Jinsi ya Kuacha ku-'Cheat' Mwenzi wako...

Umetupatia shule ya maana. Kwa kuanzia, Sasa hivi tu nimedelete contant ya 'kimeo'

Big up Allien!

Swadata Mkuu Katibu Kata!

One page. Hakuna lisilowezekana.

karibu Private Intelligence Club.
 
Unajua kuacha ''cheating'' sometimes inakuwa ngumu sana. Guilty feeling inakuwa inakuandama ukifikiria ''maumivu'' ya kuachwa atakayoyapata yule kimada wako. Na mara nyingi inakuwa ngumu zaidi hasa pale unapokuwa umeamua kumuacha bila kosa au sababu malaumu

Unaweza kuwa unamtafutia sababu au kose lolote ili iwe ticket ya kuchomokea - lakini pia unaweza kushangaa hakamatiki! Yupo perfect

Inawezekana lakini - from experience. Thanks Allien
 
mkuu hili nalo ni somo, ila ni ngumu sana coz ukimwacha kijumla ataumia sana bora kama inatokea nafasi unapiga kidogo then warudi kwa wife ,............ hasa pale unapomwacha bila kosa na hupendi kuona analia kwa sababu yako
 
Jinsi Ya Kuacha Ku-Cheat

Kwa sababu mbalimbali watu katika mahusiano wanaamua ku-Cheat wenzi wao. Wakati mwingine wanajisikia vibaya lakini hawaachi. Wanakuwa trapped, na hivyo kuifanya iwe tabia yao as long as hajashikwa. Wakati mwingine Cheating inachochewa pia na mahusiano mabaya na mwenzi wako, visasi na migogoro isiyotatuliwa katika mahusiano. Kuna sababu nyingi kwa nini Wenzi Wanacheat, hizo tutaongelea siku nyingine.

Wataalamu wanasema wakati mwingine ni vigumu kuacha Cheating kwa kuwa ni Addiction hata kama Ku-Chaet si kuzuri. Inasemekana unapocheat unajisikia uko fulfilled kwa namna Fulani. Ili uache unahitaji mahitaji kama: emotional au physical, yatoshelezwe na Mwenzi wako. Ikishindikana kuacha inakuwa ni ngoma nzito.


Hata hivyo hatima ya mwisho ya Cheating ni kujisikia Guilt; Aibu nk. Cheating haiongezi furaha katika mahusiano. Kwa kukusaidia inawezekana kabisa ukaacha Cheating. Zifuatazo ni dondoo zitakazokusaidia kuacha Ku-Chaeat:

1.Kwanza kaa chini na jiulize kwa nini Una-Cheat, Hii itakusaidia kukurudishia akili yako ya kibinadamu na utashi juu ya chaguzi zako katika maisha. Kitendo cha kuelewa tu ni kwa nini unatabia ya namna Fulani ambayo huiachi ni msingi mkubwa sana wa kukusaidia kuacha.

2.Chunguza values zako za maisha na jiulize kama Cheating ni moja kati ya hizo values zako. Hata kama umetokea katika familia ambazo Cheating ni kitu cha kawaida, lakini si lazima ukubaliane na chaguo la familia. Kataa.


3.Jiulize tena kama Kum-Cheat Mwenzi wako kunakuongezea au kukupunguzia heshima na je kwa kufanya hivyo, unamheshimu au haumheshimu mwenzi wako. Faida yake ni nini?

4.Fanya marejeo ya mahusiano yako na uangalie ni wapi pana mapungufu katika mapenzi na Intimacy. Hii itakusaidia kujua mahitaji yako ya kimapenzi. Ukishagundua ni rahisi sana kwako kuongea na mwenzako kwa uwazi mahitaji yako ya feelings na emotions. (NB: Tutajadili siku nyingine ni vipi uanweza kuongeza au kurejesha mapenzi kwa mwenzi wako).
Ongea na mwenzi wako kwa uwazi ni nini hasa anategemea u kutarajia kutoka katika mahusiano yenu ili kuboresha mapenzi na mahitaji yenu. Mweleze kwa uwazi hisia zako ni nini pia unataka kutoka kwake. Make her your best lover and friend. Traet your lover. Spoil her.


5.Achana kabisa na kata mawasiliano ya mara kwa mara na Kimada wako ya SMS na ya Simu. Acha kuwasiliana naye kwa email na kuchat online. Mblock au badili ID. Mpotezee. Ni kazi lakini kuwa jasiri. Inawezekana.

6.Kumbuka unaye Mwenzi na Familia yako ambao wote wanakupenda; kukuthamini na kukuheshimu na kuwa una Ahadi nayo. Hao ndiyo source peke yake ya furaha na Amani ya kweli kabla hujafa.

7.Achana na kufikiria mapungufu uliyonayo na vipi utayapata kwa njia haramu na jizuie hisia zako za kukutana na Kimada wako na weka azimio la kuachana naye. Mweleze ukweli Kimada wako kuwa huwezi kuendelea na uhusiano huu. Ataumia, lakini ni bora kwa Mwenzi na familia yako kama unaipenda.

8.Kumbuka huwezi kuacha Cheating mpaka umechukua uamuzi huo “Mzito” wa kuacha. Usisubiri “The right moment” ili uache Ku-Cheat. Just stop. Just Do It Right Away, Now. Immediately.


9.Fikiria madhara ya Ku-Chaet yatakuwa nini utakapokamatwa. Aibu na fedhea na guilt.

10.Kutana na rafiki zako wa Kike na wa Kiume ukiwa na Mwenzi wako na usifiche kitu. Usiwe na miada yap eke yako unless ni very genuine. Uvae utu upya kwani wa kale umekwisha.

11.Angalia jinsi ambavyo wewe, mwenzi wako na familia yako mlivyobarikiwa. Je huna shukrani? Ndo jinsi ya kushukuru kwa ku-Cheat?

12.Acha kabisa kum-criticise mwenzi wako na kumlinganisha na Kimada wako. Heshimu sana hisia na TRUST ya Mwenzi wako na Tumia muda mwingi na Mwenzi wako na Familia. Pia jizuie kuwa negative juu ya maisha yenu na mahusiano yenu. Stay positive and focused.


13.Kama unafikiri Kimada wako ni bora kuliko mwenzi wako wa sasa, napenda kukujulisha kuwa ni aslimia 5% ya mahusiano ambayo yanatoka na Cheating yatafanya kazi. Kwa hiyo hutaenda popote. Stop. Acha ubinafsi na mrudie mwenzako na muumba wako. Huna haja ya kuleta msongamano ndani ya mapenzi. Jiweke pembeni na mpenzi wako wa Ahadi.

14.Kwa kumwacha Kimada wako huwezi kufa bali utakuwa na Amani moyoni. Hata kama utaona ni vigumu kumwacha. Just stop. Katika kipindi cha wiki 3 baada ya kufanya uamuzi “Mzito” utakuwa umeshafaulu kiakili na utaweza ku-overcome feelings za withdrawal.

15.Chukua muda kufanya matengenezo na marekebisho katika ndoa yako. Jifunze jinsi ya kufanya mambo tofauti. Kama huwezi kukubaliana na hilo basi utawezaje kuacha. Fanya maamuzi sasa.

16. Mrudie Muumba wako. Tubu. Omba msamaha kwa muumba wako. Anza maisha yako upya. Shiriki katika mambo ya mungu na kijamii. Find new interests kufidia muda na pengo "hewa" la Cheating"

Allien

AMEN.
put a stop to cheating:hand:
 
mkuu hili nalo ni somo, ila ni ngumu sana coz ukimwacha kijumla ataumia sana bora kama inatokea nafasi unapiga kidogo then warudi kwa wife ,............ hasa pale unapomwacha bila kosa na hupendi kuona analia kwa sababu yako

Mkuu JKJ; inawezekana kuacha Kabisa. Believe me:

Tumia hizi:

8.Kumbuka huwezi kuacha Cheating mpaka umechukua uamuzi huo "Mzito" wa kuacha. Usisubiri "The right moment" ili uache Ku-Cheat. Just stop. Just Do It Right Away, Now. Immediately.

