Jinsi ya kukabiliana na ushindani wa wanaume wengine kwa mwenza wako

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,319
33,125
KATIKA uhusiano wa kimapenzi hakuna kosa kubwa kwa wanaume kama kutojiamini na mbaya zaidi kutomwamini mwenza wake. Kumekuwa na dhana kuwa tatizo la wivu lipo sana kwa wanawake kuliko wanaume, jambo ambalo si la kweli kwani hata wanaume nao husumbuliwa sana na ugonjwa huo.

Tofauti ni kwamba wanaume wengi hufahamu namna ya kukabiliana na wivu na asilimia kubwa hujitahidi kutoonesha hisia zao wanapokutwa na hali hiyo.

Hata hivyo pamoja na jitihada hizo, ni dhahiri kuwa bado wanaume wengi hushindwa kukabiliana na ushindani wa wanaume wenzao hasa wale wanaoonesha kuwa na hisia kwa mwanamke mmoja. Tatizo kubwa linalowasumbua inapotokea jambo kama hilo ni wivu na kutojiamini kama wanaweza kuvuta hisia za mwanamke huyo na kuwashinda wanaume wengine wenye nia kama hiyo.

Tatizo la kutojiamini mara zote humpa shida mwanamume na kumfanya siku zote awe na mashaka kuwa huenda akaja mwanamume mwingine mwenye sifa kuliko yeye na kumchukua mwenza wake.

Kwanza tatizo hilo ni kubwa na baya kwa mwanamume kwa vile hutawala mawazo yake na kutengeneza fikra za uongo kuwa hana sifa zinazostahili kuweza kushinda hisia za mwanamke anayempenda. Tatizo hilo huzidi kuwa baya zaidi pale mwanamume huyo anapotoka na mwenza wake huyo na kushuhudia wanaume wengine wanavyomkodolea macho ya kumtamani.

Hali hiyo huongeza tatizo la kutojiamini kwa mwanamume huyo na kuzaa tatizo lingine kubwa la wivu na hivyo kumfanya mwanamume ashindwe kabisa kukabiliana na ushindani wa wanaume wengine.

Wivu ni hisia kubwa ambayo humtawala binadamu, na mara nyingi humfanya mtu afikie hatua ya kumuua ampendaye, hisia hizi si binadamu tu ndiye aliyejaliwa kuwa nazo bali hata wanyama, ni hisia za asili.

Hata hivyo katika suala la ushindani na mwanamume mwenzako juu ya mwanamke mnayempenda, hisia hizi za wivu hazisaidii kitu zaidi ya kukupatia hasira ambazo zitakufanya usijiamini na kukuharibia kabisa.

Pamoja na hayo wivu pia unaweza kukufanya ufanye mambo ya kijinga na aibu kama vile kupigana kwa vile hisia hizo huwa na tabia ya kutawala mawazo na matendo yako bila kujali matokeo yake.

Ili kukabiliana na hali hiyo mwanamume unapokutana na mwanamume mwenzako ambaye anaonesha hisia zake waziwazi kwa mwenza wako usithubutu kuonesha woga au wasiwasi, wivu na kutojiamini. Kwani ukionesha hisia hizo moja kwa moja mwanamume mwenzako atajisikia kuwa ana uwezo mkubwa wa kuwa na mwenza wako kuliko wewe, na mbaya zaidi ni pale mwenza wako atakapogundua kuwa hujiamini.

Jambo la maana la kufanya ni kujiamini na kuepukana na tatizo la wivu na kubwa zaidi ni kutambua kuwa udhaifu wowote katika hilo unaweza kukupotezea mwanamke umpendaye. Pia jambo jingine la kukabiliana na ushindani wa wanaume wengine ni kwa mwanamume kujiandaa na kutarajia hali kama hiyo kabla hajatoka na mwenza wake, hali ambayo itamfanya asishangae au kuwa na wasiwasi wanaume wengine watakapomtamani mwenza wake.

Kumbuka ili uweze kujijengea heshima, uwezo na uaminifu kwa mwenza wako ni kuondokana na wasiwasi, woga, kutojiamini na mbaya zaidi wivu hasa unapokuwa na mwenza wako. Kwa hilo hata wanaume wenzako watakuheshimu na kushindwa kumwingia mwenza wako kwa vile umeonesha dhahiri huna lolote la kukupatia hofu mbele yao.
 
KATIKA uhusiano wa kimapenzi hakuna kosa kubwa kwa wanaume kama kutojiamini na mbaya zaidi kutomwamini mwenza wake. Kumekuwa na dhana kuwa tatizo la wivu lipo sana kwa wanawake kuliko wanaume, jambo ambalo si la kweli kwani hata wanaume nao husumbuliwa sana na ugonjwa huo.

