JK amteua Prof. Idriss Bilali Mshoro kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya TIRDO

My Fellow Tanzanians We have just enough religion to make us hate, but not enough to make us love one another ?

So what if the person is a Muslim can't do a job? Is he not Educated? We have to STOP THIS!!!
 
Najua kuwa ndiye mwenyekiti bodi VETA pia. Prof Mshoro sio Mzanzibari kama mwana jamvi mmoja alivyosema. Nadhani ni mtu wa Tabora (MNYAMWEZI). Amenifundisha chuo kikuu cha DSM mwaka wa nne Faculty of Engineering somo la Material Handling and Design.

Ni kati ya Maprof. ambao ni very knowledbgeble (He is very bright) kwenye mambo ya engineering. Ninachojua amesomea masters yake urusi na amechukiliwa Phd yake Udsm akiwa supervised na prof. Mshana na Masuha.
 
Mtoa hoja hakuwa na mtazamo wa udini ila mchangiaji mmoja tu na amekemewa vilivyo nadhani ni kibaraka wa CCM
Hapa tunajadili CV na c dini
Hakuna mtu anayeweza kuwagawa watanzania kwa kigezo cha UDINI :A S 465:
 
Kwanza nikupongeze kwa kututoa kwenye kile kiharufu cha udini kilichotaka kuvamia. I hate that big time!
Lakini pia I beg to differ katika hili la u-profesa. TIRDO ni taasisi ya R & D. Sote tunafahamu fika role ya UDSM (FOE na baadae CoET) katika research and development ya viwanda hapa nchini. Nina ujasiri kusema taasisi za kitaaluma kama CoET na DIT ndizo zilizo mstari wa mbele katika suala zima la tafiti za maendeleo ya kiviwanda hapa nchini. Huko ndiko chimbuko la Prof Mshoro. Katika taasisi yeyote ya kitaaluma wale wanaojitokeza katika exellence hutunukiwa kuwa maprofesa. Ni mchakato mrefu na si rahisi sana kuchakachua. Lakini juu sana ya uprofesa wake,tupo tunaomfahamu kwa utendaji wake kwa sehemu. Hebu asemwe kwa mengine kwa wanaoyafahamu lakini kwa choice ya quality, I would go for people like him if I were the president. By the way ni mwenyekiti wa bodi si mtendaji was hughuli za kila siku za shirika. Hongera prof mshoro.
to me hii ya kusema professor hainiingi akilini coz most of them ni wazee wa nadhari na failures, ndio maana profesa mzima anafuga ng'mbe kinondoni au ubungo

nadhani kuna gap ya kujua kwamba usomi na uprofesa ni tofauti na kwa wenzetu waweza ukawa profesa una degree mbili

i dont think tanzania inahitaji maprofessor kwenye sekta ya maendeleo maana wengine wakuna ni profesa wa algebra anapewa wizara ya sayansi, wakati wizara inahitaji strategist na sio bundi au bookworm
 
akichaguliwa udini acpo chaguliwa hawajasoma wana elimu ya madrasa ndugu zetu hapa hatushindani kula ng****e hapa tunataka m2 anayefaa je huyu hafai


ahsante kaka kwa tusi la "busara". Jk endelea wengine nao "wale" tuwaache walovimbiwa.
 
JF kufilia mbali. Inajadiliwa dini na si hoja! Hebu wekeni na bodi memba tuwaone. Ndio maana watu wanaamini JF imekuwa kijiwe cha chuki na majungu.

Moderators wanapaswa kukemea memberz wanaoendekeza udini,JK akichagua muislamu mwenye vigezo amekosea? Acheni hizo na JK akisema udini unakuwa wanakataa,nakubaliana na wewe.
 
Kuna haja kubwa sana ya kurudisha JKT Tanzania.....wengine tuliopitia kulikuwa na nidhamu na umoja na mshikamano....

Siku hizi watu baada ya kuendelea mbele kimawazo mnarudi nyuma...hizi dini mnazoshupalia sio zetu sisi wamatumbi lakini leo sisi ndio tunajifanya wasimamizi.

Wacheni UPUMBAVU NA FIKRA FINYO ...Mnatia kichefuchefu
 
Vyovyote vile ilimuradi life lisonge,madaraka ya raisi karibu yafanane na ya Mfalme!!?
 
Mtoa hoja hakuwa na mtazamo wa udini ila mchangiaji mmoja tu na amekemewa vilivyo nadhani ni kibaraka wa CCM
Hapa tunajadili CV na c dini
Hakuna mtu anayeweza kuwagawa watanzania kwa kigezo cha UDINI :A S 465:

Akhsante kwa kuwaweka sawa wale walionituhumu kutokana tu na fikra zao kuwaelekeza hicho walichokifikiria wao kuwa na mie nakifikiria hivyo.
 
Wana Jamii forums tuwe tunatoa hoja na kufanya utafiti wa kina kwa habari tunazorusha hapa;mambo ya tabia za kiswahili tuyapunguze.Mada hii tuiache maana sioni umuhimu wake .Watu wazima mnaanza kujadili upuuzi.Naamini nyote ni wasomi mtakuwa mmenielewa.Sihitaji kuchangia katika hili kwani uelewa umekuwa tofauti kati ya waliochangia mada.

Wewe ndiye unayeleta upuuzi kwa sababu ya uchanga wako humu jamvini. Hebu thibitishia jamvi hili ni kitu gani nilichokieleza hapo ambacho ni cha kipuuzi kama unavyodai.

Kwa taarifa yako (nina hakika hujui), ni kawaida ya mwana-JF yeyote anapopata habari yoyote huwashirikisha wanajamvi wengine katika kuijadili habari hiyo positively. Na hicho ndicho nilichokifanya; nimepata habari ya uteuzi huo wa nafasi hiyo kubwa katika mojawapo ya mashirika yetu makubwa, nimewashirikisha wana JF wenzangu kuwapatia taarifa. Na mimi si wa kwanza kuleta habari ya namna hii.
Kwa mfano kuna watu wameeleza wasifu wa Prof. Mshoro kitaaluma na kiutendaji, je huo nao ni upuuzi?

Ni sawasawa tu na mtu anatufahamisha juu ya uteuzi wa waziri fulani labda, au katibu mkuu wa wizara fulani au habari yoyote juu ya jambo fulani iwe nje ya nchi ama ndani ya nchi (kama kweli wewe ni active member wa JF unapaswa kuwa unayajua haya).

Vinginevyo, kama unaona kuna kitu kimekuudhi au nimeenda kinyume na sheria za JF nafasi iko wazi ya wewe kushtaki kwa Mods ili waniadhibu na unapaswa kulithibitisha hilo. Vinginevyo soma hoja za wenzio, chukua unayoona inakufaa isiyokufaa iache. Ukishindwa kabisa tafuta majamvi mengine ama threads nyingine unazopendezwa nazo.
 
Is Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi a full time job? Kwa maelezo hayo chini inaonyesha Mshoro anahama kuotoka Ardhi University kwenda TIRDO!

Wapi palipoandikwa kuwa Mshoro anahama kutoka Ardhi kwenda Tirdo? Wewe ndo umeelewa hivyo, wenzio wengine wote wameelewa inavyopaswa kueleweka.
 
gud for him? ardhi wana walimu wa kutosha?[/QUOTE]

mkuu kabla yake alikuwa prof. IDRISSA KIKULA ambae sasa yupo UDOM, huyu nae ni mzanzibar na anashutumiwa kwa kuweka wanzanzibar wengi kwenye admistration, kuanzia alivyokuwa ardhi hadi asaiv UDOM. kaaaaaz kwel kwel.


