JK adanganywa tena

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
WIKI chache baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa agizo akitaka uzio wa viwanja vya michezo Jangwani ubomolewe, imebainika kuwa agizo hilo limeshindwa kutekelezeka kwa sababu eneo hilo limeuzwa kwa mwekezaji ambaye ni raia wa China.

Hivyo watendaji wa Halmashauri ya Ilala na Wizara ya Ardhi wanabanwa na masharti ya mkataba unaodaiwa kuingiwa baina yao na mwekezaji huyo.

Imebainika kuwa Rais Kikwete alitoa agizo hilo Aprili 3 mwaka huu baada ya kupewa taarifa potofu na hivyo kutoa amri ambayo haitekelezeki kisheria.

Akiweka jiwe la msingi la upanuzi wa barabara ya New Bagamoyo, eneo la Mwenge-Tegeta, Rais Kikwete aliagiza uzio huo ubomolewe lakini hadi jana hakuna bomoabomoa yoyote iliyokuwa imefanywa katika eneo hilo.

Chanzo chetu kutoka ndani ya halmashauri ya Ilala kilisema mkataba huo umempa mwekezaji huyo haki ya kujenga maghala mbalimbali ‘magodauni', kwa makubaliano kwamba yangeinufaisha pia halmashauri hiyo.

Ilibainishwa zaidi kuwa mkataba huo uliingiwa kibinafsi na baadhi ya viongozi wa Ilala kutokana na tamaa ya fedha huku wakishindwa kuzingatia kuwa eneo hilo ni maalum kwa ajili ya michezo.

Baadhi ya madiwani wamekuwa wakipiga kelele za mara kwa mara kuhusu uwanja huo wa michezo wa Jangwani lakini hakuna hatua zilizochukuliwa hadi sasa licha ya Rais Kikwete kutoa agizo lake.

"Ni vigumu kwa watendaji wa halmashauri hiyo kuvunja uzio huo kwa sababu wao ndio walioshiriki kuingia mkataba huo mbovu.

"Haya ndiyo mambo tunayopigia kelele kila wakati lakini hatusikilizwi maana halmashauri ina wataalam wa ardhi wa kutosha iweje wanashindwa kujua umuhimu wa viwanja vile?" kilihoji.

Kilisisitiza kuwa kutokana na Rais Kikwete kuwa ndiye mhimili mkuu wa dola basi ana jukumu la kuhakikisha maagizo anayoyatoa yanatekelezwa ipasavyo.

Rais Kikwete ametakiwa kuingia na kusimamia agizo hilo binafsi kwa kwenda na kuvunja uzio huo mwenyewe kwani sio rahisi kwa walioingia mkataba kusimamia agizo hilo kutokana na kulinda maslahi yao.

Hadi habari hii inaandikwa uzio wa mabati bado upo ndani ya viwanja hivyo huku wizara ikiitaka halmashauri ya Ilala ibomoe lakini majibu yanayotolewa na halmashauri hiyo ni kwamba wamezuiwa kufanya utekelezaji huo.
 
mimi nadhani hata jk anatuzuga tu, anajua sana eneo limeuzwa hiyo, huyo JERRY naibu meya kwenye baraza lililopita, kama wameuza alihusika moja kwa moja kama mjumbe na naibu meya, na huyo ni mtu wa jk, si unaona magufuli alivyopigwa stop asibomoe mabango hapa DAR , ni bora sisi tufe na moshi wa kwenye foleni na uchumi wetu uporomoke lakini , hawa watu wapate posho, hii ni michezo ya siasa ya JK kujifua lawama kama anavyomfanya EL na RA baada ya kuiba hela na kumuweka mjengoni sasa kawatosa
 
mimi nadhani hata jk anatuzuga tu, anajua sana eneo limeuzwa hiyo, huyo JERRY naibu meya kwenye baraza lililopita, kama wameuza alihusika moja kwa moja kama mjumbe na naibu meya, na huyo ni mtu wa jk, si unaona magufuli alivyopigwa stop asibomoe mabango hapa DAR , ni bora sisi tufe na moshi wa kwenye foleni na uchumi wetu uporomoke lakini , hawa watu wapate posho, hii ni michezo ya siasa ya JK kujifua lawama kama anavyomfanya EL na RA baada ya kuiba hela na kumuweka mjengoni sasa kawatosa
Hata mimi naanza kuona huu ni usanii tunaochezewa na JK kwa kujifanya hajui kitu, inawezekana hata hii issue alijua nini kinaendelea leo ndio anajidai kutoa amri ubomolewe na kuwageuka kama alivyowageuka kina RACHEL.
 

WIKI chache baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa agizo akitaka uzio wa viwanja vya michezo Jangwani ubomolewe, imebainika kuwa agizo hilo limeshindwa kutekelezeka kwa sababu eneo hilo limeuzwa kwa mwekezaji ambaye ni raia wa China.

Hivyo watendaji wa Halmashauri ya Ilala na Wizara ya Ardhi wanabanwa na masharti ya mkataba unaodaiwa kuingiwa baina yao na mwekezaji huyo.
Imebainika kuwa Rais Kikwete alitoa agizo hilo Aprili 3 mwaka huu baada ya kupewa taarifa potofu na hivyo kutoa amri ambayo haitekelezeki kisheria. Akiweka jiwe la msingi la upanuzi wa barabara ya New Bagamoyo, eneo la Mwenge-Tegeta, Rais Kikwete aliagiza uzio huo ubomolewe lakini hadi jana hakuna bomoabomoa yoyote iliyokuwa imefanywa katika eneo hilo.


Wakati Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, akipewa onyo na Rais Kikwete akitakiwa aache ubabe wa kubomoa maeneo ya watu, agizo hilo la Rais limekuwa ni kinyume na maagizo yake mwenyewe kwa waziri wake.
Baada ya agizo hilo la Rais kuonekana halitekelezeki kisheria, hivyo jitihada za makusudi zinafanywa kujaribu kuvunja sheria ili kulinda heshima ya Rais.
Halmashauri ya Ilala na Wizara ya Ardhi katika siku za hivi karibuni zimekuwa zikitupiana mpira kuhusu nani hasa anayestahili kutekeleza agizo hilo la Rais, huku mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Gabriel Fuime, akisema wameambiwa wasubiri kwanza.

Chanzo cha habari kutoka ndani ya halmashauri ya Ilala kilisema mkataba huo umempa mwekezaji huyo haki ya kujenga maghala mbalimbali ‘magodauni’, kwa makubaliano kwamba yangeinufaisha pia halmashauri hiyo.
Ilibainishwa zaidi kuwa mkataba huo uliingiwa kibinafsi na baadhi ya viongozi wa Ilala kutokana na tamaa ya fedha huku wakishindwa kuzingatia kuwa eneo hilo ni maalum kwa ajili ya michezo.

“Unajua siasa inafika mahali watu wanajisahau....maana jambo hilo tumejitahidi kulizungumza kupitia vikao hata kuibuka mizozo ndani ya hivyo vikao lakini tunaishia kuzomewa,” alieleza.

Alieleza kuwa mkataba huo ulipelekwa hadi katika semina ya madiwani iliyofanyika Januari 9 na 10 mwaka huu Landmark Hotel ili kupata baraka za madiwani, lakini baadhi waliupinga kwa kuwa haukufuata utaratibu.
“Kwa kuwa viongozi wa Ilala wanajua fika kuwa kuna madiwani ambao wana midomo...walichokifanya ni kuwaweka karibu na inaonekana fedha imetumika ili kuwanyamazisha midomo,” kilifafanua.

Aidha, chanzo hicho kilieleza kuwa mikataba isiyokuwa na manufaa ndiyo inayosababisha halmashauri hiyo kuporomoka licha ya kuwa na vyanzo vingi vya mapato tofauti na wilaya ya Temeke.

Baadhi ya madiwani wamekuwa wakipiga kelele za mara kwa mara kuhusu uwanja huo wa michezo wa Jangwani lakini hakuna hatua zilizochukuliwa hadi sasa licha ya Rais Kikwete kutoa agizo lake.

“Ni vigumu kwa watendaji wa halmashauri hiyo kuvunja uzio huo kwa sababu wao ndio walioshiriki kuingia mkataba huo mbovu.
“Haya ndiyo mambo tunayopigia kelele kila wakati lakini hatusikilizwi maana halmashauri ina wataalam wa ardhi wa kutosha iweje wanashindwa kujua umuhimu wa viwanja vile?” kilihoji.

Kilisisitiza kuwa kutokana na Rais Kikwete kuwa ndiye mhimili mkuu wa dola basi ana jukumu la kuhakikisha maagizo anayoyatoa yanatekelezwa ipasavyo.

Rais Kikwete ametakiwa kuingia na kusimamia agizo hilo binafsi kwa kwenda na kuvunja uzio huo mwenyewe kwani sio rahisi kwa walioingia mkataba kusimamia agizo hilo kutokana na kulinda maslahi yao.
Hadi habari hii inaandikwa uzio wa mabati bado upo ndani ya viwanja hivyo huku wizara ikiitaka halmashauri ya Ilala ibomoe lakini majibu yanayotolewa na halmashauri hiyo ni kwamba wamezuiwa kufanya utekelezaji huo.


Hii si mara ya kwanza kudanganywa kwa Rais kwani ameshadanganywa zaidi ya mara 12 miongoni mwa mambo aliyodanganywa ni pamoja na ile ya kuzindua mradi wa Bwawa la Manchira lililoko wilayani Serengeti wakati tayari wananchi wamekwishafungua kesi Mahakama Kuu ya Mwanza wakidai fidia.

Kesi hiyo iliyofunguliwa ni matokeo ya viongozi wa serikali wilayani humo kuhusika kuwalipa fidia watu wasiohusika na kuwaacha walengwa waliofanyiwa tathmini.

Pia aliwahi kudanganywa kwamba daraja la Mkenda lililoko Ruvuma ambalo ni njia muhimu kuelekea Msumbiji, lilikuwa limekamilika.
Katika tukio jingine, Rais aliwahi kupewa taarifa zisizo sahihi kuhusu tuhuma za rushwa zilizokuwa zikimkababili Anatory Choya kisha akamteua kuwa mkuu wa wilaya, lakini siku siku chache baadaye akafunguliwa mashtaka na TAKUKURU.

Mwaka juzi, akiwa ziarani Mbeya msafara wa Rais ulishambuliwa kwa mawe na watu, lakini wasaidizi wake wakaja kutoa taarifa kwamba watu hao walikuwa ni wahuni na walikuwa wakimsubiri Rais kwa muda mrefu bila mafinikio.
Hata hivyo, baadaye uchunguzi huru ulibainisha kwamba tukio hilo lilikuwa na mafungamano ya kisiasa na makovu ya mchakato wa uchaguzi ndani ya CCM kwa mwaka 2005.

Mlolongo huo mrefu wa upotoshaji taarifa kwa Rais uliibuka tena katika utoaji wa magari ya misaada ambapo badala ya kupewa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Longido alipewa wa Ngorongoro.
Tukio hilo lilimfanya mkuu huyo wa nchi kukasirika na kumzodoa mkurugenzi huyo, lakini baadaye ikabainika mkurugenzi huyo alikwenda kutokana na makosa ya maafisa wa Ikulu.

Katika mlolongo huo, tukio kubwa kabisa ni Rais kutia saini kwa mbwembwe Sheria ya Gharama za Fedha za Uchaguzi ambayo ilichomekwa vipengele nje ya Bunge kitu ambacho ni kinyume cha sheria.
Tukio hilo ambalo ni la uvunjifu wa Katiba, liliibuliwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, ambaye awali, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Fedrerick Werema, alikanusha.
Hata hivyo, baadaye sheria hiyo ilirudishwa bungeni na kukarabatiwa kwa mgongo wa mabadiliko ya sheria mbalimbali.

Mei mwaka jana, Rais alipewa taarifa za upotoshaji kuhusu mazungumzo ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) na serikali, kwa kuelezwa shirikisho hilo halikuhudhuria mkutano wa saa 4:00 asubuhi kama ilivyopangwa.

Hata hivyo, TUCTA wakatoa ushahidi wa barua za mwaliko wa mkutano huo wa Aprili 22 mwaka jana, ambazo zilikuwa mbili moja ikionyesha walitakiwa kufika katika mazungumzo Hazina saa 4:00 asubuhi na nyingine saa 8:00 mchana.

Katika kuonyesha upotoshaji kwa Rais, wasaidizi hao walimpa barua iliyokuwa ikionyesha walipaswa kukutana saa 4:00 asubuhi huku ile ya saa 8:00 wakawa wameificha. Rais akizungumza na wazee wa mkoa wa Dares Salaam aliwashambulia viongozi wa TUCTA hasa Naibu Katibu Mkuu, Nicolas Mgaya, akimwita mnafiki, mzandiki, na mchochezi

Haya mwana jamii fuatilia gazeti la Tanzania daima la tarehe 23/04/2011.
 
Nashangaa eti Rais anadanganywa tena na mawaziri wake. Ajabu eti??????
Ndo maana wanashindwa hata kutoa hoja za msingi kwenye hii mikataba feki. Kumbe wanazungukana wenyewe kwa wenyewe, yaani Rais na mawaziri wake.
 
huyo bwana ni msaliti wa kundi ka two brothers na sisi watanzania kwa ujumla, anafanya mambo kwa kujiosha baada ya kuchafua na kupata manufaha, kama kweli anataka libomolewe alishindwa nini kuwambia vijana wake wa baraza la mawaziri mmoja wao hakasimamie bomoa bomoa hiyo,
kwa nini maagizo yake ni kama ya diwani badala ya raisi yaani anaongea kama hana mamlaka, i
harafu anatoa maagizo hayana ufuatiliaji, kwa mfano aliposema nilisema hapo jangwani pabomolewe lakini mpaka sasa hakuna kilichofanyika, ina maana yeye alisema tu na kwenda zake bila yeye mwenye kuomba taarifa ya utekerezaji, ndio maana watu wanachota tu pesa yetu kwa mikataba feki
Hata mimi naanza kuona huu ni usanii tunaochezewa na JK kwa kujifanya hajui kitu, inawezekana hata hii issue alijua nini kinaendelea leo ndio anajidai kutoa amri ubomolewe na kuwageuka kama alivyowageuka kina RACHEL.
 
Mmmhhh huyu raisi kiboko, kama anadanganywa katika haya yaliyo wazi tunayoweza kuyaona... vipi yale ya ndani... 2015 mbali sana!!
 
Mmmhhh huyu raisi kiboko, kama anadanganywa katika haya yaliyo wazi tunayoweza kuyaona... vipi yale ya ndani... 2015 mbali sana!!

Asante kwa kulitambua hilo. Kweli 2015 kwa staili hii ni mbali tena mno.
Hii ndo ARI MPYA, NGUVU MPYA NA KASI MPYA. hahahaha.
 
nchi ilishamshinda hii tangu awamu yake ya kwanza...
Sasa hayo ni ya hapa Dar.
Tukienda mikoani huko kwenye mikataba mibovu ya wawekezaji wa Madini si ndio unaweza kula nyama ile hali ni ijumaa kuu?
 
Kwanza watanzania lazima tumjue huyu anayeitwa rais ana tabia gani specific. Ninachojua mimi ni kwamba kikwete ni msahaulifu na wasaidizi wake wanamjua hivyo. Ndiyo maana anapotoa maagizo hawatishiki sana kwani wanajua maagizo hayo yataishia majukwaani tu. Leo hii ukimkumbusha kuhusu uzio wa Jangwani usije ukashangaa kuwa amesahau.
 
Kwanza watanzania lazima tumjue huyu anayeitwa rais ana tabia gani specific. Ninachojua mimi ni kwamba kikwete ni msahaulifu na wasaidizi wake wanamjua hivyo. Ndiyo maana anapotoa maagizo hawatishiki sana kwani wanajua maagizo hayo yataishia majukwaani tu. Leo hii ukimkumbusha kuhusu uzio wa Jangwani usije ukashangaa kuwa amesahau.
Labda kale ka-ugonjwa ka kuanguka anguka ndiko kana affect uwezo wake wa kukumbuka mambo.
 
WIKI chache baada ya Rais Jakaya Kikwete kutoa agizo akitaka uzio wa viwanja vya michezo Jangwani ubomolewe, imebainika kuwa agizo hilo limeshindwa kutekelezeka kwa sababu eneo hilo limeuzwa kwa mwekezaji ambaye ni raia wa China.

Hivyo watendaji wa Halmashauri ya Ilala na Wizara ya Ardhi wanabanwa na masharti ya mkataba unaodaiwa kuingiwa baina yao na mwekezaji huyo.

Imebainika kuwa Rais Kikwete alitoa agizo hilo Aprili 3 mwaka huu baada ya kupewa taarifa potofu na hivyo kutoa amri ambayo haitekelezeki kisheria.

Akiweka jiwe la msingi la upanuzi wa barabara ya New Bagamoyo, eneo la Mwenge-Tegeta, Rais Kikwete aliagiza uzio huo ubomolewe lakini hadi jana hakuna bomoabomoa yoyote iliyokuwa imefanywa katika eneo hilo.

Chanzo chetu kutoka ndani ya halmashauri ya Ilala kilisema mkataba huo umempa mwekezaji huyo haki ya kujenga maghala mbalimbali ‘magodauni’, kwa makubaliano kwamba yangeinufaisha pia halmashauri hiyo.

Ilibainishwa zaidi kuwa mkataba huo uliingiwa kibinafsi na baadhi ya viongozi wa Ilala kutokana na tamaa ya fedha huku wakishindwa kuzingatia kuwa eneo hilo ni maalum kwa ajili ya michezo.

Baadhi ya madiwani wamekuwa wakipiga kelele za mara kwa mara kuhusu uwanja huo wa michezo wa Jangwani lakini hakuna hatua zilizochukuliwa hadi sasa licha ya Rais Kikwete kutoa agizo lake.

“Ni vigumu kwa watendaji wa halmashauri hiyo kuvunja uzio huo kwa sababu wao ndio walioshiriki kuingia mkataba huo mbovu.

“Haya ndiyo mambo tunayopigia kelele kila wakati lakini hatusikilizwi maana halmashauri ina wataalam wa ardhi wa kutosha iweje wanashindwa kujua umuhimu wa viwanja vile?” kilihoji.

Kilisisitiza kuwa kutokana na Rais Kikwete kuwa ndiye mhimili mkuu wa dola basi ana jukumu la kuhakikisha maagizo anayoyatoa yanatekelezwa ipasavyo.

Rais Kikwete ametakiwa kuingia na kusimamia agizo hilo binafsi kwa kwenda na kuvunja uzio huo mwenyewe kwani sio rahisi kwa walioingia mkataba kusimamia agizo hilo kutokana na kulinda maslahi yao.

Hadi habari hii inaandikwa uzio wa mabati bado upo ndani ya viwanja hivyo huku wizara ikiitaka halmashauri ya Ilala ibomoe lakini majibu yanayotolewa na halmashauri hiyo ni kwamba wamezuiwa kufanya utekelezaji huo.

Ni kweli kwamba rais hakupewa taarifa sahihi juu ya matumizi ya eneo la Jangwani kuliko na ukuta wa mabati.Si kweli kwamba eneo lile limeuzwa kwa mwekezaji wa Kichina!Usahihi ni kwamba kinachofanyika pale ni ujenzi wa Depot ya mabasi yaendayo haraka ya DAR RAPID TRANSIT AGENCY.Huu ni mradi wa serikali uko chini ya Jiji na Wizara ya Tawala za Mikoa(TAMISEMI).Kilichotokea ni kwamba Mkandarasi BEIJING CONTRUCTION AND ENGINEERING CO.LTD alipewa kazi na akaanza kuzungushia ukuta wa mabati ili kuanza kazi ya Ujenzi.MAMLAKA ZINAZOHUSIKA wote wakiwa na habari na hata yeye Mh.Rais akiwa na habari kupitia kwa watendaji wake aliridhia eneo hilo limegwe kwa ajili ya kazi hiyo akisema, Namnukuu,"The area is for public usage hata na huu MRADI ni wa public" Sasa kudanganywa kuko wapi zaidi ya kukurupuka tuu.Na kwa mantiki hiyo kuna baraka za ngazi zote ndo maana hapabomolewi hadi Mh.Rais asimame tena jukwaani na kuwataka radhi wananchi kwamba naye amekurupuka kusema.
 
Raisi hajadanganywa katika hili. Alipotembelea Wizara ya Ujenzi; kabla ya huo uzio kuwekwa, walimpa taarifa juu ya mpango huo na akawauliza iwapo wamezingatia kuwa hilo ni eneo la viwanja vya michezo. Inaelekea jamaa wizara na Manispaa hawakuchukulia kwa uzito maagizo yake hadi alipoona uzio wa mabati.
Swali hapa ni kama uzio haujabomolewa je, ujenzi unaendelea?
 
Ni kweli kwamba rais hakupewa taarifa sahihi juu ya matumizi ya eneo la Jangwani kuliko na ukuta wa mabati.Si kweli kwamba eneo lile limeuzwa kwa mwekezaji wa Kichina!Usahihi ni kwamba kinachofanyika pale ni ujenzi wa Depot ya mabasi yaendayo haraka ya DAR RAPID TRANSIT AGENCY.Huu ni mradi wa serikali uko chini ya Jiji na Wizara ya Tawala za Mikoa(TAMISEMI).Kilichotokea ni kwamba Mkandarasi BEIJING CONTRUCTION AND ENGINEERING CO.LTD alipewa kazi na akaanza kuzungushia ukuta wa mabati ili kuanza kazi ya Ujenzi.MAMLAKA ZINAZOHUSIKA wote wakiwa na habari na hata yeye Mh.Rais akiwa na habari kupitia kwa watendaji wake aliridhia eneo hilo limegwe kwa ajili ya kazi hiyo akisema, Namnukuu,"The area is for public usage hata na huu MRADI ni wa public" Sasa kudanganywa kuko wapi zaidi ya kukurupuka tuu.Na kwa mantiki hiyo kuna baraka za ngazi zote ndo maana hapabomolewi hadi Mh.Rais asimame tena jukwaani na kuwataka radhi wananchi kwamba naye amekurupuka kusema.
Hata mimi nilisikia ni kwa ajili ya mabasi yaendayo kasi, kama alikuwa anajua hili basi alikurupuka!
 
Kuna ile ya cheki ya mfano iliokuwa na ikionyesha tarakimu tofauti na kilichoandikwa.
 
Rais wetu anadanganyika kirahisi. Huyu ni Mangungo wa Msovero mpya.
 
Rais wetu anadanganyika kirahisi. Huyu ni Mangungo wa Msovero mpya.

Duh! Umenikumbusha mbali sana. Mangungo alisaini mikataba ya ulaghai. Basi ndivyo anavyofanya this jamaa.
Lakini yeye anafanya kwa kujua kabisa.
 
Mithali 29:12-Mwenye kutawala akisikiliza uongo,Basi watumishi wake wote watakuwa waovu"!
Hili ni hatari sana katika ulimwengu wa kiroho na matokeo yake yako dhahiri kila mahali! Eeh Mungu uiherehemu nchi yetu!!!
 
Back
Top Bottom