Huioni hii Mkuu ?:

6.Kumbuka unaye Mwenzi na Familia yako ambao wote wanakupenda; kukuthamini na kukuheshimu na kuwa una Ahadi nayo. Hao ndiyo source peke yake ya furaha na Amani ya kweli kabla hujafa.
 
Mkuu JKJ; inawezekana kuacha Kabisa. Believe me:

Tumia hizi:

8.Kumbuka huwezi kuacha Cheating mpaka umechukua uamuzi huo "Mzito" wa kuacha. Usisubiri "The right moment" ili uache Ku-Cheat. Just stop. Just Do It Right Away, Now. Immediately.

Huioni hii Mkuu ?:

6.Kumbuka unaye Mwenzi na Familia yako ambao wote wanakupenda; kukuthamini na kukuheshimu na kuwa una Ahadi nayo. Hao ndiyo source peke yake ya furaha na Amani ya kweli kabla hujafa.


Umenena.

Hiyo namba six ndo haswa ilikuwa pona yangu. Nikitazama vile mwenyezi Mungu kanijalia hii familia niiongoze na kuilinda, then niliona hakuna haja ya kupoteza muda, amana na staha yangu kwa sababu ya wanawake wengine no matter what! Kama wanandoa, maudhi yapo tu hata kama tutaishi mwezini au chini ya maji, lakini suluhisho kamwe si kutafuta mwenzi mwingine. Now, what I do, plan, earn is for my family bana.And this makes me the happiest man, kwamba sioni hata vile vimaudhi vya waifu.

Ubarikiwe na endelea kutupa nondo.
 
Mkuu topic yako njema sana ceteris paribas. Unakuta mwenzi wako Kama room mate vile. Kwa mwezi mara 1 na ikizidi mara 2. Na mshaongea wee mpk umechoka. Sasa unapata kigango. Kimetulia si mchezo. Kipi bora,kuwaza mpk upate stroke au kuburudika na kirefusha maisha?
 
Respect Allien!.
Nna fiance ambae nampenda na kumthamini sana, na isitoshe uko mpango wa kufunga nae pingu za maisha. Shida ni kuwa kuna dada ambae nae yuko kasi ile mbaya, na fiance wangu hayuko aware kiviile...
Kwa kutumia hizo kanuni nadhani ntaweza kumpa ukweli na ndo utakuwa mwisho, japo kwa nyakati tofauti nimekuwa niki-mcheat! Vyovyote na amini kweli itaniweka huru.

Ubarikiwe sana Allien may God give u extraodinary insight.
 
Duuh, kumbe hii ipo bado.

Just in case unahitaji kupata ushahidi usio na mashaka juu ya mwenzi wako unayemshuku anakucheat, tafadhali tuwasiliane.

Vigezo na masharti kuzingatiwa!
 
Allien una ongea kwa marejeo thabiti. Yaelekea una uzoefu mkuu. Twambie wewe uliacha baada ya kucheat mara ngapi ili tujua mihimili yetu ilipofika tujilinganishe. Hapo najua nimeongea kiswahili sanifu kabisa!!!
 
Post zingine ni very helpful. Thanks kwa somo, tatizo hilo linanisumbua sana. Naomba kama mtu anamjua mshauri nasaha wa mambo haya anielekeze. Lakini mshauri asiwe religious sana. Nataka psychologist. Mwenye msaada tuwasiliane kupitia ndandawamalenja@gmail.com. Kwa kweli nitashukuru sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom