JK aalika warembo wa Miss East Africa Ikulu

Sep 15, 2008
54
0
3.JPG


Raisi wetu amealika Ikulu warembo wa Miss EA usiku wa kuamkia leo.
Hii sio mara ya kwanza, huwa siku zote anaalika ma-celeb wa kibongo wamtembelee Ikulu, haina ubaya wowote, ila nnachoshangaa mbona huwa haaliki watu wanaochangia kwenye maendeleo ya taifa letu, kwa mfano watoto waliofaulu, kitaifa au hata kimataifa (kama yule aliyeshinda SADC essay competition) kuonyesha kuwa hao ndio role models wanaotakiwa kufuatwa, yeye ni vitu vya starehe starehe tu.
 
3.JPG


Raisi wetu amealika Ikulu warembo wa Miss EA usiku wa kuamkia leo.
Hii sio mara ya kwanza, huwa siku zote anaalika ma-celeb wa kibongo wamtembelee Ikulu, haina ubaya wowote, ila nnachoshangaa mbona huwa haaliki watu wanaochangia kwenye maendeleo ya taifa letu, kwa mfano watoto waliofaulu, kitaifa au hata kimataifa (kama yule aliyeshinda SADC essay competition) kuonyesha kuwa hao ndio role models wanaotakiwa kufuatwa, yeye ni vitu vya starehe starehe tu.

Jamani tukosoe penye uzito wa mustakabli wa nchi yetu hao Mamiss na celebrities kwenda Ikulu ina ubaya gani? Si ndo ku-enhance intergration jamani? au mi nathani hapa swala liwe wale wanaotafuta agenda na maslahi yao binafsi (Wafanyabiashara)! Kwa mfano hawa wanaoenda kutoa zawadi ndani ya Ikulu! Ikulu ikitoa zawadi ni sawa! isitoshe JK amekuwa akialika hata wanafunzi bora unaosema fuatilia utajua hukusema kweli!
 
3.JPG


Raisi wetu amealika Ikulu warembo wa Miss EA usiku wa kuamkia leo.
Hii sio mara ya kwanza, huwa siku zote anaalika ma-celeb wa kibongo wamtembelee Ikulu, haina ubaya wowote, ila nnachoshangaa mbona huwa haaliki watu wanaochangia kwenye maendeleo ya taifa letu, kwa mfano watoto waliofaulu, kitaifa au hata kimataifa (kama yule aliyeshinda SADC essay competition) kuonyesha kuwa hao ndio role models wanaotakiwa kufuatwa, yeye ni vitu vya starehe starehe tu.


JK anatisha wewe...usifanye mchezo na kile kidume! After all decion amwalike nani asimwalike nani liko kwa anayealika so hili swali hapa sio mahala pake. Mfuate ikuluuuuuuuuuuuu atakujibu au subiri ile forum ya kisanii ya Tido Mhando na Rais umuulize kwa sms au email
 
mmm, hata mi nimeshangaa, hajawahi kufanya nao hafla timu ya taifa ya football, walemavu japo wakati wa sikukuu. huyu kaona warembo tu ale nao vitamu tamu.
 
He know what he wants from those girls! kidume cha pwani kile!!!!!!!!!!!
 
mmm, hata mi nimeshangaa, hajawahi kufanya nao hafla timu ya taifa ya football, walemavu japo wakati wa sikukuu. huyu kaona warembo tu ale nao vitamu tamu.

Hapo juu in red alishawahi kufanya au kumbukumbu zangu haziko right any one correct me.
 
Ni lini ataongea na wasomi wetu wa vyuoni ili kujua matatizo yao na kutafuta jinsi ya kukuza elimu Tanzania?

This guy has his priorities backwards!
 
Ni lini ataongea na wasomi wetu wa vyuoni ili kujua matatizo yao na kutafuta jinsi ya kukuza elimu Tanzania?

This guy has his priorities backwards!

Tangu lini wasomi waka-entertain? No delicious food for the eyes there!:rolleyes:

Kukutana na watu amboa watakuboa na kukuharibia mood inataka moyo kama vile unakunywa quinine. Nani anaweza kuinywa bila kuumwa?
 
