kama hili hulioni, macho yako yana kutu
meliona mie jini, langamiza wetu watu
zaidi ya subiani, kiziwi kupewa tutu
jini hili jini gani, chano chake damu zetu?
Mbona mekaa kimya, au jini mwamogopa?
hata kama hana haya, vidonge vyake tampa
mie sioni vibaya, kwa mola wangu naapa
dawa ya baya ubaya, si museme hapa hapa!
Hili ni jukwaa la lugha, wee kama sio mtaalam wa lugha kaa kimya, huna haja ya kuchangia. Hapa imetumika lugha ya picha na hilo jini lililotajwa humo sio jini unalolifikiria wee. Unayotaka kuyaleta ktk jukwaa hili wala hayastahili.
Jini limekuwa gumzo bara na visiwani
Jini linanyonya damu na kuweka gizani
Jini hili twalijua na tutaliweka kiganjani
Jini hili si maimuna wala shubiani
Jini lenyewe jeupe kama "Muirani"
Jini limeng'angani halisikii la muadhini
Jini halikubali linataka kutulisha majani
Jini lina kibri, kushanda mumiani
Jini limejikita uraini mpaka bungeni
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.