Jinsi wanavyotuona & The Illusion of Power

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Unajua ukiwa juu unaweza kuviona vitu vyote vilivyoko chini kuwa ni vidogo; Na kwa kadiri unavyoenda juu zaidi ndivyo vitu hivyo vinaonekana kuwa vidogo zaidi. Hata hivyo ukweli wa mambo ni kuwa siyo udogo wa vitu bali ni umbali uliopo kati ya wewe na vitu hivyo ndivyo vinavyokufanya uvione kuwa vidogo. Sasa ukividharau na kuvitendea kama vile ni vidogo utakapoanguka na kujikuta umeangukia majabari kosa halitakuwa kwa majabari hayo!

Kwa muda mrefu sasa watawala wetu yaonekana wanazidi kwenda mbali na wananchi na kwa kadiri wanavyokwenda mbali ndivyo wanazidi kutuona wadogo na kutudharau. Na bila ya shaka kwa kadiri wanapigiwa makofi, wanavimulimuli kwenye misafara yao na saluti zikiangushwa kila wapitapo basi ndivyo na wenyewe wanavyojiona wako juu zaidi.

Katika hiki ambacho naweza kukiita kuwa ni kiinimacho cha madaraka (the illusion of power) basi wale walio katika madaraka hujiona kuwa siyo tu wanastahili bali ni haki yao kuwa hapo walipo. Kwa hawa wazo la "cheo ni dhamana" halipo tena na kwao cheo kinageuka kuwa "haki" yao. Kwa watu hawa ambao mawazo yao yamepotoka "kutumikia wananchi" kwao kunamaanisha "kujitumikia mwenye nchi".

Hivyo inapotokea wananchi wanapoanza kuwahoji na kuwauliza; au pale wanapotakiwa kutoa maelezo majibu yao hao watawala yanakuwa ni ya dharau (contempt) na ya kibabe. Majibu yao yanaenda kwenye wigo wa kejeli kana kwamba wao miungu wasiokufa (immortals) hawatakiwi kuulizwa maswali na binadamu wafao (mortals).

Sakata zima la ufisadi uliokubuhu ambao umepotezea nchi yetu zaidi ya Shilingi trilioni moja kwa muda mrefu ni ushahidi wa jinsi gani watawala wetu wameamua kujikweza na sisi wengine kututweza. Hadi leo hii wizi uliotokea Benki Kuu ungetosha siyo tu kumfukuzisha mtu mmoja kazi bali kuifumua benki nzima hiyo na kuinda upya.

Wakati wanajeshi wetu walipoasi mwaka 1964 na kusababisha hali ya wasiwasi nchini hadi kutaka Waingereza waingilie kati kuzima maasi hayo, uzito wake ulionekana. Ndugu zangu hoja yangu ni kuwa Benki Kuu ilikuwa imeasi Taifa na uongozi wake kufanya financial mutiny na kusababisha Taifa letu kuwa na wasiwasi. Kitendo cha kuacha watu wachache waiteke Benki Kuu na kuchota fedha za maskini wa Tanzania kwa vile tu wanaweza ni sababu tosha ya kuomba hata wageni waje waisimamie Benki Hii na hatimaye kuirudisha kwenye mikono ya Watanzania.

Leo hii waliopewa jukumu la kuchunguzu suala la EPA wanatetemeka mbele ya wezi wa mali zetu na kama wanaogwaya mbele ya mizimu wanawabembeleza watuachilie. NI kama vile tumewekewa nira kwenye shingo zetu na tunatumikishwa pasipo ridhaa yetu! Saa imefika ya kuvunja nira hiyo na kugoma kuwalimia mashamba yao na kuwaparuia nafaka zao!

Tutaweza vipi kuongozwa na watu ambao wanatuzuga? Ni kweli sanduku la kura litawaamulia lakini hatutafika huko hadi tukatae katika fikra na mawazo yetu kuwa na viongozi kama hawa licha ya uzuri wa nyimbo zao, na umahiri wa rangi za nguo zao! Lazima tuwakatae katika fikra zetu kuwa wameshindwa kuliongoza Taifa letu na kimsingi wanajiongoza wao wenyewe kufikia mafanikio ya watoto na wana familia zao!