Amewaalika watu tofauti tofauti nadhani hata wakati wa mwezi mtukufu wa ramadhani ameshaandaa futari ikulu na baadhi ya watu walihudhuria, nadhani tujitahidi kuangalia mazuri yake mengi na siyo mabaya yake machache.
 
Jamani tukosoe penye uzito wa mustakabli wa nchi yetu hao Mamiss na celebrities kwenda Ikulu ina ubaya gani? Si ndo ku-enhance intergration jamani? au mi nathani hapa swala liwe wale wanaotafuta agenda na maslahi yao binafsi (Wafanyabiashara)! Kwa mfano hawa wanaoenda kutoa zawadi ndani ya Ikulu! Ikulu ikitoa zawadi ni sawa! isitoshe JK amekuwa akialika hata wanafunzi bora unaosema fuatilia utajua hukusema kweli!

kama umesoma thread yangu vizuri, nimesema kabisa kuwa hamna ubaya.
ila kama mchangiaji mmoja alivyosema, this guy has his priorities backwards, as mimi, nadhani pamoja na wengi wetu tunaamini kuwa raisi wa nchi kuwaalika hao washiriki wa urembo hakuliletei tija taifa, na mimi, pia hapa naamini naongea kwa niaba ya wengi, hatuoni umuhimu wa hao warembo kualikwa ikulu, ukizingatia kuwa hilo ni shindano la urembo ambalo haliendi sehemu yeyete zaidi ya hapo mlimani city.

Pia naomba kujua kama keshawatembelea waathirika wa maporomoko Same, nilisikia ametangaza mpango wa kwenda, a month after, sijui keshaenda, au anaentertain mamiss ikulu tu.

afu keshaambiwa awe anapumzika, sasa si afadhali hizo nguvu angekuwa anazisave kutumika kwenye mambo muhimu kitaifa ambayo tumemwajiri na tunamlipa kuyafanya badala ya kufanya haya, afu yakifika mambo ya msingi anaishiwa nguvu.
 
hamna kumbukumbu au ndio wengine mna chuki binafsi,amealika wengi tu hata timu ya taifa stars alishaialika na mabo mengine mengi ameyafanya huko ikulu ya kuwaalika wanamichezo,hata hasheem thabit alimualika,au hamridhiki mpaka awaalike na nyie na awaalike kwa jambo lipi hasa mlilolifanya labda awaalike na aseme leo nawaalika wale wote wenye chuki binafsi na roho za kwanini pengine mnaweza kwenda kwa njia hiyo.
 
JK anatisha wewe...usifanye mchezo na kile kidume! After all decion amwalike nani asimwalike nani liko kwa anayealika so hili swali hapa sio mahala pake. Mfuate ikuluuuuuuuuuuuu atakujibu au subiri ile forum ya kisanii ya Tido Mhando na Rais umuulize kwa sms au email

huyu ni raisi, so suala ya yeye anamuona nani katika cheo chake cha uraisi na anatumiaje ikulu, ambayo ni ofisi ya serikali linanihusu kwa asilimia mia moja na moja (101%) na wala siwezi kunyamaza.

pia hapa ni mahali pake kujadiliwa as fedha zinazotumika kuwaalika hao warembo, chakula wanachokula, hata kama wanakula kidogo kwa ajili ya dayati, ni kodi yangu nnayokatwa kila mwezi kwenye mshahara wangu, na kila siku kwenye mambo mengine ya maisha yangu!

wewe ndio hapa sio mahali pako, maana hata hujui masuala yanayokuhusu kama mtanzania na yasiyokuhusu, unadhani Ikulu mali ya raisi? ikulu mali yako wewe na watanzania wote, na kujua inatumikaje ni muhimu kwako, unaweza kunyamaza kwa kutojali au kutojua, lakini usitake kuwafumba mdomo wanaojali kama mimi!
 
kama umesoma thread yangu vizuri, nimesema kabisa kuwa hamna ubaya.
ila kama mchangiaji mmoja alivyosema, this guy has his priorities backwards, as mimi, nadhani pamoja na wengi wetu tunaamini kuwa raisi wa nchi kuwaalika hao washiriki wa urembo hakuliletei tija taifa, na mimi, pia hapa naamini naongea kwa niaba ya wengi, hatuoni umuhimu wa hao warembo kualikwa ikulu, ukizingatia kuwa hilo ni shindano la urembo ambalo haliendi sehemu yeyete zaidi ya hapo mlimani city.

