JK alikusudia Kutudanganya, au alidanganywa ili atudanganye?

Mkuu kupeleka bungeni ni suala la kikatiba na lipo wazi kabisa. Alichosisitiza Rais ni kwamba siyo hati ziwekwe mezani tu bali Report ya CAG ipate muda wa kutosha wa kujadiliwa Bungeni.

Jana nimeulizia Report ya CAG yaani general report iliyojadiliwa bungeni nikaelekezwa niende ofisini ama nimtume mtu akanichukulie bila malipo yoyote.

Mtoa mada anasema report zinazotangazwa haziwezi kumfanya mtu kutoa ushauri; ni kweli. wanachoweka pale hasa kwenye magazeti ni sehemu tu ya report yaani Opinion ambayo pale utapata kujua tu kama taasisi imepewa hati safi, ya mashaka ama chafu au mkaguzi alishindwa kabisa kutoa hati (disclaimer). Pale kunakuwa hakuna kitu kinachoitwa management letter ambayo ndiyo inaongelea matatizo ama

Mkuu Kimbunga, hizi ripoti zinapatikana sana, tatizo letu wabongo ni hodari wa kulalamika na kulaumu! CAG report huwa zinapatikana kirahisi kabisa...mathalani, wakati wa maonesho ambapo wananchi wanakusanyika kwa wingi, hizi ripoti huwa zinatolewa kwa anayezihitaji....tena wanaweka hadi kwenye softcopy(CD)!! Wabongo, hatuna utamaduni wa kusoma....leo hii wanajifanya kuzungumzia ripoti za CAG kufanywa siri! Library zetu vyuo vikuu zinageuka Study Room, na unakuta mtu anaanza first year hadi anamaliza, hajawahi azima kitabu!!!!
 
Dibaji ya CAG inasema hivi: "Kutungwa kwa Sheria ya Ukaguzi wa Umma Na. 11 ya mwaka 2008 kumeongeza mawanda ya ukaguzi wangu kwa kunipa madaraka ya kufanya kaguzi nyingine zaidi ya ukaguzi wa kawaida wa taarifa za fedha. Kwa mujibu wa sheria hii natakiwa kufanya ukaguzi wa ufanisi, utambuzi na mazingira na kaguzi mbalimbali maalum kama zinavyojitokeza. Ni matumaini yangu kwamba, kwa kuanzishwa kwa sheria mpya ya Ukaguzi wa Umma, Ofisi yangu itaweza kuimarisha udhibiti wa fedha na kuisaidia Serikali kuimarisha uwajibikaji. Sheria hii pia itaniwezesha kuwa huru katika kulithibitishia Bunge masuala yanayohusu uwajibikaji, uwazi na matumizi bora ya rasilimali hasa kuona kwamba rasilimali hizo zimetumika vizuri kwa kuzingatia uchumi,ufanisi na kama ilivyotarajiwa na kupitishwa na Bunge."

Bado haitoshi? Hivi nyie wenzangu mnaosema enzi za JK ripoti za CAG zilifanywa siri mnakaa dunia ipi? Mbona hata ilikuwa ukienda pale uwanja wa maonesho (Sabasaba) huwa CD za ripoti ya CAG zinatolewa kama njugu? Tatizo lenu, hamtaki kutafuta habari.....hizi ripoti kwa muda mrefu zinapatikana tena kiurahisi kabisa!

Ni kweli kabisa mkuu CD zilitolewa kama njugu maonesho ya Sabasaba. Ni kweli dibaji ya sheria ya CAG inampa nguvu zaidi ya kufanya ukaguzi wa ufanisi, kumpa uhuru zaidi na kudhibiti matumizi mabaya.

Lakini nadhani hukupata kikalio cha hoja yangu. Mimi nimesema hizo ripoti za jumla zipo, lakini wakati wa utawala wa mkapa CAG alitoa zaidi ya hizo ripoti za jumla. Labda nikupe mfano ili uweze kuelewa tofauti ya ninachozungumza mimi na unachozungumza wewe.

Katika report ya jumla utapata muktasari wa hali ya menejimenti ya pesa kwa Halmashauri ya Kilombero, kwa mfano. Lakini hutapata ripoti nzima ya ukaguzi ya Halmashauri ya Kilombero. Kipindi cha Mkapa, ungeweza kuzipata kwenye tovuti ya CAG au ukiandika barua Kwa CAG anakupatia. Kuanzia 2006 hazijapatikana.