Acheni majungu Idrisa Kikula ni mtu wa Iringa tena Mbena kama sikosei pia Prof Mshoro kwao Tabora siyo Zanzibar...majungu na udini hausaidii. Mtu apewe nafasi kwa merit ya sifa alizonazo siyo kwa sababu ya dini kama wengi mnavyotaka wana jf
 
Kama tutaendelea hivi na maswala ya udini basi ni kansa ya aina yake. Nilidhani kitaalauma Prof. Idrissa Bilali Mshoro amekuwa ni chaguo sahihi, sasa kurukia udini ni jambo la kushangaza. JF msiwe jamvi la poor thinking, na simple minds.

Anaendelea kuwa Makamu mkuu wa chuo cha Ardhi; uenyekiti wa Bodi sio full time position.

Nawakilisha.

Msilazimishe watu kuelewa vile mnavyotaka ninyi.
Hapo kwenye red: Hakuna sehemu yoyote niliyotamka kuwa Prof. Mshoro anahama kutoka Ardhi kwenda Tirdo.
 
haya ma upuuzi ya udini yanachosha kwakweli... Aliyesema urafiki ndio kigezo kikubwa (amepatia sana) lakini kama uwezo ungekuwa unazingatiwa urafiki hau-matter kivile. Nyerere alimuweka shemeji yake warioba kuwa waziri mkuu. Siasa za udini tuwaachie wanigeria huko, sisi nchi yetu ina nafasi zakutosha kukidhi ndoto za wengi tu we nye uwezo. Haiwezekani katika kurusha sarafu ukipata 'bichwa' basi wewe unajipendelea kwasababu nawewe unakichwa, ikipata 'mwenge' (tails) ni sawa kwasababu hamfanani ( the difference here of course being that selecting people for important posts is not like coin tossing but the 50/50 analogy is relevant as far as christianity/islam is concerned). Muacheni rais aweke watu anaowaamini, pale watakapo fanya makosa au ikionekana ni wadhaifu ndio wakosolewe na kuawjibishwa katika jamii, vyombo vya habari, kisiasa na ingekuwa vizuri zaidi kisheria. Udini ni upuuzi tuu kwakuwa mwishoe chenge na lowassa wangetetewa kama kusingekuwa na jina aziz kwenye list ya magamba yaliyotolewa (mfano tuu..facts not withstanding).

warioba hakuteuliwa na nyerere kuwa waziri mkuu,jaribu kukumbuka mkuu na kwa ushauri waache wadini wanyukane wenyewe
 
Swali la kujiuliza hapa ni kuwa je kuna umuhimu wa hili shirika kuendelea kuwepo?...madhumuni ya kuanzishwa kwake bado yapo?...hizo research za kuendeleza viwanda bado zipo?.........kama hazipo au kama madhumuni yake yamepotea basi ni vema shirika lingevunjwa au kuwezeshwa ili yale malengo yake yatimizwe......hili la kuangalia uteuzi kwa misingi ya dini halina mantiki kwanimtendaji akiwa mbaya aumivu ni kwa wote bila kuchagua dini.
 
Swali la kujiuliza hapa ni kuwa je kuna umuhimu wa hili shirika kuendelea kuwepo?...madhumuni ya kuanzishwa kwake bado yapo?...hizo research za kuendeleza viwanda bado zipo?.........kama hazipo au kama madhumuni yake yamepotea basi ni vema shirika lingevunjwa au kuwezeshwa ili yale malengo yake yatimizwe......hili la kuangalia uteuzi kwa misingi ya dini halina mantiki kwanimtendaji akiwa mbaya aumivu ni kwa wote bila kuchagua dini.