Pia naomba kujua kama keshawatembelea waathirika wa maporomoko Same, nilisikia ametangaza mpango wa kwenda, a month after, sijui keshaenda, au anaentertain mamiss ikulu tu.

afu keshaambiwa awe anapumzika, sasa si afadhali hizo nguvu angekuwa anazisave kutumika kwenye mambo muhimu kitaifa ambayo tumemwajiri na tunamlipa kuyafanya badala ya kufanya haya, afu yakifika mambo ya msingi anaishiwa nguvu.

inabidi kuvumilia tu, vinginevyo thread nyingine humu mmmh!!! JK is our Diplomat NO. 1, hivyo alikuwa anafanya kazi ya watanzania kwa wepesi kabisa na kirahisi. amefanya kile ambacho marais wengine wowote wa mataifa mengine wanafanya. kumbuka mamiss wale wanawakilisha nchi zao. Juzi juzi rais Jacob Zuma ameplay host kwa mamiss wa miss world ikulu, mwaka jana Rais mlokole wa Burundi, Nkuruzinza aliwaalika warembo wa East Africa Ikulu na kula nao chakula cha mchana. Hata mzee Mandela alipokuwa rais aliwaalika.
 
hamna kumbukumbu au ndio wengine mna chuki binafsi,amealika wengi tu hata timu ya taifa stars alishaialika na mabo mengine mengi ameyafanya huko ikulu ya kuwaalika wanamichezo,hata hasheem thabit alimualika,au hamridhiki mpaka awaalike na nyie na awaalike kwa jambo lipi hasa mlilolifanya labda awaalike na aseme leo nawaalika wale wote wenye chuki binafsi na roho za kwanini pengine mnaweza kwenda kwa njia hiyo.

hapo hupingani na sisi, maana uliowataja wengi ndio maselebriti!
ingawa wengine, wanafaa kuigwa na kualikwa, ila washiriki wa miss east afrika, LOH! hii sikubaliani nayo!
 
hamna kumbukumbu au ndio wengine mna chuki binafsi,amealika wengi tu hata timu ya taifa stars alishaialika na mabo mengine mengi ameyafanya huko ikulu ya kuwaalika wanamichezo,hata hasheem thabit alimualika,au hamridhiki mpaka awaalike na nyie na awaalike kwa jambo lipi hasa mlilolifanya labda awaalike na aseme leo nawaalika wale wote wenye chuki binafsi na roho za kwanini pengine mnaweza kwenda kwa njia hiyo.


Kama hicho ndicho kigezo, warembo wamefanya nini? Kwani kati ya kazi zake muhimu kwa Taifa na hii ya kualika wasanii maarufu imo? Na kama imo ni namba ngapi kwenye top priorities zake au list (shajara) ya vitu vyake alivyopanga kufanya kwa siku, week, mwezi na mwaka?
 
sijui lini atawaalika wasiojiweza wale viwete wa kule posta na ombaomba wote.kweli mambo ya urembo yameiteka TANZANIA kila kona miss kata ,miss tarafa sijui hadi kwa watoto sijui umiss
 
Jamani kwa nchi ku host mashindano kama hayo ina manufaa kweli though hamuwezi kuyaona lakini kwa walio kwenye sector ya utalii ni rahisi saana kuona, kwakupitia hayo mashindano nchi inajulikana, ili kufanikisha hayo lazima kuwe na political support, alichokifanya JK sio kibaya hata kidogo la wala hakuwa na nia mbaya alifayanya kwa niaba ya watz wote

kwakutokwenda same mpaka leo kwahapo,,, binafsi naona sio vizuri kama kumbukumbu zangu ziko sahihi baada ya maafa ya same kuna kijiji kimoja Bagamoyo yalitokea mafuriko lakini hakuna mtu aliyekufa nadhani kesho yake JK aliwatembelea,,, kinachonishangaza ni kwanini hakwenda SAME pia??atakuwa na sababu lakini naamini alikuwa na uwezo wa kuwatembelea na kuwapa pole kama rais wao bila kuonyesha upendeleo wa wazi wazi
 
Back
Top Bottom