Ili kunidhibitishia kwamba mimi nazusha, naomba niwekee link hapa ya report nzima za ukaguzi aa Halmashauri ya Kilombero, Wizara ya Ujenzi, na Shirika la viwango - TBS. Hizi nimezitoa kama mifano tu

La pili, kwamba sheria mpya imempa CAG mamlaka zaidi ya kudhibiti pesa za umma. Kikalio cha hoja yangu ni kwamba, pamaja na ukweli kwamba idadi ya hati safi imeongezeka, viwango vya ufujaji pia vimeongezeka la wahusika hawajachukuliwa hatua na wanalindwa waziwazi. Hayo ni maneno ya JK mwenyewe kwamba pesa zimezidi kuliwa na walaji amewaita mchwa

Naomba ujaribu kuelewa hoja na kikalio chake kabla hujakurupuka kutetea tafadhali
 
Ila anafanya vizuri hivi tujiulize uhuru anaotoa JK umesaidia sana kufukua mengi kwa kweli japo anachelewa kuchkua hatua.

LAKINI NIMEANZA KUHISI NA KUONA KUWA TUTAMKUMBUKA SANA KWA UHURU HUU NA STYLE YAKE YA KUWAFUMBUA WATANZANIA, HILO HALITAKUWA NA MJADALA SUBIRINI BAADA YA 2015, TENA IKITOKEA MKAFANYA KOSA CCM AWE MEMBE!!!

ILA AKIWA SLAA/ZITTO/MKIRA NAO WAENDELEZE UHURU HUO.

suala la transparency amewin to a great xtent
 
Ila anafanya vizuri hivi tujiulize uhuru anaotoa JK umesaidia sana kufukua mengi kwa kweli japo anachelewa kuchkua hatua.

LAKINI NIMEANZA KUHISI NA KUONA KUWA TUTAMKUMBUKA SANA KWA UHURU HUU NA STYLE YAKE YA KUWAFUMBUA WATANZANIA, HILO HALITAKUWA NA MJADALA SUBIRINI BAADA YA 2015, TENA IKITOKEA MKAFANYA KOSA CCM AWE MEMBE!!!

ILA AKIWA SLAA/ZITTO/MKIRA NAO WAENDELEZE UHURU HUO.

tena anawalazmisha hata wendawazimu wake wawe wawaz
 
Mkuu Kimbunga, hizi ripoti zinapatikana sana, tatizo letu wabongo ni hodari wa kulalamika na kulaumu! CAG report huwa zinapatikana kirahisi kabisa...mathalani, wakati wa maonesho ambapo wananchi wanakusanyika kwa wingi, hizi ripoti huwa zinatolewa kwa anayezihitaji....tena wanaweka hadi kwenye softcopy(CD)!! Wabongo, hatuna utamaduni wa kusoma....leo hii wanajifanya kuzungumzia ripoti za CAG kufanywa siri! Library zetu vyuo vikuu zinageuka Study Room, na unakuta mtu anaanza first year hadi anamaliza, hajawahi azima kitabu!!!!

Sawa mkuu, lakini bado hujajibu hoja yangu. Hebu jaribu kusoma bandiko langu vizuri halafu ulete link hapa inayothibitisha hayo maneno yako
 
inavyoonekana watanzania tunapenda na tunaridhika kusikia maneno mazuri kutoka kwa viongozi wetu wa juu bila kufuatilia na bila kutafakari ukweli wa hayo maneno. hii ni kwa kuangalia comment za wengi humu jf na reaction za watu mitaani baada ya hotuba za hao viongozi esp. JK.
 
The Guadian Newspaper reports today about Kikwete's yesterday speech as follows:

CAG has been given powers to immediately take legal measures against officials proved to have embezzled public funds, he said, adding that he can recommend for the police and Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB) to investigate the culprits even before the report is tabled in Parliament.
 
Ni kweli aliwah kusema,siku aliyopokea hzo taarifa IKULU ndo alimwambia CAG apeleke Bungeni zijadiliwe

Naomba niulize. Kwani sheria inayoisimamia CAG inasemaje? Taarifa za CAG zinatakiwa ziifikie mihimili ipi na katika utaratibu gani.? Je ni nakala moja ya ripoti za CAG inasambazwa kwa mihimili husika au CAG anaruhusiwa kuchakachua ripoti kutegemea na ni kwa muhili upi unaipokea

Mwishoni ni vema kama sheria ingempa madaraka CAG ya kufuatilia upoteaji wa mali za Taifa na uwezo wa kuprosecute na kurecover mali akijiridhisha mali hizo zilifujwa.
 
..mamlaka ya utendaji kazi ya CAG yamebainishwa na sheria ya BUNGE.

..marekebisho ya karibu kabisa kuhusu sheria ya utendaji wa ofisi ya CAG yamefanywa na bunge mwaka 2004, kabla JK hajawa Raisi.

..JK ni muongo anapodai yeye ndiye ametoa mamlaka kwa CAG wakati tunaelewa kabisa mamlaka ya utendaji kazi ya ofisi hiyo yamebainishwa na sheria ya bunge.

NB:

..JK alipokea ripoti ya CAG badala ya kuifanyia kazi akatimka zake kwenda Brazil.

..alipokuwa Brazili na aliporudi akapewa taarifa kwamba ripoti hiyo imeleta mtafaruku bungeni, akadai huo ni upepo tu, akatimka kwenda zake kumzika Bingu wa Mutharika.
 
Katika hotuba yake kwa watanzania kupitia sherehe za Mei Mosi leo, Rais Kikwete amezungumza mengi kuhusu taarifa za CAG na utekelezaji wa mapendekezo ya CAG. Mojawapo ya mambo aliyosema ni kwamba aliagiza CAG aweke taarifa za ukaguzi wazi ili wananchi wazijadili. Sijawahi kusikia hiyo kauli wala waraka unaoelekeza hivyo. Lakini hilo siyo tatizo.

Enzi za utawala wa BWM, idara na Wizara nyingi za serikali ndo ziliwezeshwa kuanzisha tovuti na kuweka taarifa muhimu za serikali. Ofisi ya CAG nayo ilianzisha tovuti yake kipindi hicho, kama ilivyokuwa nyingine, kwa ufadhili wa serikali za nje.

Wakati huo CAG alikuwa akibandika taarifa zote za ukaguzi. Yaani taarifa kuu kama zinazobandikwa sasa (serikali kuu, serikali za mitaa na Mashirika ya umma). Alifanya zaidi, akibandika taarifa za ukaguzi na hesabu za kila Wizara, shirika la umma na kila halmashauri na mkoa. Hakuishia hapo, alitoa nakala zilizosainiwa kwa mtu yeyote (mtu yeyote) aliyeomba nakala ya ukaguzi ya taasisi yoyote ya umma.

Kuanzia mwaka 2006, CAG hajabandika taarifa za ukaguzi za taasisi moja moja na alikataa kutoa nakala za taarifa hizo pale zilipoombwa. Madai yake yalikuwa "Ni maagizo kutoka juu". Pia ukifuatilia taarifa hizo kwenye taasisi husika zimezuiwa kwa maelezo hayo hayo.

Ni vema ikaeleweka kwamba aina ya taarifa anazobandika CAG tangu 2006, hazimuwezeshi mtu kupata picha nzima ya financial management ya taasisi moja moja na hivyo hutaweza kutoa maoni wala kutatua matatizo yaliyopo. Pengine ndiyo maana, kama alivyosema Rais, hati safi zimeongezeka kipindi cha utawala wake, lakini pia amekiri viwango vya ufujaji wa pesa za umma vimepindukia kila ngazi ya serikali.

Swala la pili, Rais amesema aliagiza mjadala wa wazi wa ripoti za CAG bungeni. Hilo niwaachie mpime wenyewe!

Nimeona nitoe maoni yangu tu

Hapo kwenye red kama ni kweli alisema atakuwa kaboronga na inaonesha wazi jinsi mhimili mmoja(serikali) kuingilia shughuli za mhimili mwingine(bunge), sidhani kama katiba au kanuni za bunge zinaruhusu rais kupanga agenda za bunge!
 
Naamini watu wanazidi kufunguliwa; lakini alivyosema kuwa "wananchi wetu hawali mapanki" alikuwa anasema kweli au alidanganywa? Wapo walioamini kuwa aliyosema Rais yote ni kweli na hayahitaji kuhojiwa. sasa hivi watu wanasikiliza halafu kuna mambo wanapuuzia..
 
Swala la pili, Rais amesema aliagiza mjadala wa wazi wa ripoti za CAG bungeni. Hilo niwaachie mpime wenyewe!
Ni kweli ni vigumu kumuamini JK hata pale anapojitahidi kuonyesha kuwa anawajibika. Anapojiosha kuwa mjadala wa bungeni yeye ndiye aliyeushawishi, alimuagiza nani na kwa nini hakuyasema hayo kwa wananchi kupitia hotuba zake au vyombo vya habari? Shinikizo la upinzani na ndani ya chama chake limeanza kumuingia ndio maana anaanza kubwabwaja. Asitudanganye kuwa eti debate zote tena zile zinazosuta serikali yake yeye ndiye anayezianzisha au kuzishabikia.
 
Back
Top Bottom