Leo hii baada ya kuuliza sana Mkapa anaenda kulia na yeye ni Bangusilo na ya kuwa ameonewa na kusingiziwa hivi wanatuchukuliaje sisi? Binafsi sitaki kusikia tena maneno yao hasa ya kizugaji hadi pale kwenye suala la Ballali kwanza watakapotoa majibu ya maswali nitakayowavurumishia kesho!

Sitaki tena kuzugwa, sitaki kufanywa duni, sitaki kuonwa mdogo, sitaki tena kuburuzwa kama debe liburuzwazo na gari mkweche! Sitaki tena kuambiwa "Serikali imesema" halafu iwe mwisho. Nataka serikali ikisema iseme kitu ambacho kinaeleweka, chenye ukweli, ukweli mtupu, na ukweli wote! Sitaki tena kusikia kuwa kuna mtu anaoenewa.

Wito wangu kwa watawala wetu!! Sitisheni mazungumzo na mafisadi, ichukueni nchi yetu kwa nguvu toka mikononi mwao, na vunjeni majadiliano yenu na wezi!! Imetosha kuwabembeleza, imetosha kukaa nao na kuwaomba waturidishie mali zetu! Wakati umefika kama kuwaachia hizo fedha zetu tuwaachie lakini tunataka waiachilie nchi yetu ili na sisi hatimaye tupate nafasi ya kuijenga nchi yetu sisi wenyewe!!

Mkataba na kuzimu lazima ukome, na majadiliano na mapepo yasitishwe!! Tunataka uhuru wetu, uhuru wa kufikiri, uhuru wa kutenda, uhuru wa kupata habari za kweli, uhuru wa kuwapinga usiku na mchana, uhuru wa kuamua na kwenda!! Tunataka uhuru wetu wa kuwa na Taifa la kisasa tukinyang'anya ukiritimba wa madaraka yao na kuwapora ubwanyenye wa uhodhi wa mamlaka yao.

Kama wanatuona sisi ni duni na wadogo kwa vile wao wako mbali... ngoja basi watuone kwa kadiri tunavyowasogelea karibu! Watakimbia~~!
 
Unajua ukiwa juu unaweza kuviona vitu vyote vilivyoko chini kuwa ni vidogo; Na kwa kadiri unavyoenda juu zaidi ndivyo vitu hivyo vinaonekana kuwa vidogo zaidi. Hata hivyo ukweli wa mambo ni kuwa siyo udogo wa vitu bali ni umbali uliopo kati ya wewe na vitu hivyo ndivyo vinavyokufanya uvione kuwa vidogo. Sasa ukividharau na kuvitendea kama vile ni vidogo utakapoanguka na kujikuta umeangukia majabari kosa halitakuwa kwa majabari hayo!

Kwa muda mrefu sasa watawala wetu yaonekana wanazidi kwenda mbali na wananchi na kwa kadiri wanavyokwenda mbali ndivyo wanazidi kutuona wadogo na kutudharau. Na bila ya shaka kwa kadiri wanapigiwa makofi, wanavimulimuli kwenye misafara yao na saluti zikiangushwa kila wapitapo basi ndivyo na wenyewe wanavyojiona wako juu zaidi.

Katika hiki ambacho naweza kukiita kuwa ni kiinimacho cha madaraka (the illusion of power) basi wale walio katika madaraka hujiona kuwa siyo tu wanastahili bali ni haki yao kuwa hapo walipo. Kwa hawa wazo la "cheo ni dhamana" halipo tena na kwao cheo kinageuka kuwa "haki" yao. Kwa watu hawa ambao mawazo yao yamepotoka "kutumikia wananchi" kwao kunamaanisha "kujitumikia mwenye nchi".

