Bill
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 8,277
- 8,492
...Aikana sera ya maisha bora, Asema si yake, ilikuwapo tangu uhuru
Source: Majira, Monday, 05 October 2009 08:16 Na Mwandishi Maalumu, Mwanza
WAKATI kaulimbiu ya kampeni zilizomweka madarakani Rais Jakaya Kikwete 'Maisha bora kwa kila Mtanzania' ikizidi kuhojiwa na wananchi kama imesaidia kuboresha maisha yao, jana rais huyo ameikana akisema si yake bali ilikuwapo hata kabla ya uhuru.
Taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu ilimkariri Rais Kikwete akiikana sera hiyo kuwa wanaosema ameileta yeye wanabeza, wakati sera hiyo ilikuwapo na itaendelea kuwapo hata baada yake.
Wapo watu wanaobeza kuwa hii sera ya maisha bora imeletwa na akina Kikwete. Sisi tumeendeleza sera ile ile ambayo taifa hili limekuwa linatekeleza tokea uhuru wetu na wala kazi hii haitaishia kwangu mimi, hata wale viongozi watakaonifuata wataendeleza sera hii kwa sababu kazi ya kujenga maisha bora kwa wananchi haihishi, haina kikomo, alisema.
Rais Kikwete alisema kuwa hata kabla ya uhuru, Mwalimu Julius Nyerere alitambua ili uhuru na umoja viweze kudumishwa ni lazima wananchi wake wapate maisha bora na ndiyo maana akawatambua maadui wakuu watatu ujinga, maradhi na umasikini- na njia za kukabiliana na maadui hao.
Rais Kikwete ameyasema hayo mjini Mwanza juzi jioni alipozungumza na vijana wa CCM ambao walioondoka mjini Mwanza jana kwenda Butiama, Mkoani Mara, kwa Matembezi Maalum ya kumuezi Mwalimu kwenye kumbukumbu ya miaka 10 tangu kifo chake, Oktoba 14, 1999.
Vijana 166 kutoka mikoa yote ya Tanzania wanashiriki katika Matembezi hayo ya siku 10 na yatakayopitia njia ambayo Mwalimu Nyerere alitembea mwaka 1967 katika kuunga mkono na kuhamasisha Azimio la Arusha.
Kaulimbiu ya Matembezi hayo ni Uhuru na Kazi na miongoni mwa mambo ambayo vijana hao watafanya njiani ni kukarabati Shule ya Msingi ya Mwisenge ambako Mwalimu Nyerere alipata elimu yake ya msingi.
Rais Kikwete aliwashangaa Watanzania ambao wanabeza uhuru wa Tanzania na kufurahia wakati jina la Tanzania linaposhambuliwa na wageni na kuwasihi Watanzania kuzidi kumuenzi mwalimu.
Wamarekani wale wanaye George Washington sisi tunaye Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kila nchi ina mwasisi wake ambaye anakumbukwa kwa aliyoyasimamia, amesema Mwalimu na kuongeza:
La kwanza la kumkumbuka Mwalimu ni uhuru wa nchi yetu. Huyu alikuwa ni kiongozi aliyeambiwa achague kati ya siasa ama kazi ya ualimu huyu mzee wetu akachagua siasa na utumishi wa umma bila hata kujua atakula nini.
Akachagua kupigania uhuru wa nchi yetu. Kama mnavyojua nyote hii kazi ya siasa ni kamari..unakwenda kugombea ukijua kuna kupata ama kukosa..lakini yeye alifanya uamuzi sahihi wa kupigania uhuru,
Rais Kikwete alisema kuwa uhuru siyo mipaka bali ni heshima ya nchi na ndiyo maana Tanzania haitasita kumkabili yoyote ambaye atajaribu kuchezea uhuru huo.
Kuhusu umoja wa taifa, Rais Kikwete amesema kuwa Mwalimu alihakikisha kuwa uhuru wa nchi unazaa umoja ili nchi iwe moja na isigawanyike vipande vipande kwa sababu yoyote ile.
Aliondoa viashiria vyote vya kuvunja umoja wa taifa tokea mwanzo kabisa. Aliondoa uchifu ili kuondoa nguvu za ukabila. Alitambua hatari ya dini na akataifisha shule zote za dini ili vijana wetu waelimishwe na kulelewa kama vijana wa taifa moja na siyo vijana wa dini tofauti.
WAKATI kaulimbiu ya kampeni zilizomweka madarakani Rais Jakaya Kikwete 'Maisha bora kwa kila Mtanzania' ikizidi kuhojiwa na wananchi kama imesaidia kuboresha maisha yao, jana rais huyo ameikana akisema si yake bali ilikuwapo hata kabla ya uhuru.
Taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu ilimkariri Rais Kikwete akiikana sera hiyo kuwa wanaosema ameileta yeye wanabeza, wakati sera hiyo ilikuwapo na itaendelea kuwapo hata baada yake.
Wapo watu wanaobeza kuwa hii sera ya maisha bora imeletwa na akina Kikwete. Sisi tumeendeleza sera ile ile ambayo taifa hili limekuwa linatekeleza tokea uhuru wetu na wala kazi hii haitaishia kwangu mimi, hata wale viongozi watakaonifuata wataendeleza sera hii kwa sababu kazi ya kujenga maisha bora kwa wananchi haihishi, haina kikomo, alisema.
Rais Kikwete alisema kuwa hata kabla ya uhuru, Mwalimu Julius Nyerere alitambua ili uhuru na umoja viweze kudumishwa ni lazima wananchi wake wapate maisha bora na ndiyo maana akawatambua maadui wakuu watatu ujinga, maradhi na umasikini- na njia za kukabiliana na maadui hao.
Rais Kikwete ameyasema hayo mjini Mwanza juzi jioni alipozungumza na vijana wa CCM ambao walioondoka mjini Mwanza jana kwenda Butiama, Mkoani Mara, kwa Matembezi Maalum ya kumuezi Mwalimu kwenye kumbukumbu ya miaka 10 tangu kifo chake, Oktoba 14, 1999.
Vijana 166 kutoka mikoa yote ya Tanzania wanashiriki katika Matembezi hayo ya siku 10 na yatakayopitia njia ambayo Mwalimu Nyerere alitembea mwaka 1967 katika kuunga mkono na kuhamasisha Azimio la Arusha.
Kaulimbiu ya Matembezi hayo ni Uhuru na Kazi na miongoni mwa mambo ambayo vijana hao watafanya njiani ni kukarabati Shule ya Msingi ya Mwisenge ambako Mwalimu Nyerere alipata elimu yake ya msingi.
Rais Kikwete aliwashangaa Watanzania ambao wanabeza uhuru wa Tanzania na kufurahia wakati jina la Tanzania linaposhambuliwa na wageni na kuwasihi Watanzania kuzidi kumuenzi mwalimu.
Wamarekani wale wanaye George Washington sisi tunaye Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kila nchi ina mwasisi wake ambaye anakumbukwa kwa aliyoyasimamia, amesema Mwalimu na kuongeza:
La kwanza la kumkumbuka Mwalimu ni uhuru wa nchi yetu. Huyu alikuwa ni kiongozi aliyeambiwa achague kati ya siasa ama kazi ya ualimu huyu mzee wetu akachagua siasa na utumishi wa umma bila hata kujua atakula nini.
Akachagua kupigania uhuru wa nchi yetu. Kama mnavyojua nyote hii kazi ya siasa ni kamari..unakwenda kugombea ukijua kuna kupata ama kukosa..lakini yeye alifanya uamuzi sahihi wa kupigania uhuru,
Rais Kikwete alisema kuwa uhuru siyo mipaka bali ni heshima ya nchi na ndiyo maana Tanzania haitasita kumkabili yoyote ambaye atajaribu kuchezea uhuru huo.
Kuhusu umoja wa taifa, Rais Kikwete amesema kuwa Mwalimu alihakikisha kuwa uhuru wa nchi unazaa umoja ili nchi iwe moja na isigawanyike vipande vipande kwa sababu yoyote ile.
Aliondoa viashiria vyote vya kuvunja umoja wa taifa tokea mwanzo kabisa. Aliondoa uchifu ili kuondoa nguvu za ukabila. Alitambua hatari ya dini na akataifisha shule zote za dini ili vijana wetu waelimishwe na kulelewa kama vijana wa taifa moja na siyo vijana wa dini tofauti.