JK aainisha nguzo kuu sita za kuleta maendeleo Afrika

Kidudu Mtu

Member
Nov 7, 2009
64
0
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ametaja nguzo kuu sita ambazo amesema kuwa zikitekelezwa ipasavyo zitaharakisha kasi ya maendeleo ya Bara la Afrika.

Miongoni mwa nguzo hizo ni Bara la Afrika kuhakikisha kuwa linabuni njia bora zaidi, endelevu zaidi na za uerevu zaidi wa jinsi ya kutumia raslimali zake muhimu kama vile madini na mafuta kwa ajili ya maendeleo ya watu wa Bara hilo.

Rais Kikwete ametaja nguzo hizo sita wakati aliposhiriki katika mdahalo kuhusu Fikra Mpya za Mkakati wa Maendeleo ya Afrika – Rethinking Africa’s Development Strategy - kwenye siku ya kwanza ya Mkutano wa 40 wa Taasisi ya Uchumi Duniani ya World Ecocomic Forum unaofanyika mjini Davos, Uswisi.

Mkutano huo unaoshiriki viongozi kutoka zaidi ya nchi 30 duniani na baadhi ya viongozi maarufu na mashuhuri wa nyanja ya uwekezaji, biashara, uchumi na maendeleo duniani, umeanza leo, Jumatano, Januari 28, 2010, kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Congress Centre.

Miongoni mwa washiriki wenzake katika mdahalo huo wa kwanza wa Mkutano huo wa WEF alikuwa ni Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Donald Kaberuka, Mwenyekiti na Rais wa Benki ya Exim ya China Li Ruogu na Maria Ramos, Mtendaji Mkuu wa Kundi la Benki ya Absa ya Afrika Kusini ambaye aliendesha mdahalo huo.

Akifafanua kuhusu nguzo hiyo ya kwanza ya Bara la Afrika kutumia vizuri, kwa njia endelevu na erevu raslimali zake, Rais Kikwete amesema kuwa uchimbaji wa madini na mafuta katika Afrika lazima uwasaidie Waafrika.

“Ni jambo lisilokubalika kuwa madini ama mafuta yanachimbwa katika Bara la Afrika, lakini jamii zinazozunguka machimbo hayo havinufaiki na uchimbaji huo. Baadhi ya makampuni ya uwekezaji katika machimbo yanathubutu hata kuagiza maji ya kunywa, ama kuagiza chakula, ama hata kukodisha malori ya kusomba mchanga kutoka nje ya Bara hili,” amesema Rais Kikwete.

Nguzo ya pili muhimu kwa maendeleo ya Afrika, kwa mujibu wa Rais Kikwete, ni umuhimu wa Bara la Afrika kuendeleza na kudumisha mageuzi ya kiuchumi ambayo yameuwezesha uchumi wa Bara hilo kukua kwa namna ya uendelevu kwa zaidi ya miaka 10 mfululizo kabla ya misukosuko ya karibuni ya uchumi duniani.

Rais Kikwete ameitaja misukosuko hiyo kuwa ni pamoja na kupanda ghafla na kwa kiwango kikubwa kwa bei za mafuta duniani, kupanda sana na ghafla kwa bei ya chakula duniani kabla ya kuanza kunyumba kwa kiasi kikubwa mno kwa uchumi wa jumla wa dunia.

Rais Kikwete ameitaja nguzo kuu ya tatu kuwa ni umuhimu wa Bara la Afrika kuendeleza uwekezaji wake katika sekta ya miundombinu, ili kuboresha kiwango cha uzalishaji wa wakulima na kuwawezesha kufikisha mazao yao haraka sokoni.

Rais Kikwete amesema kuwa nguzo kuu ya nne kwa uchumi wa Afrika kuweza kukua kwa haraka zaidi ni Bara la Afrika kuwekeza katika kilimo ambacho ni muhimili wa kati ya asilimia 70 na 80 ya Waafrika wote wanaoishi kwa kutegemea kilimo.

“Kilimo kitatuwezesha kuwa na usalama na uhakika wa chakula. Tunaweza kuuza akiba nchi za nje ili kujipatia fedha zaidi za kilimo,” amesema Rais Kikwete katika mdahalo huo.

Rais ameongeza kuwa nguzo kuu ya tano ya uchumi wa Bara la Afrika ni ulazima wa Bara hilo kuwekeza katika mtaji wa maendeleo ya binadamu yaani kuwekeza katika elimu na afya.

“Tumewekeza sana katika elimu ya msingi. Tumefanya vizuri katika elimu hiyo, lakini elimu ya msingi ni elimu ya kufuta ujinga. Lazima sasa tuelekeze nguvu zetu katika elimu ya sekondari na elimu ya chuo kikuu. Na hasa katika elimu ya sayansi. Ni elimu ya namna hiyo itakayokabdilisha Bara letu,” Rais Kikwete amewaambia watazamaji na wasikilizaji katika mdahalo huo.

Nguzo ya sita na ya mwisho, kwa mujibu wa Rais Kikwete, ni kukuza haraka ushirikiano wa kikanda (regional integration) kama kukusanya nguvu za pamoja za nchi mbali mbali kukabiliana na changamoto za maendeleo.

Akijibu swali kuhusu rushwa kama kikwazo cha maendeleo katika Afrika, Rais Kikwete amesema kuwa ni jambo la kusikitisha kuona baadhi ya watu nje ya Afrika wakiamini kuwa kila mtu katika Afrika, kila mtumishi wa umma katika Afrika, anakula rushwa.

“Lazima tukumbe kuwa Bara la Afrika linalo mataifa 53 na mataifa haya yanatofautiana kwa namna nyingi. Ni kweli ipo rushwa katika Afrika, kama ilivyokuwapo rushwa katika sehemu nyingine duniani.

Lakini siyo kwamba kila Mwafrika ama mtumishi wa umma katika Afrika anakula rushwa. Ni vizuri tunachukua muda kujifunza mema yanayotoka katika Bara hili,” amefafanua Rais Kikwete.​

 
I am simply embarrassed by this despicable mockery of our collective intelligence.
 
huyu naye ni mbabaishaji, ana kawaida ya kuimba asicho kijua, hatujasahau hapa kwetu mambo ya maisha bora kwa kila mtanzania, bila ya ufafanuzi wa namna gani yatakuja, au kwa njia gani katuacha kwenye mataa labda ndiyo yale kusikia tu trip zake za majuu
 
HUYU jamaa hajui wakati wa kunyamaza?with what is going on in TZ he should never open his mouth to express ANY opinion for like 30 years.
 
Anasema vitu ambavyo yeye mwenyewe hajui jinsi ya kuvifanya, ananikumbusha watoto wa chekechea wanavyokaririshwa nyimbo bila ata kujua zinamaanisha nini, mambo ya madesa kaaazi kwelikweli...
 
Vichekesho kweli vya JK. Kwenye majukwaa anajua jinsi ya kujipalisha chati huku hana lolote analofanya hata kwenye hayo anayoongea.
  1. Maliasili - Sijui kama kuna mtanzania anayefaidika zaidi ya Balozi Ammy Mpungwe. Wengine wote tunazisikia tu Tanzanite na Gold kwenye news.
  2. Mageuzi ya kiuchumi - Sijui ni investor gani atakayekuja kwenye nchi isiyo na umeme.
  3. Miundo Mbinu - TRC imeshindikana, Bandari usiseme, ATC ndio kabisaa
  4. Kilimo - Tumesikia pakinadiwa sera, je kuna mabadiliko yoyote? nope!
  5. Elimu - Angalau Lowassa alifanya vituko vya shule za kata, since then kimyaa. Wanaongeza wabunge badala ya kusomesha waalimu.
  6. Regional Intergration - Zadi ya viongozi, wananchi walio wengi wote wanaona kuwa nchi yao haijajiandaa vema kushindana na wengine.
Sasa huyu JK anachoongea na anayofanya ni wapi kwa wapi? Atayafanya lini maana tayari huu ni mwaka wake wa 5?
 
Na kitabu kimeshaandikwa juu ya makubwa aliyoyafanikisha katika miaka 4 ya uongozi wake.
 
2.jpg
 
Kabla hujarukia Afrika, nakuomba umalize kwanza matatizo ya nyumbani kwako.

Asante Mr. President. Home First.
 

Akifafanua kuhusu nguzo hiyo ya kwanza ya Bara la Afrika kutumia vizuri, kwa njia endelevu na erevu raslimali zake, Rais Kikwete amesema kuwa uchimbaji wa madini na mafuta katika Afrika lazima uwasaidie Waafrika.


Nguzo ya pili muhimu kwa maendeleo ya Afrika, kwa mujibu wa Rais Kikwete, ni umuhimu wa Bara la Afrika kuendeleza na kudumisha mageuzi ya kiuchumi ambayo yameuwezesha uchumi wa Bara hilo kukua kwa namna ya uendelevu kwa zaidi ya miaka 10 mfululizo kabla ya misukosuko ya karibuni ya uchumi duniani.


Rais Kikwete ameitaja nguzo kuu ya tatu kuwa ni umuhimu wa Bara la Afrika kuendeleza uwekezaji wake katika sekta ya miundombinu, ili kuboresha kiwango cha uzalishaji wa wakulima na kuwawezesha kufikisha mazao yao haraka sokoni.

Rais Kikwete amesema kuwa nguzo kuu ya nne kwa uchumi wa Afrika kuweza kukua kwa haraka zaidi ni Bara la Afrika kuwekeza katika kilimo ambacho ni muhimili wa kati ya asilimia 70 na 80 ya Waafrika wote wanaoishi kwa kutegemea kilimo.

Rais ameongeza kuwa nguzo kuu ya tano ya uchumi wa Bara la Afrika ni ulazima wa Bara hilo kuwekeza katika mtaji wa maendeleo ya binadamu yaani kuwekeza katika elimu na afya.

Nguzo ya sita na ya mwisho, kwa mujibu wa Rais Kikwete, ni kukuza haraka ushirikiano wa kikanda (regional integration) kama kukusanya nguvu za pamoja za nchi mbali mbali kukabiliana na changamoto za maendeleo.

Huyu nae anaongea nini?..kwani hizo nguzo amezijua leo?.,si anazifahamu, yeye mwenyewe amezitumiaje kuleta maendeleo kwa watanzania..,unafiki tu hakuna lolote hapa.
 
Na kitabu kimeshaandikwa juu ya makubwa aliyoyafanikisha katika miaka 4 ya uongozi wake.


Jasusi, umesoma kitabu hicho?

Mie hata nikipewa kitabu hicho bure kabisa pamoja na bakshisi ya fedha za motisha bado sitakipokea. Huyo Prosper Ngowi ni mmoja wa waalimu wa Mzumbe walionunua digrii huko COU au PWE baada ya kushindwa kuipata kihalali huko Norway. Kama alishindwa kuchambua mambo huko nyuma akakosa digrii basi sidhani kama kweli anaweza kuchambua mambo complex yanayohusu serikali na jamii kwa jumla katika mazingira ya leo. Niliwahi kukumbana na mwalimu mmoja aliyekuwa akisisitiza kuwa NYANI HAGEUKI KUWA BINADAMU HATA SIKU MOJA.
 
Hapa ni vichekesho. Afrika haitakuja kuendelea. Hifadhini maneno yangu na myarejee miaka 100 toka leo. Kama ikitokea nilikuwa wrong basi mwageni kinyesi kwenye kaburi langu.
 
lakini tusimlaumu saana yeye anaandaliwa kila kitu kazi ni rahisi tu NI KUSOMA, uraisi raha kweli
 
Back
Top Bottom