Hivyo inapotokea wananchi wanapoanza kuwahoji na kuwauliza; au pale wanapotakiwa kutoa maelezo majibu yao hao watawala yanakuwa ni ya dharau (contempt) na ya kibabe. Majibu yao yanaenda kwenye wigo wa kejeli kana kwamba wao miungu wasiokufa (immortals) hawatakiwi kuulizwa maswali na binadamu wafao (mortals).

Sakata zima la ufisadi uliokubuhu ambao umepotezea nchi yetu zaidi ya Shilingi trilioni moja kwa muda mrefu ni ushahidi wa jinsi gani watawala wetu wameamua kujikweza na sisi wengine kututweza. Hadi leo hii wizi uliotokea Benki Kuu ungetosha siyo tu kumfukuzisha mtu mmoja kazi bali kuifumua benki nzima hiyo na kuinda upya.

Wakati wanajeshi wetu walipoasi mwaka 1964 na kusababisha hali ya wasiwasi nchini hadi kutaka Waingereza waingilie kati kuzima maasi hayo, uzito wake ulionekana. Ndugu zangu hoja yangu ni kuwa Benki Kuu ilikuwa imeasi Taifa na uongozi wake kufanya financial mutiny na kusababisha Taifa letu kuwa na wasiwasi. Kitendo cha kuacha watu wachache waiteke Benki Kuu na kuchota fedha za maskini wa Tanzania kwa vile tu wanaweza ni sababu tosha ya kuomba hata wageni waje waisimamie Benki Hii na hatimaye kuirudisha kwenye mikono ya Watanzania.

Leo hii waliopewa jukumu la kuchunguzu suala la EPA wanatetemeka mbele ya wezi wa mali zetu na kama wanaogwaya mbele ya mizimu wanawabembeleza watuachilie. NI kama vile tumewekewa nira kwenye shingo zetu na tunatumikishwa pasipo ridhaa yetu! Saa imefika ya kuvunja nira hiyo na kugoma kuwalimia mashamba yao na kuwaparuia nafaka zao!

Tutaweza vipi kuongozwa na watu ambao wanatuzuga? Ni kweli sanduku la kura litawaamulia lakini hatutafika huko hadi tukatae katika fikra na mawazo yetu kuwa na viongozi kama hawa licha ya uzuri wa nyimbo zao, na umahiri wa rangi za nguo zao! Lazima tuwakatae katika fikra zetu kuwa wameshindwa kuliongoza Taifa letu na kimsingi wanajiongoza wao wenyewe kufikia mafanikio ya watoto na wana familia zao!

Leo hii baada ya kuuliza sana Mkapa anaenda kulia na yeye ni Bangusilo na ya kuwa ameonewa na kusingiziwa hivi wanatuchukuliaje sisi? Binafsi sitaki kusikia tena maneno yao hasa ya kizugaji hadi pale kwenye suala la Ballali kwanza watakapotoa majibu ya maswali nitakayowavurumishia kesho!

Sitaki tena kuzugwa, sitaki kufanywa duni, sitaki kuonwa mdogo, sitaki tena kuburuzwa kama debe liburuzwazo na gari mkweche! Sitaki tena kuambiwa "Serikali imesema" halafu iwe mwisho. Nataka serikali ikisema iseme kitu ambacho kinaeleweka, chenye ukweli, ukweli mtupu, na ukweli wote! Sitaki tena kusikia kuwa kuna mtu anaoenewa.

Wito wangu kwa watawala wetu!! Sitisheni mazungumzo na mafisadi, ichukueni nchi yetu kwa nguvu toka mikononi mwao, na vunjeni majadiliano yenu na wezi!! Imetosha kuwabembeleza, imetosha kukaa nao na kuwaomba waturidishie mali zetu! Wakati umefika kama kuwaachia hizo fedha zetu tuwaachie lakini tunataka waiachilie nchi yetu ili na sisi hatimaye tupate nafasi ya kuijenga nchi yetu sisi wenyewe!!

Mkataba na kuzimu lazima ukome, na majadiliano na mapepo yasitishwe!! Tunataka uhuru wetu, uhuru wa kufikiri, uhuru wa kutenda, uhuru wa kupata habari za kweli, uhuru wa kuwapinga usiku na mchana, uhuru wa kuamua na kwenda!! Tunataka uhuru wetu wa kuwa na Taifa la kisasi tukinyang'anya ukiritimba wa madaraka yao!

Kama wanatuona sisi ni duni na wadogo kwa vile wao wako mbali... ngoja basi watuone kwa kadiri tunavyowasogelea karibu! Watakimbia
~~!

Mimi nilishajiandaaa na episode two ya hii series....

background music ni ile ile ya tarantata ta ta nta tanta .. hii ni remix...
 
Wito wangu kwa watawala wetu!! Sitisheni mazungumzo na mafisadi, ichukueni nchi yetu kwa nguvu toka mikononi mwao, na vunjeni majadiliano yenu na wezi!!

Inference ya huu wito ni kwamba Watawala na mafisadi ni watu tofauti!

Nakataa!
 
kesho!

Sitaki tena kuzugwa, sitaki kufanywa duni, sitaki kuonwa mdogo, sitaki tena
!
THEY FEAR YOU BECAUSE YOU ARE YOUNG,THEY FEAR YOU BECAUS YOUR THE FEATURE,, HOW FEARFUL THEY MUST BE THAT THAT THEY SHOT YOU CHILDREN ,HOW POWERFUL YOU MUST BE THAT THEY FEAR YOU SO MUCH,YOUR POWERFUL BECAUSE YOUR GENERATOR OF FREDOM. BISHOP TUTU
 
Wito wangu kwa watawala wetu!! Sitisheni mazungumzo na mafisadi, ichukueni nchi yetu kwa nguvu toka mikononi mwao, na vunjeni majadiliano yenu na wezi!! Imetosha kuwabembeleza, imetosha kukaa nao na kuwaomba waturidishie mali zetu! Wakati umefika kama kuwaachia hizo fedha zetu tuwaachie lakini tunataka waiachilie nchi yetu ili na sisi hatimaye tupate nafasi ya kuijenga nchi yetu sisi wenyewe!!

MMKijiji! Great post.

Nimekaa nimetafakari sana. nimekwenda to the extent ya kumuhoji Mugu..inakuwaje? Mungu yule yule wa wimbo wetu wa Taifa..! INAKUWAJE!

Inakuwaje hasa Kwa Tanzania ninayoijua...?

Inwezekaneje Tanzania iliyotolewa jasho na watu muhimu..iwe hivi ilivyo? Kirahisi tu!

Ni kweli haya yanatokea? Tena kwa haraka hivi?

Nimekuja na mtizamo mmoja tu!

Oh..Kumbeee UJINGA hauchagui size ya Mtu kwa urefu, umri, kimo, kitambi, kisomo, kiwango cha uongozi, umashuhuri na dimension nyingine nyingi physicaly , chemicaly etc. UJINGA NI UJINGA TU!!

Nimegundua kuwa kuna mahali nilikuwa nimekosea..nafikiri nilikuwa brainwashed..sina hakika kuwa ilikuwa ni shuleni, mtaani, kanisani, tarafani au wapi..lakini matukio yanatokea Tanzania sasa hivi yananilazimu ni elewe kuwa UJINGA umekita nyanja ya Uongozi wa Taifa.

Kuna Ujinga usioelezeka.

Kinachonishangaza ni kuwa inakuwaje ujinga uwe na nguvu kiasi hiki? Ok..Inabidi nilazimeke kujifunza tena anatomy ya Ujinga.

Inakuwaje Wajinga kiasi hiki watuongoze..na kama sisi sio kama wao..mbona hakuna kianachotokea against them..? au ndiyo illusion yenyewe?? Au ndio sisi na sio wao? This must be proved very soon!

Leo ni EPA..Kesho Vijipesa..kkutwa hiki...next wiki "kafa hajafa.." Ujinga mtupu!

Lakni ..vipi..sisi amabo sio kama wao tunaogozwa nao?

Realy suprising, Wapi tunakosea? Au wao wapi wanapatia..Ni realative i think!!

Anyway....niseme very clearly kwa Hawa viongozi..maana nafikiri kwa Illusion iliyopo..wao wanafikiri sisi niwajinga..na sisi tunafikiri wao ni wajinga..Lakini..ukweli upo karibuni..kabisa..Nitaeleza jinsi Illusion inavyowezekana kuwa broken down kirahisi tu!

Kwa illusion ..!!

Fisi mwenye njaa akiona Taswira ya mwenzi mchanga kwenye bwawa la maji..kwenye fikra zake finyu na njaa na uroho unaomsukuma anapata picha kuwa ule ni mfupa umeanguka barabarani..anarukia kwenye maji anayoyaona kama barabara na ANAZAMA.... So? imekwesha. Maani huyu fisi kiukweli ni limbukeni tu..nani haoni hivyo?

Viongozi wetu!

I tell you this...You are seriously in deep state of "illusion of power" and we know how to work thisout to our advantage..na karibuni mtarukia kwenye dimbwi la kina kirefu mkifuata Mfupa sorry EPA..na kwa kweli mtazama.. This is not a joke..... but and ...

But

You still have a chance to recover your diginity..njooni majukwaani..RUDISHENI NCHI YETU...nini kigumu hapo?... Tuwasiliane!!!
 
Inference ya huu wito ni kwamba Watawala na mafisadi ni watu tofauti!

Nakataa!


Kuhani Mkuu.. mafisadi ni zaidi ya watawala wetu. Wapo mafisadi kwenye watawala na wapo mafisadi nje ya watawala; kitu kimoja kinachowaunganisha ni ufisadi wao. Hivyo wale walioko nje ya utawala wanalala kitanda kimoja na mafisadi walio madarakani na matokeo yake wanazalisha vitendo vya kifisadi katika taasisi, mashirika na idara mbalimbali.

Si watawala wetu wote ni mafisadi, lakini mafisadi wote wangekuwa na nguvu wangependa kututawala. Ndio maana tunalia leo nira yao na ivunjwa na ndoa yao haramu ya mkeka ikomeshwe! Tunataka watawala wetu warudishe posa zao za mafisadi, na wawe huru kuolewa tena na uzalendo! Wale wazalendo waliobakia katika nafasi za uongozi wakati wao umefika wa kudai Taifa lao badala ya kuwaacha wenzao mafisadi waendeleze libeneke la ukuwadi wa mafisadi.

Kwa namna yoyote ile mafisadi wapigwe vita; wawe madarakani au nje ya madaraka; wawe wasomi au siyo wasomi; wanaotutawala au wanaotaka kututawala! Kwa hili hakuna mswalie Mtume tena!!
 
Unajua ukiwa juu unaweza kuviona vitu vyote vilivyoko chini kuwa ni vidogo; Na kwa kadiri unavyoenda juu zaidi ndivyo vitu hivyo vinaonekana kuwa vidogo zaidi. Hata hivyo ukweli wa mambo ni kuwa siyo udogo wa vitu bali ni umbali uliopo kati ya wewe na vitu hivyo ndivyo vinavyokufanya uvione kuwa vidogo. Sasa ukividharau na kuvitendea kama vile ni vidogo utakapoanguka na kujikuta umeangukia majabari kosa halitakuwa kwa majabari hayo!

Kwa muda mrefu sasa watawala wetu yaonekana wanazidi kwenda mbali na wananchi na kwa kadiri wanavyokwenda mbali ndivyo wanazidi kutuona wadogo na kutudharau. Na bila ya shaka kwa kadiri wanapigiwa makofi, wanavimulimuli kwenye misafara yao na saluti zikiangushwa kila wapitapo basi ndivyo na wenyewe wanavyojiona wako juu zaidi.