Tofauti ni kwamba wanaume wengi hufahamu namna ya kukabiliana na wivu na asilimia kubwa hujitahidi kutoonesha hisia zao wanapokutwa na hali hiyo.

Hata hivyo pamoja na jitihada hizo, ni dhahiri kuwa bado wanaume wengi hushindwa kukabiliana na ushindani wa wanaume wenzao hasa wale wanaoonesha kuwa na hisia kwa mwanamke mmoja. Tatizo kubwa linalowasumbua inapotokea jambo kama hilo ni wivu na kutojiamini kama wanaweza kuvuta hisia za mwanamke huyo na kuwashinda wanaume wengine wenye nia kama hiyo.

Tatizo la kutojiamini mara zote humpa shida mwanamume na kumfanya siku zote awe na mashaka kuwa huenda akaja mwanamume mwingine mwenye sifa kuliko yeye na kumchukua mwenza wake.

Kwanza tatizo hilo ni kubwa na baya kwa mwanamume kwa vile hutawala mawazo yake na kutengeneza fikra za uongo kuwa hana sifa zinazostahili kuweza kushinda hisia za mwanamke anayempenda. Tatizo hilo huzidi kuwa baya zaidi pale mwanamume huyo anapotoka na mwenza wake huyo na kushuhudia wanaume wengine wanavyomkodolea macho ya kumtamani.

Hali hiyo huongeza tatizo la kutojiamini kwa mwanamume huyo na kuzaa tatizo lingine kubwa la wivu na hivyo kumfanya mwanamume ashindwe kabisa kukabiliana na ushindani wa wanaume wengine.

Wivu ni hisia kubwa ambayo humtawala binadamu, na mara nyingi humfanya mtu afikie hatua ya kumuua ampendaye, hisia hizi si binadamu tu ndiye aliyejaliwa kuwa nazo bali hata wanyama, ni hisia za asili.

Hata hivyo katika suala la ushindani na mwanamume mwenzako juu ya mwanamke mnayempenda, hisia hizi za wivu hazisaidii kitu zaidi ya kukupatia hasira ambazo zitakufanya usijiamini na kukuharibia kabisa.

Pamoja na hayo wivu pia unaweza kukufanya ufanye mambo ya kijinga na aibu kama vile kupigana kwa vile hisia hizo huwa na tabia ya kutawala mawazo na matendo yako bila kujali matokeo yake.

Ili kukabiliana na hali hiyo mwanamume unapokutana na mwanamume mwenzako ambaye anaonesha hisia zake waziwazi kwa mwenza wako usithubutu kuonesha woga au wasiwasi, wivu na kutojiamini. Kwani ukionesha hisia hizo moja kwa moja mwanamume mwenzako atajisikia kuwa ana uwezo mkubwa wa kuwa na mwenza wako kuliko wewe, na mbaya zaidi ni pale mwenza wako atakapogundua kuwa hujiamini.

Jambo la maana la kufanya ni kujiamini na kuepukana na tatizo la wivu na kubwa zaidi ni kutambua kuwa udhaifu wowote katika hilo unaweza kukupotezea mwanamke umpendaye. Pia jambo jingine la kukabiliana na ushindani wa wanaume wengine ni kwa mwanamume kujiandaa na kutarajia hali kama hiyo kabla hajatoka na mwenza wake, hali ambayo itamfanya asishangae au kuwa na wasiwasi wanaume wengine watakapomtamani mwenza wake.

Kumbuka ili uweze kujijengea heshima, uwezo na uaminifu kwa mwenza wako ni kuondokana na wasiwasi, woga, kutojiamini na mbaya zaidi wivu hasa unapokuwa na mwenza wako. Kwa hilo hata wanaume wenzako watakuheshimu na kushindwa kumwingia mwenza wako kwa vile umeonesha dhahiri huna lolote la kukupatia hofu mbele yao.
Haya bwana wamesikia!! wapi yo yo? mkurugenzi Fidel mmesikia hayo?nasikia kwa wivu wazee mpaka mnakondeana
 
Wivu huua!Unakuua wewe mwenye wivu polepole..ila kabla hujakata roho wawezasababisha madhara kwa wengine.
 
hilo tatizo mara nyingi utakuta watu wanapoteza uaminifu ktk mapenzi na hua mwanzo wa kutafuta small nyumba
 
Unatakiwa uwe na wivu usizidi sana ukiwa mpole na kujiamini sana utagongewa unlimited.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom