jitahidi ujiamini mwenyewe

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,148
Nini maana ya kujiamini au staha?
Kujiamini au Staha (self esteem) ni jinsi unavyojiona mwenyewe, ni image yako mwenyewe, kama una staha ya juu (high self esteem) maana yake unajiona mzuri kila eneo na kama una staha ya chini maana yake unajiona mbaya katika maeneo yote ya maisha yako.
Kuwa na staha ya chini (low self esteem, low self image) ni ugonjwa unaowasumbua wanawake wengi sana katika jamii yetu ya sasa kuliko wakati wowote katika historia ya dunia.

Tunaposema mwanamke fulani ana low self esteem au low self image tuna maana gani?
Hii ina maana kwamba mwanamke anakaa mwenyewe na kuanza kujishangaa kwa nini hana marafiki wa kweli.
Anakuwa na hamu ya kuongea na mtu ana kwa ana na anajua huyo mtu hayupo.
Ni mwanamke anayejisikia kwamba wengine hawawezi kumpenda wakigundua kwamba ni yeye halisi so anajitahidi kujifanya fulani ili watu wampende.
Ni mwanamke anayeogopa kuongeea na wanawake wenzake wa rika moja kwa maana kwamba yeye hayupo smart kama wao.
Ni mwanamke anayeamini wafanyakazi wa kike wa ofisini kwa mume wake ni wazuri zaidi kuliko yeye hivyo kila siku mume akirudi anaonywa na kwamba ajihadhari na hao wanawake.


Ni mwanamke anayejisikia mjinga fulani au maskini fulani au failure fulani hasa akiwa nyumbani kwake peke yake akifikiria maisha.
Ni kujishangaa kwa nini watu wengine wana uwezo na talents nyingi kuliko yeye.
Ni mwanamke anayejisikia hapendezi na havutii tena kimapenzi (sexually unattractive).
Ni mwanamke kujisikia ameshindwa kuwa mke na mama.
Ni mwanamke ambaye hapendi kitu chochote kuhusu yeye na kutamani ingekuwa vile na vile kama wengine.
Ni mwanamke kutamani muda wote angekuwa Fulani au angekuwa mtu mwingine.
Ni mwanamke anayejisikia hapendwi na hapendi mtu na matokeo yake anafunikwa na huzuni na upweke.

Ni mwanamke anayejisikia moyoni yupo empty hasa kwa kukosa upendo wa kweli.
Ni mwanamke ambaye anahisi wanawake ambao mume wake anaongea nao ni wazuri kuliko yeye hivyo wanaweza kumchukua au kutembea naye.
Ni mwanamke anayesubiri kuwe kweusi aanze kutoa machozi mazito kwa kujihurumia kwa hali aliyonayo na amefunikwa na msongo wa mawazo.
Ni mwanamke anayejiangalia kwenye kioo na kujiona hafai na kutamani sura yake ingekuwa kama ya fulani au angekuwa kijana zaidi.
Ni mwanamke anayejiangalia mwili wake na kujiona amenenepa na kwamba hakuna mtu atampenda tena na kwamba maisha yake ya kimapenzi na mumewe mwisho kwa kuwa amenenepa mno.
Na mengine mengi yanayofanana na hayo!

Je, low self esteem huwapata wanawake tu?
Kuwa na staha ya chini au ndogo si kwa wanawake tu bali huwapata zaidi wanawake.
Low self esteem ni tishio la dunia nzima hakuna cha motto, kijana mzee, rangi, tamaduni au jamii au kabila wote hukumbana na kuwa na staha ya chini.
Hili dubwana huweza kummeza mtu yeyote pale tu akianza kujisikia hayupo respected na mwingine.

Asilimia 90 ya wazo la low self esteem au low self image hyujengwa kwa kuwaza kuhusu wengine wanavyowaza kuhusu wewe.
Kawaida huwa inakuwa ngumu sana kujiamini mwenyewe kama the rest of the world wanaamini wewe ni dumb, ugly, mvivu, boring, uncreative, undesirable nk.

“No one can stand the awful knowledge that he/she is not needed”
 
Back
Top Bottom