Ndugu zangu wote waliopata mkopo na wale waliokosa kwanza kabisa nipende kwa pamoja sote tumshukuru Mwenyezi Mungu kwani ana mipango na sisi wanadamu aijalishi umepata mkopo au la. Basi ndugu zangu bila kuwachosha nilete yangu yalo moyoni na atakayeweza kunipa mawazo, maoni na msaada mwingine naomba atupie hapa. Mimi ni kijana niliyezaliwa katika kijiji kidogo nikiwa mtoto wa 17 kati ya watoto 30 wa baba yangu nikimaanisha kuwa kuna wakubwa zangu wasio na uwezo mzuri kiuchumi 16 na wadogo zangu ambao pengine wananitegemea 12. Kutokana na hali hiyo ya familia niliamua kukimbilia kutafuta elimu ambayo itakuwa ni mkombozi kwangu na hata familia na jamii kwa ujumla. Basi kwa neema ya Mungu nilifanikiwa kufaulu kidato cha nne kwa kupata dalaja la kwanza (16 ) na baadae kujiunga kidato cha tano na cha sita nikafaulu kwa dalaja la kwanza (9) basi kama ilivyo furaha ya wengi hata mimi mwenzenu mimefanikiwa kuchaguliwa Bachelor of science in nursing university of Dodoma na kupata mkopo 4,032,500/= lakini baada ya kusikia kuwa mtu anapopata GPA kali mfano 5 inakuwa ni lahisi kutoka kielimu na pengine kubakizwa chuoni kuwa tutorial lecturer nimekuja kwenu wa jf na great thinkers muweze kunipa/kutupa mawazo au ushauri sisi sote ili kuepukana na supplementary, kuto disco na hatimae kupata GPA kali hili kuweza kukomboa familia kama yangu na zaidi kupata elimu ambayo itakuwa ya manufaa kwa jamii na wala si elimu ya kukariri ukizingatiwa nitadili na afya ya binadamu. ASANTE KWA KUNISIKILIZA , NAKARIBISHA MAWAZO/ Ushauri WENU.