Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
K agoma kusaini sheria mpya
*NI YA KAMPUNI ZA SIMU KUJISAJILI SOKO LA HISA DAR
Ramadhan Semtawa
BAADA ya kusaini Sheria ya gharama za uchaguzi ambayo imegubikwa na utata, Rais Jakaya Kikwete ameshtuka na amegoma kusaini sheria inayobana makampuni ya elektroniki ikiwemo ya simu na posta kujisajili kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).
Habari za uhakikika zimelidokeza gazeti hili jana kuwa Rais Kikwete alikataa kusaini sheria hiyo akitaka Muswada wake ufanyiwe marekibisho katika kifungu cha 26 ambacho pamoja na mambo mengine, kinabana makampuni ya simu kujisajili DSE kwa lazima.
Kifungu hicho tayari kilipingwa na kampuni za simu nchini wakati mjadala huo ukijadiliwa kwenye mkutano wa 18 wa bunge mjini Dodoma, ambako walitaka kilegezwe.
Said Arfi ambaye ni msemaji wa kambi ya upinzani katika mambo ya mawasiliano, sayansi na teknolojia akisoma maoni ya kamati, alipinga vifungu mbalimbali vya muswada huo, kikiwemo kifungu cha 26.
Kwa habari zaidi soma Mwananchi.
*NI YA KAMPUNI ZA SIMU KUJISAJILI SOKO LA HISA DAR
Ramadhan Semtawa
BAADA ya kusaini Sheria ya gharama za uchaguzi ambayo imegubikwa na utata, Rais Jakaya Kikwete ameshtuka na amegoma kusaini sheria inayobana makampuni ya elektroniki ikiwemo ya simu na posta kujisajili kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).
Habari za uhakikika zimelidokeza gazeti hili jana kuwa Rais Kikwete alikataa kusaini sheria hiyo akitaka Muswada wake ufanyiwe marekibisho katika kifungu cha 26 ambacho pamoja na mambo mengine, kinabana makampuni ya simu kujisajili DSE kwa lazima.
Kifungu hicho tayari kilipingwa na kampuni za simu nchini wakati mjadala huo ukijadiliwa kwenye mkutano wa 18 wa bunge mjini Dodoma, ambako walitaka kilegezwe.
Said Arfi ambaye ni msemaji wa kambi ya upinzani katika mambo ya mawasiliano, sayansi na teknolojia akisoma maoni ya kamati, alipinga vifungu mbalimbali vya muswada huo, kikiwemo kifungu cha 26.
Kwa habari zaidi soma Mwananchi.