Indume Yene
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 2,950
- 711
Nimesoma kwenye gazeti la Mwananchi kuwa JK alipokuwa kwenye ziara yake huko Ludewa, kabla ya kupanda kwenye jukwaa alipokea simu kutoka kwa balozi wa marekani nchini Bw. Alfonso E. Lenhardt. JK alidai kuwa balozi huyo alimwambia kuwa Rais Obama aliisifia Tanzania Kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kufuata utawala bora.
Ni vizuri pale Rais kama Obama kutambua uzuri wa taifa letu, lakini inatia shaka kama Obama aliongelea Tanzania kuhusu utawala bora. Nilisikia akiongelea South Africa (From Tyranny to democratic reforms), Congo Kinshasa (Human rights abuse), Kenya (New constitution).
Je wapi Obama aliongelea utawala bora wakati kuna fisadiz wengine bado wanadunda. Je Kikwete alidanganya ili aonekane kuwa ni kiongozi bora na kujiongezea kura? Je ni kweli balozi Alfonso E. Lenhardt alisema hayo wakati Rais wake hakuongelea hiyo mada kwa Tanzania? Nani hapa alidanganya? na kwa nini?
MWANANCHI quotes"Akizungumzia ujumbe aliopewa kwenye simu na balozi wa Marekani nchini, Kikwete alisema kuwa amehakikishiwa misaada kuendelea kumiminika Tanzania kutoka taifa hilo kubwa duniani
"Nilikuwa nazungumza na balozi wa Marekani nchini na amenieleza kuwa rais wa nchi hiyo, Barack Obama akiwa katika mkutano wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa alitolea mfano kuwa Tanzania ni nchi inayofuata utawala bora hivyo wataendelea kutusaidia," alisema Kikwete,
"Maneno haya yanasemwa na Wamarekani sio mimi... watu wanasema tu Marekani, Marekani lakini huo ndio ukweli wenyewe; huo ndio ujumbe niliopata; wameonyesha kutusaidia na watatusaidia,".
Angalia video ujiridhishe. Karibu kwa maoni.
http://www.youtube.com/watch?v=1s7eHoRBqKI
Ni vizuri pale Rais kama Obama kutambua uzuri wa taifa letu, lakini inatia shaka kama Obama aliongelea Tanzania kuhusu utawala bora. Nilisikia akiongelea South Africa (From Tyranny to democratic reforms), Congo Kinshasa (Human rights abuse), Kenya (New constitution).
Je wapi Obama aliongelea utawala bora wakati kuna fisadiz wengine bado wanadunda. Je Kikwete alidanganya ili aonekane kuwa ni kiongozi bora na kujiongezea kura? Je ni kweli balozi Alfonso E. Lenhardt alisema hayo wakati Rais wake hakuongelea hiyo mada kwa Tanzania? Nani hapa alidanganya? na kwa nini?
MWANANCHI quotes"Akizungumzia ujumbe aliopewa kwenye simu na balozi wa Marekani nchini, Kikwete alisema kuwa amehakikishiwa misaada kuendelea kumiminika Tanzania kutoka taifa hilo kubwa duniani
"Nilikuwa nazungumza na balozi wa Marekani nchini na amenieleza kuwa rais wa nchi hiyo, Barack Obama akiwa katika mkutano wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa alitolea mfano kuwa Tanzania ni nchi inayofuata utawala bora hivyo wataendelea kutusaidia," alisema Kikwete,
"Maneno haya yanasemwa na Wamarekani sio mimi... watu wanasema tu Marekani, Marekani lakini huo ndio ukweli wenyewe; huo ndio ujumbe niliopata; wameonyesha kutusaidia na watatusaidia,".
Angalia video ujiridhishe. Karibu kwa maoni.
http://www.youtube.com/watch?v=1s7eHoRBqKI
Last edited by a moderator: