kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
Rais Jakaya Kikwete amezindua harambee ya kuchangia ujenzi wa kituo cha wanafunzi cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), iliyofanikisha kupatikana kwa jumla ya Sh. 1,430,583,000.
Uzinduzi wa harambee hiyo ulifanyika Ikulu juzi usiku jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na watu mashuhuri wakiwemo Mabalozi Alonso Leinhardt (Marekani), Bjarne Sorensen (Denmark), Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu, Mawaziri na wafanyabiashara.
Akizungumza wakati wa harambee, Rais Kikwete alisema: Mimi ni mkereketwa wa elimu na ndio maana sikusita kukubali ombi la Profesa Mukandala (Rwekaza) aliponieleza mpango huu.
Rais Kikwete ambaye aliahidi kuchangia Sh. milioni 10, alisema atakuwa balozi wa kuomba michango kwa marafiki zake na kwamba suala hilo ataliwasilisha kwenye serikali yake ili nayo ichangie.
Kadhalika, aliwasilisha ahadi za marafiki zake ambao waliahidi kuchangia Sh. bilioni moja.
Rais wa wahitimu wa UDSM ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa kituo hicho, Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba, alisema chuo hicho kwa sasa kinakabiliwa na tatizo kubwa la miundombinu zikiwemo nyumba za walimu, ofisi, madarasa na hosteli za wanafunzi.
Alisema ujenzi wa miundombinu hiyo hauwezi kufanikiwa kwa kuitegemea serikali pekee na kwamba mkakati uliopo ni kujenga utamaduni wa kushiriki ujenzi wa vyuo hususani kule walikosoma.
Tumeshakaribia asilimia 20 ya gharama za ujenzi wa kituo hiki, alisema.
Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Rwekaza Mukandala, alisema gharama za ujenzi wa kituo hicho unakadiriwa kuwa Sh. bilioni 17.
Alifafanua kuwa kitakuwa na maeneo ya kupumzika wanafunzi, hosteli, sehemu za michezo, maktaba, huduma za vyakula na benki, ofisi za serikali ya wanafunzi na kituo cha intaneti.
Alisema kwa kuanzia, wafanyakazi chuoni hapo, wamechangia Sh. bilioni 1.2.
Kituo hiki kinajengwa kama kumbukumbu ya miaka 50 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambacho kilijengwa Oktoba, 1961 miezi michache kabla ya uhuru, alisema Profesa Mukandala.
Katika harambee hiyo, Sh. milioni 64 zilikuwa fedha taslimu wakati ahadi ni Sh. 1,366,583,000.
CHANZO: NIPASHE
Uzinduzi wa harambee hiyo ulifanyika Ikulu juzi usiku jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na watu mashuhuri wakiwemo Mabalozi Alonso Leinhardt (Marekani), Bjarne Sorensen (Denmark), Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu, Mawaziri na wafanyabiashara.
Akizungumza wakati wa harambee, Rais Kikwete alisema: Mimi ni mkereketwa wa elimu na ndio maana sikusita kukubali ombi la Profesa Mukandala (Rwekaza) aliponieleza mpango huu.
Rais Kikwete ambaye aliahidi kuchangia Sh. milioni 10, alisema atakuwa balozi wa kuomba michango kwa marafiki zake na kwamba suala hilo ataliwasilisha kwenye serikali yake ili nayo ichangie.
Kadhalika, aliwasilisha ahadi za marafiki zake ambao waliahidi kuchangia Sh. bilioni moja.
Rais wa wahitimu wa UDSM ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa kituo hicho, Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba, alisema chuo hicho kwa sasa kinakabiliwa na tatizo kubwa la miundombinu zikiwemo nyumba za walimu, ofisi, madarasa na hosteli za wanafunzi.
Alisema ujenzi wa miundombinu hiyo hauwezi kufanikiwa kwa kuitegemea serikali pekee na kwamba mkakati uliopo ni kujenga utamaduni wa kushiriki ujenzi wa vyuo hususani kule walikosoma.
Tumeshakaribia asilimia 20 ya gharama za ujenzi wa kituo hiki, alisema.
Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Rwekaza Mukandala, alisema gharama za ujenzi wa kituo hicho unakadiriwa kuwa Sh. bilioni 17.
Alifafanua kuwa kitakuwa na maeneo ya kupumzika wanafunzi, hosteli, sehemu za michezo, maktaba, huduma za vyakula na benki, ofisi za serikali ya wanafunzi na kituo cha intaneti.
Alisema kwa kuanzia, wafanyakazi chuoni hapo, wamechangia Sh. bilioni 1.2.
Kituo hiki kinajengwa kama kumbukumbu ya miaka 50 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambacho kilijengwa Oktoba, 1961 miezi michache kabla ya uhuru, alisema Profesa Mukandala.
Katika harambee hiyo, Sh. milioni 64 zilikuwa fedha taslimu wakati ahadi ni Sh. 1,366,583,000.
CHANZO: NIPASHE