' na 'wasionacho', huku 'walionacho' ndiyo wameendelea kushika dola kwa kutumia wakala (aka vibaraka) wao waliowaweka madarakani.

Kinachoendelea sasa hivi ni upande wa 'wasionacho' kuona 'sasa imetosha' kwani kujikomboa kwa njia za halali za kidemokrasia imekuwa vigumu kutokana na ukweli kwamba dempokrasia hiyo imekuwa ni uharamia tu kwani hufanyika katika mazingira ya rushwa kubwa kutoka kwa wachache 'walionacho' hivyo kujinyakulia ushindi kila mara.

Mazingira haya ya demokrasia ndiyo yanaonekana hapa Tz ingawa pengine itachukua muda mrefu hadi nchi kupata 'Red Shirts' wake. Nina hakika kuna baadhi katika utawala wa CCm wanaelewa hivyo ingawa wengi bado hawaoni mbali -- wanaona mwisho wa pua zao tu.

Ninachojiuliza ni kwamba hivi utawala wa JK, na hasa JK mwenyewe anawaonaje wale Red Shirts? Anawaona ni kundi dogo tu la wahuni ambali haliwawakilkishi watu wowote?
 
jina lako la 'kafirbangi' haliendani kabisa na uzito/ukweli/unyeti na hoja uliyoitoa.
Ni kweli JMK na wenzake kina Makamba na Chiligati kama wanataka kupona wajifunze katika hili la RED SHIRTS. Umma ukisema 'sasa inatosha', risasi za moto alizojivunia Mkulu wakati anaongea na 'wazee wa Dar' hakika hazitafua dafu!!! The time is so near!!
 
jina lako la 'kafirbangi' haliendani kabisa na uzito/ukweli/unyeti na hoja uliyoitoa.
Ni kweli JMK na wenzake kina Makamba na Chiligati kama wanataka kupona wajifunze katika hili la RED SHIRTS. Umma ukisema 'sasa inatosha', risasi za moto alizojivunia Mkulu wakati anaongea na 'wazee wa Dar' hakika hazitafua dafu!!! The time is so near!!

Asante Mkulu, tuko pamoja. Jina hilo lisikupe tabu, for 'what's in a name?' Humu JF kikubwa ni hoja, siyo utumbo.
 
Hatuna bado well developed miidle class kama kule Thailand. Watu wetu mablanketi mazito mno na utawala wa CCM wanalifahamu hivyo. Lakini ikos siku, maana ...kimya kikuu huwa kina mshindi mkuu. Inatia moyo kuna wachache katika uongozi wa CCm wameanza kulibaini hilo. Ni mwanzo mzuri, kwani haiwezekani wote wakawa vipofu!

Hata hivyo, hii topic haijatulia hapa, siyo mahala pake. Naomba Mods aihamishie jukwaa la Siasa.
 
Asante Mkulu, tuko pamoja. Jina hilo lisikupe tabu, for 'what's in a name?' Humu JF kikubwa ni hoja, siyo utumbo.

Kama ulivyoelezwa hapo juu,jina lako na vitendo vyako vya kuvuta bangi usingepaswa kuzungumzia jambo zito kama hili.Kutokana na hali yako hata hukusema cha maana "Walio nacho........wasionacho......".Nani hao huko Thailand.
Kubwa unalolitaka ni kutumia kituko cha Thailand kushawishi watanzania.Hata hivyo watanzania walio wengi hawako kama wewe na hao waThailand.
Huoni hata hizo mbinu zao za kibangi bangi hazijawavutia watu na sasa wanazidi kusambaratika.
 
Kama ulivyoelezwa hapo juu,jina lako na vitendo vyako vya kuvuta bangi usingepaswa kuzungumzia jambo zito kama hili.Kutokana na hali yako hata hukusema cha maana "Walio nacho........wasionacho......".Nani hao huko Thailand.
Kubwa unalolitaka ni kutumia kituko cha Thailand kushawishi watanzania.Hata hivyo watanzania walio wengi hawako kama wewe na hao waThailand.
Huoni hata hizo mbinu zao za kibangi bangi hazijawavutia watu na sasa wanazidi kusambaratika.

Inaonekana hujui yale yanayotokea Thailand, na hasa historia yake ya miongo ya karibuni. Bila shaka hufuatilii kwa karibu sababu ya kutokea kwa hali hiyo. Inashangaza katika enzi hizi za satellite TV na Internet, kuna wengine bado wako gizani kweli kweli. Lakini nadhani watu kama wewe huwa mnajisikia vibaya (kwa hofu) misuguano kama hiyo inapotokea katika sehemu nyingine za dunia, na huwa ni jinamizi kufikiria itokee hapa.

Hata hivyo huklo Thailand bila shaka watawala watashinda tu kwa sababu wanazo, chini ya himaya yao, nguvu za dola – na si wananbchi. Narudia tena – soma vizuri historia ya karibuni ya nchi hiyo.

Narudia kusema‘Walionacho' ni wale katika tabaka la juu linalotawala wakishirkiana na maswahiba wao wa kibiashara.

Katika Thailand, tabaka hili pia linbajmumuisha vyombo vya usalama na ulinzi (jeshi, polisi) na pia, kibaya zaidi mahakama, chombo kinachotegemewa katika kutoa haki.

Kwa hiyo wananchi waliko wengi hawana mahala pa kukimbilia, kisiasa, kiuchumi, na hata kisiasa, kwani wenye pesa ndiyo wameshika hatamu. Kwa mfano, serikali ya sasa ya waziri Mkuu Abhisit Vejajiva iliingia madarakani kmwa nguvu za mahakama, na wananchi wengi waliamini hiyo ilifanyika kwa nguvu za ‘walionanacho' ili kukidhi matakwa yao.

Sijasema kuwa Tanzania imeshafikia hatua iliyofikiwa Thailand, la hasha, lakini ingefaa watawala wetu wakaiona hali hiyo na kuangalia iwa;po nasi hapa tunakwenda sawasawa. Nina hakika kwamba tukikuacha wewe na wengine wachache wanafaidi keki ya taifa chini ya CCM, wananchi wengi wanaona hatuko katika right trajectory – both politically and economically.

Ni rahisi kuwa-dismiss watu wanaodai haki kuwa ni wavuta bangi, kwani hiyo ni kauli ya kawaida kutoka kwa watawala, lakini ni sahihi pia kusema hata watawala nao bila shaka hulewa bangi, kwani wanaonekana kulewa sana madaraka na kusahau wamasikini walio wengi.
 
Back
Top Bottom