MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 705
Ingelikua nimeambiwa, wala singediriki kuyasema haya, lakini kumbe ni uongo?
Kwanza, JK ametamka jana kwenye kampeni mkoani Kilimanjaro kwamba Serikali imefanikiwa kuwapeleka watumishi 47 wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, kwenda India, Marekani na Israel (ni baadhi tu ya nchi alizotaja...) kusomea uuguzi, nusu kaputi na udaktari wa magonjwa wa moyo, lengo likiwa kuwa na uwezo wa kufanya upasuaji wa moyo hapa nchini.
JK amesema kwamba "hawa ni vijana wadogo lakini ni very bright people", yaani wana uwezo mkubwa. Kudhihirisha hilo, JK amesema kwamba mwaka huu, tayari upasuaji (open heart surgery) umefanyika kwa wagonjwa 258.
Nimewadadisi baadhi ya madaktari wa Muhimbili, wamesema hilo si kweli.
JK anazidi kudhihirisha jinsi yeye mwenyewe na Serikali yake wasivyo makini. Jambo kama hili, la takwimu, unapaswa kuwa na takwimu ZINAZOTHIBITIKA, sio za KUFIRIKIKA!
Kwa mtaji huu, tutarajie Serikali itakayoendesha shughuli zake kwa dhana na hisia, si kwa uwazi na ukweli!
Unataka mabadiliko toka kwa CCM? Hakuna mabadiliko. Ni SI-HASA tu!
Kama bado unaamini kwamba CCM ndicho chama kinachofaa, utakapounguzwa kikaangoni usilalamike hukuonywa.
Siku njema.
-> Mwana wa Haki
Paople's Power! 2010 Hatudanganyiki! Join the Movement for Change NOW!
Kwanza, JK ametamka jana kwenye kampeni mkoani Kilimanjaro kwamba Serikali imefanikiwa kuwapeleka watumishi 47 wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, kwenda India, Marekani na Israel (ni baadhi tu ya nchi alizotaja...) kusomea uuguzi, nusu kaputi na udaktari wa magonjwa wa moyo, lengo likiwa kuwa na uwezo wa kufanya upasuaji wa moyo hapa nchini.
JK amesema kwamba "hawa ni vijana wadogo lakini ni very bright people", yaani wana uwezo mkubwa. Kudhihirisha hilo, JK amesema kwamba mwaka huu, tayari upasuaji (open heart surgery) umefanyika kwa wagonjwa 258.
Nimewadadisi baadhi ya madaktari wa Muhimbili, wamesema hilo si kweli.
JK anazidi kudhihirisha jinsi yeye mwenyewe na Serikali yake wasivyo makini. Jambo kama hili, la takwimu, unapaswa kuwa na takwimu ZINAZOTHIBITIKA, sio za KUFIRIKIKA!
Kwa mtaji huu, tutarajie Serikali itakayoendesha shughuli zake kwa dhana na hisia, si kwa uwazi na ukweli!
Unataka mabadiliko toka kwa CCM? Hakuna mabadiliko. Ni SI-HASA tu!
Kama bado unaamini kwamba CCM ndicho chama kinachofaa, utakapounguzwa kikaangoni usilalamike hukuonywa.
Siku njema.
-> Mwana wa Haki
Paople's Power! 2010 Hatudanganyiki! Join the Movement for Change NOW!