Katika hiki ambacho naweza kukiita kuwa ni kiinimacho cha madaraka (the illusion of power) basi wale walio katika madaraka hujiona kuwa siyo tu wanastahili bali ni haki yao kuwa hapo walipo. Kwa hawa wazo la "cheo ni dhamana" halipo tena na kwao cheo kinageuka kuwa "haki" yao. Kwa watu hawa ambao mawazo yao yamepotoka "kutumikia wananchi" kwao kunamaanisha "kujitumikia mwenye nchi".

Hivyo inapotokea wananchi wanapoanza kuwahoji na kuwauliza; au pale wanapotakiwa kutoa maelezo majibu yao hao watawala yanakuwa ni ya dharau (contempt) na ya kibabe. Majibu yao yanaenda kwenye wigo wa kejeli kana kwamba wao miungu wasiokufa (immortals) hawatakiwi kuulizwa maswali na binadamu wafao (mortals).

Sakata zima la ufisadi uliokubuhu ambao umepotezea nchi yetu zaidi ya Shilingi trilioni moja kwa muda mrefu ni ushahidi wa jinsi gani watawala wetu wameamua kujikweza na sisi wengine kututweza. Hadi leo hii wizi uliotokea Benki Kuu ungetosha siyo tu kumfukuzisha mtu mmoja kazi bali kuifumua benki nzima hiyo na kuinda upya.

Wakati wanajeshi wetu walipoasi mwaka 1964 na kusababisha hali ya wasiwasi nchini hadi kutaka Waingereza waingilie kati kuzima maasi hayo, uzito wake ulionekana. Ndugu zangu hoja yangu ni kuwa Benki Kuu ilikuwa imeasi Taifa na uongozi wake kufanya financial mutiny na kusababisha Taifa letu kuwa na wasiwasi. Kitendo cha kuacha watu wachache waiteke Benki Kuu na kuchota fedha za maskini wa Tanzania kwa vile tu wanaweza ni sababu tosha ya kuomba hata wageni waje waisimamie Benki Hii na hatimaye kuirudisha kwenye mikono ya Watanzania.

Leo hii waliopewa jukumu la kuchunguzu suala la EPA wanatetemeka mbele ya wezi wa mali zetu na kama wanaogwaya mbele ya mizimu wanawabembeleza watuachilie. NI kama vile tumewekewa nira kwenye shingo zetu na tunatumikishwa pasipo ridhaa yetu! Saa imefika ya kuvunja nira hiyo na kugoma kuwalimia mashamba yao na kuwaparuia nafaka zao!

Tutaweza vipi kuongozwa na watu ambao wanatuzuga? Ni kweli sanduku la kura litawaamulia lakini hatutafika huko hadi tukatae katika fikra na mawazo yetu kuwa na viongozi kama hawa licha ya uzuri wa nyimbo zao, na umahiri wa rangi za nguo zao! Lazima tuwakatae katika fikra zetu kuwa wameshindwa kuliongoza Taifa letu na kimsingi wanajiongoza wao wenyewe kufikia mafanikio ya watoto na wana familia zao!

Leo hii baada ya kuuliza sana Mkapa anaenda kulia na yeye ni Bangusilo na ya kuwa ameonewa na kusingiziwa hivi wanatuchukuliaje sisi? Binafsi sitaki kusikia tena maneno yao hasa ya kizugaji hadi pale kwenye suala la Ballali kwanza watakapotoa majibu ya maswali nitakayowavurumishia kesho!

Sitaki tena kuzugwa, sitaki kufanywa duni, sitaki kuonwa mdogo, sitaki tena kuburuzwa kama debe liburuzwazo na gari mkweche! Sitaki tena kuambiwa "Serikali imesema" halafu iwe mwisho. Nataka serikali ikisema iseme kitu ambacho kinaeleweka, chenye ukweli, ukweli mtupu, na ukweli wote! Sitaki tena kusikia kuwa kuna mtu anaoenewa.

Wito wangu kwa watawala wetu!! Sitisheni mazungumzo na mafisadi, ichukueni nchi yetu kwa nguvu toka mikononi mwao, na vunjeni majadiliano yenu na wezi!! Imetosha kuwabembeleza, imetosha kukaa nao na kuwaomba waturidishie mali zetu! Wakati umefika kama kuwaachia hizo fedha zetu tuwaachie lakini tunataka waiachilie nchi yetu ili na sisi hatimaye tupate nafasi ya kuijenga nchi yetu sisi wenyewe!!

Mkataba na kuzimu lazima ukome, na majadiliano na mapepo yasitishwe!! Tunataka uhuru wetu, uhuru wa kufikiri, uhuru wa kutenda, uhuru wa kupata habari za kweli, uhuru wa kuwapinga usiku na mchana, uhuru wa kuamua na kwenda!! Tunataka uhuru wetu wa kuwa na Taifa la kisasi tukinyang'anya ukiritimba wa madaraka yao!

Kama wanatuona sisi ni duni na wadogo kwa vile wao wako mbali... ngoja basi watuone kwa kadiri tunavyowasogelea karibu! Watakimbia~~!

Mkuu sina la kuongeza hapa maana ninaweza kuharibu ila nasema HUU NI MSUMARI maana siku zote hawapendi kusikia ukweli.
 
Rev. Kishoka,
Mkuu sasa nakuelewa vizuri... ama kweli tumshukuru Mungu... Watanzania wameamka.
Unajua mkuu tukiwa vitani wanajeshi kupata usingizi na kushusha guard zao wakijua wana walinzi imara, lakini kama ulinzi hauaminiki basi hata usingizi hukosekana na kila mtu huwa mlinzi wa usiku huo.
Tanzania ya leo kutokana na uzmebe wa ulinzi wa kiongozi wetu, umetufanya sote tuwe macho na kwa mara ya kwanz aktk historia ya nchi yetu wananchi wamekuwa macho wakishtuka hata jani likitikisika baada ya kupoteza mali zetu kibao...
Sasa hivi ni wakati adui zetu wanafahamu kuwa usiku hakuna aliyelala na mchana ni vita tuu.. kweli tutachoka sana lakini halali mtu hadi kieleweke!..
Hatuna mlinzi tufanyeje?
 
Rev. Kishoka,
Mkuu sasa nakuelewa vizuri... ama kweli tumshukuru Mungu... Watanzania wameamka.
Unajua mkuu tukiwa vitani wanajeshi kupata usingizi na kushusha guard zao wakijua wana walinzi imara, lakini kama ulinzi hauaminiki basi hata usingizi hukosekana na kila mtu huwa mlinzi wa usiku huo.
Tanzania ya leo kutokana na uzmebe wa ulinzi wa kiongozi wetu, umetufanya sote tuwe macho na kwa mara ya kwanz aktk historia ya nchi yetu wananchi wamekuwa macho wakishtuka hata jani likitikisika baada ya kupoteza mali zetu kibao...
Sasa hivi ni wakati adui zetu wanafahamu kuwa usiku hakuna aliyelala na mchana ni vita tuu.. kweli tutachoka sana lakini halali mtu hadi kieleweke!..
Hatuna mlinzi tufanyeje?


Ahh at last nimeanza kupata support ya walioelewa maana halisi! I am glad sasa naeleweka and you may share the "gospel" with Bubu ambaye ni Tomaso!
 
wazee wa zamani walisema "joto la fedha", wakimaanisha kuw mtu akiwa karibu na fedha (japo si zake, au amekopa), hupata joto fulani na kuanza kutenda vitendo vya kushangaza.

hawa viongizi wetu nao naona wamekubwa na maradhi haya haya ya joto la fedha. wengi utawaona wema wanapokuwa katika ngazi za chini ya serikali, wakipata nafasi tu ya kuwa juu, joto linawaingia na huanza kufanya vitendo katili kwa jamii yao.

wajuwe kuwa wananchi wameshajua kama wao wanasumbuliwa na maradhi kama maradhi mengine, na kwa vile wananchi wanawapenda viongozi wao, wapo katika jitihada za kuwapatia dawa itakayowatoa katika maradhi yao.

maradhi si kilema, maradhi kupatiwa dawa na yakapoa........karibu tutawaponesha viongozi kwa lazima.

mwaka huu hatutaki aliyeko juu msubiri chini, mwaka huu aliyeko juu tutamfata huko huko juu tukampe dawa size yake.
 