Akhsante kwa kuchangia kivingine mkuu.
Kwa wengine: Hii ndio aina ya michango tunayoitaka badala ya kulaumu tu mara oh..mleta hoja kaileta kwa misingi ya dini...! Mtu hana hata proof ya anachokiongea.
 
gud for him? ardhi wana walimu wa kutosha?[/QUOTE]

mkuu kabla yake alikuwa prof. IDRISSA KIKULA ambae sasa yupo UDOM, huyu nae ni mzanzibar na anashutumiwa kwa kuweka wanzanzibar wengi kwenye admistration, kuanzia alivyokuwa ardhi hadi asaiv UDOM. kaaaaaz kwel kwel.

jamani hebu acheni ubaguzi akiwa mzanzibar au mnyamwezi mimi naona wote sawa sisi tunachotaka wawe na sifa za kufanya yale majukumu waliyopewa ipasavyo. kuwa dini fulani au kabila fulani nadhani haina maana yyte ktk maendeleo ya nchi yetu.
 
Na nyie chaguaneni huko CDM, si mmejipanga hata kumsafisha EL?

hebe acheni unafiki wa kidini sisi tunachotaka ni mtu mchapa kazi hivyo asijajiwe mtu kwa dini yake au kabila lake au rangi yake. wanajamii pls acheni hii dhambi ya kubaguana kwa udini au ukabila.
 
Swali la kujiuliza hapa ni kuwa je kuna umuhimu wa hili shirika kuendelea kuwepo?...madhumuni ya kuanzishwa kwake bado yapo?...hizo research za kuendeleza viwanda bado zipo?.........kama hazipo au kama madhumuni yake yamepotea basi ni vema shirika lingevunjwa au kuwezeshwa ili yale malengo yake yatimizwe......hili la kuangalia uteuzi kwa misingi ya dini halina mantiki kwanimtendaji akiwa mbaya aumivu ni kwa wote bila kuchagua dini.

Uko sahihi kabisa swali lingine la muhimu kujiuliza je hawa wenyeviti wa bodi responsibility zao ni nini.Are they just not ceremonial position? Uwepo au kutokupowepo kwa hawa wenyeviti na bodi zao kunanufaishaje au kudhoofisha mashirika yetu

Mi nadhani wataalam na wasomi wafanye reserch ya michango , utendaji na majukumu ya hizi so called bodi za mashirika mbali mbali.

Bodis are there but mashirika bado yanaingia kwenye hasara alafu hawa wanabodi hawaulizwi.

Otherwise tumpongeze prof
 
wana JF, Haya mambo ya udini tumekuwa tukiweka mizaha lkn ipo siku tutalia kifo cha kusaga meno! Kwangu mimi nachukua nafasi hii kumpöngeza Prof Mshoro na hasa wazazi wake kwa kuwekeza kwenye elimu. Kwa mji wa Tabora ambao wenyeji wengi wa pale hawakujali elimu dunia na kujishughulisha zaidi na elimu za kiimani. Sikusudii kusema zile imani wengi mnaoziamini tu. Mji wa Tabora ni miongoni mwa miji mikongwe sehemu kubwa ya wakazi wake wana amini dini za kale kama maswezi, migabho nk. Ni nadra sana kupata wasomi wawili wazuri tu kutoka kwenye familia moja kama ya Arehemu Sheikh Mshoro wa pale Mwanza Road. Hawa jamaa Idrisa na ndugu yake yule pamoja na kutoka kwenye familia ya sheikh kwa wanaowafahamu watakubaliana na mimi kuwa walishaasi huo 'uislamu' Prof tumepiga naye maji pale Survey kuanzia Mikoroshoni Bar kwa mama nguruwe hadi Tamarilo pale nyuma penye umaarufu fulani. Mshoro TRA ndiye mmiliki wa baa zote pale zenye jina la RUFITA kuanzia pale Sinza Mori siku hizi maarufu kama Big Ben hadi kule Kinyerezi bila kusahau ile bendi ya Banza Stone, Rufita Connection. Uko wapi udini wa kina Mshoro hapa zaidi ya sisi humu ndani ambao udini ni kwa yule ambaye ni mtu tofauti na dini yako. Tanzania tunaletewa dini nyingine muda mfupi ujao itakuwa na mashabiki wengi ambao hata msahafu wa dini hiyo hawajawahi kuuona na bila shaka kiongozi wa dini atatoka humu JF kama sio Chama cha Magamba!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom