JK ajitahidi kuacha legacy ya kuukomaza upinzani

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,772
Tunapoelekea mwisho wa uongozi wa JK, ni kipi ambacho Watanzania tutamkumbuka kutuachia (legacy)?

Niliwahi kumwandikia JK kwamba lengo la Nyerere kukubali upinzani uanze lilikuwa ni kwa maslahi ya Taifa. Nikashauri kwamba ajitahidi aukuze upinzani japo yeye ni kiongozi wa CCM. Nilisema hata pakiwa na ziara za viongozi wa nje ahakikishe anaweka kwenye ratiba voingozi wa upinzani, vyama vyenye uwakilishi mkubwa bungeni, wakutane na viongozi hao wa nje, awahusishe viongozi wa upinzani katika baadhi ya ziara zake za nje na hata kuwaalika Ikulu kila mara kwa majadiliano juu ya matatizo makubwa ya nchi - kama mgomo wa madaktari, thamani ya shilingi, umeme nk.

Nilisema ajitahidi angalau chama kimoja cha upinzani kitufikishe kama ilivyo Marekani kwa Democrats na Republicans. Nilisema akifanya hivi ataacha CCM na hicho chama cha upinzani vyote vikiwa strong kwa maslahi ya taifa, na yeye akaheshimika sana baada ya kumaliza uongozi wake, nchini na kimataifa.

Tofauti yake, akiwa kama Mkapa, raisi mstaafu na viongozi kama yeye, wakatukana vyama vya upinzani na viongozi wao, wanapaswa kukumbuka kwamba Tanzania pia inaweza kutokea tukawa na raisi na serikali kutoka chama cha upinzani. Wanafikiri watachukuliwaje na raisi waliyemtukana pamoja na chama chake kabla hajachukua madaraka? Hata kwa mtu asiye na hulka ya kisasi, kutoa heshima inayostahili kwa raisi mstaafu aliyetukana wewe na chama chako kabla hamjachukua nchi ni ngumu sana. Wanaweza kujikuta siku moja huko mbeleni hata escort ya polisi hawapati tena na wanafoleni barabarani kwenye traffic kama raia wengine.

Mwana CCM yeyote mwenye akili anapaswa kusikitika akiona watu wanafanya kampeni za kuua vyama vya upinzani nchini. Maslahi ya taifa ndilo lililokuwa lengo la Nyerere kukubali vyama vya upinzani, sasa kwa nini kuwe na harakati za kuua upinzani?

Na ndio maana mwanasiasa yeyote mwenye akili hatatumia matusi juu ya chama kingine.
 
Sure hili ni jambo la kumsifia JK indirectly au diretcly . Lakini Jiuize je JK kweli anapenda iwe hivyo au ni udahifu na mipasuko iliyochochewa na Mtandao.

Iwe ni kwa udhaifu au kwa mapenzi Sometime hata mm nadhani JK was the right man from CCM na kiasi fulani anastahli sifa. Chini ya uongozi wake ameongeza uncertainity Ndani ya CCM kitu ambacho ni nafuu kwa demokrasia.
 
he better be fair that way to rescue hata hiko kidogo kilichobakia ccm....

pia ni vizuri tukampongeza kwa matumizi mazuri ya taasisi yake ya uraisi....he is cultivating the behaviour kuwa upinzani si uadui kama mazionist wengi wa CCM wanavyodhani......

ni vizuri kwa watu wanaoaspire siasa kutambua kuwa siasa si AJIRA!
 
sijaelewa !! 1985 wakati vyama vingi vinaruhusiwa nyerere hakuwa Rais sasa unaposema eti nyerere aliruhusu vyama vingi ndo nilipoacha hata kusoma post yako ...maana unani mislead!!
 
Hebu acheni upuuzi, yaani ustawi wa upinzani inabidi uruhusiwe na raisi???????, guyz are u serious??????? Kwamba raisi ndiyo anaamua kuwe na upinzani mkali kama marekani? raisi anakuza upinzani? raisi ndiyo amekubali Nassari ashinde sio?????? Na hii ndiyo usikute ni mitazamo ya watu wanaoitwa wasomi Tanzania!! Basi tumpe madaraka ya kuamua ni wakati gani tufurahi na wakati gani tunune!!!!!!!!!!!!!!! Kama taifa we have a problem, big problem!!!!!!!!!!!!!!
 
sijaelewa !! 1985 wakati vyama vingi vinaruhusiwa nyerere hakuwa Rais sasa unaposema eti nyerere aliruhusu vyama vingi ndo nilipoacha hata kusoma post yako ...maana unani mislead!!
Hata wewe una tatizo la uwelewa, vyama vingi havikurudishwa mwaka 1985.......bali miaka ya 90.
 
sijaelewa !! 1985 wakati vyama vingi vinaruhusiwa nyerere hakuwa Rais sasa unaposema eti nyerere aliruhusu vyama vingi ndo nilipoacha hata kusoma post yako ...maana unani mislead!!

Kumbuka kwamba katika kura ya maoni (referandum) kwamba tuanze mfumo wa vyama vingi au la, asilimia 80% ya watanzania walisema tuendelee na chama kimoja, na asilimia 20% wakasema tuwe na vyama vingi. Wakati serikali ikielekea kuidhinisha maoni ya wengi wape katika referandum hiyo, Nyerere aliingilia kati akatoa ushawishi kwamba wale wa asilimia 20% wasikilizwe badala ya wale asilimia 80%, kutokana na mazingira halisi ya kidunia wakati huo. Hivyo basi serikali ikaridhia kuanzisha mfumo wa vyama vingi.

Sasa hutasema Nyerere alianzisha mfumo wa vyama vingi japo hakuwa raisi wakati huo?
 
"Sometimes yes,sometimes no!";
kikwete anaweza kutumia udhaifu wake kiuongozi kujenga argument kwamba ameimarisha upinzani!
UONGO ukisemwa sana na kutetewa kwa nguvu zote unaweza kugeuka kuwa ukweli!
 
Wakuu, naona kama JK amesikiliza ushauri wangu ki-namna! Nampongeza sana. Hili ndilo kubwa na la maana sana alilotuachia JK
 
Back
Top Bottom