Kitu kimoja ambacho wanashindwa kuelewa ni kwamba uongozi(kama sio utawala) wao una mwanzo na mwisho, Siku moja, siku moja ambayo naijua ipo ingawa wao hawataki kuiona uongozi huo utashikwa na watu wenye uchungu na nchi yao, watu wanaoamini kwamba No one owns Tanzania, but that we are only borrowing it from future generations who will one day ask us what have we done to protect it.
Na siku hiyo itakuja ,na ni wale wenye busara tu ndio wanaweza kuona siku hiyo, kama nabii Nuhu ilivyoweza kuiona siku ya ghalka ya maji, na ni kumbukumbu za matendo yao ndizo zitakazo toa tofauti ya yule aliyekuawa kiongozi wa Kweli na Mtawala, kama itakavyokuwa kwenye vitabu vya kumbukumbu ya mja siku ya paradiso.
Mimi siku hiyo naiona , nona jinsi mafisadi watakavyolia na kusaga meno,naona watakavyo kana mali zao kama wanavyoanza kukana Meremeta na Tangold lakini itakuwa too late.Watawaita watawala wakipindi hicho wasaliti lakini hawatajari kwani wananchi watawaona kama mitume ilyotumwa na mora wao baada ya kusikia kilio chao kwa muda mrefu, kama alivyo kisikia kilio cha wana Islaeli kule Misri.
Ndio mimi naiona siku hiyo labda ni illusion na day dreams lakini na hisi hata baadhi ya wana JF humu wanaiona siku hiyo!
Je wewe unaiona?
 
Kuanguka kwao kutakuwa ni kwa kujitakia! Wamejitwisha wenyewe mzigo wasioweza kuubeba na sasa migongo inawauma; wanaona aibu kuutua, na kwenda mbele wana demadema!!
 
naona Tanzania Daima wamesita kutoa makala niliyowatumia.. wametoa ya zamani.... well ilihitaji ujasiri siwalaumu. Nitawabandikia kwenye klhnews nikidamka.
 
Jamani hawa watawala bado wako mbali sana na wananchi ndo maana hata vitu kama kifo cha balali wanasema ni kifo cha kawaida wakati wao wenyewe wamejenga mazingira ya kukifanya kisiwe kifo cha kawaida, bado hawajajua kuwa watanzania wamesha amka na kuwa jabali kubwa linalowasubiri waanguke na kujipigiza wenyewe, bado wanaona kama watanzania ni mbumbu wanakubaliana na kila kitu ilimradi serikali imesema, bado wanafikiri watanzania hawawezi kuunganisha dots na kupata jawabu na wanasema kila mtu na ya kwake na kuja kukanusha kwa kumvisha msemaji wa mwanzo personal statement ili lisijulikane kama ni la serikali wakati huo wanawatusha wapinzania personal statement kama ni za vyama vyao.

Labda wanaowapenda wajaribu kuwapigia ngoma ili wawaonyeshe jabali wataloangukia na kusambalatika kama pande la mchanga lianavojipigiza kwenye mwamba, lakini kwa walivyo hata wakisikia ngoma kama inayopigwa na Judge Warioba hawataangalia chini kuna nini wataendelea kushuka kwa kasi wakati wao wakijua kuwa bado wanapanda.

Wananchi wenyewe wamejaribu kuwapigia ngoma lakini bado watawala hawa wanaendele kuwateua manaodha wao wanaosahau kuangalia chini wanakoshukia wakijua kuwa wanapanda wakati wanashuka.
 
o REV WHY DISTABING GOD BY EMPTY THANKS OVER THIS MINISTER OF FOREGN AFFAIRS.

No we need to thank God for giving us JK, otherwise everything would be a secret that should not leave the wall intended to stay, and perhaps JF would have already banned from air and no ground to talk freely.
 
Back
Top Bottom