Ni Jini Jamani??!!!
Ni hivi, nilikuwa natoka kazini nimesimama stand ya daladala nikisubiri usafiri kwenda home, ilikuwa kama saa tatu hivi usiku as usual tulikuwa wengi stand hivyo sikuwa na wasi kabisa.
Ilipita Range Rover Sport ikasimama kwa mbele kidogo na stand na alishuka binti ambaye kiukweli sikumfahamu ila alionekana kunifahamu vyema kuanzia jina na mpaka ninapoishi. Nasema hivyo kwa sababu, aliposhuka kwenye gari alikuja direct kwangu na kulitaja jina langu sahihi na kuniambia twende nikupe lift kwa kuwa mie napita kwenu then naelekea kwangu.
Kwa respect aliyonionyesha nilishindwa kukataa ila nilimwambia nipo na rafiki yangu na akakubali twende naye.
Ila niwe mkweli Jamani! kuna wanawake wameumbwa jamani!! Huyu binti ni miongoni mwa walioumbwa vyema na Sir God!
Kwenye gari alikuwa peke yake na mimi na msela wangu huku nikiwa nimekaa siti ya mbele tukistorisha. Nilijaribu kumdodosa ye ni nani na kanijuaje, kieukweli kabisa sikupata kumfahamu na simfahamu mpaka leo.
Alinishusha kwangu na mshikaji wangu, ye akaenda zake na sijamuona tena mpaka leo.
TATIZO lilonikumba ni kwamba, karibu kila siku huyu binti namuota kila mara ndotoni na huwa hizi ndoto huja mfano wa live hivii na ni almoast 5th months sasa.
Ninavyomuota ni anakuja kwangu, hunisalimia, kunikumbatia na kunibusu kisha huondoka zake akitabasamu na ni siku moja nilimuota amekaa kwa muda mrefuu sana tukipiga story, believe or not ukiniuliza story zenyewe sikumbuki ila tulikuwa palepale kitandani kwangu.
Marafiki na jamaa zangu wananiambia ni jini mahaba kanipenda, lakini je mbona hatu`do` kama inavyosemekana kuwa jini mahaba akikupenda mna`do` mpaka unakonda na kuchoka ile mbaya??
Msaada wenu wana JF kwa anayeweza kufahamu hii situation maana nishaanza kuwa na hofu sasa na siku hizi namuota hata mchana nikisinzia na nikisema ninywe pombe ili nisimuote, huja amekasirika na kunifokea kwa nini nalewa.
Ni hivi, nilikuwa natoka kazini nimesimama stand ya daladala nikisubiri usafiri kwenda home, ilikuwa kama saa tatu hivi usiku as usual tulikuwa wengi stand hivyo sikuwa na wasi kabisa.
Ilipita Range Rover Sport ikasimama kwa mbele kidogo na stand na alishuka binti ambaye kiukweli sikumfahamu ila alionekana kunifahamu vyema kuanzia jina na mpaka ninapoishi. Nasema hivyo kwa sababu, aliposhuka kwenye gari alikuja direct kwangu na kulitaja jina langu sahihi na kuniambia twende nikupe lift kwa kuwa mie napita kwenu then naelekea kwangu.
Kwa respect aliyonionyesha nilishindwa kukataa ila nilimwambia nipo na rafiki yangu na akakubali twende naye.
Ila niwe mkweli Jamani! kuna wanawake wameumbwa jamani!! Huyu binti ni miongoni mwa walioumbwa vyema na Sir God!
Kwenye gari alikuwa peke yake na mimi na msela wangu huku nikiwa nimekaa siti ya mbele tukistorisha. Nilijaribu kumdodosa ye ni nani na kanijuaje, kieukweli kabisa sikupata kumfahamu na simfahamu mpaka leo.
Alinishusha kwangu na mshikaji wangu, ye akaenda zake na sijamuona tena mpaka leo.
TATIZO lilonikumba ni kwamba, karibu kila siku huyu binti namuota kila mara ndotoni na huwa hizi ndoto huja mfano wa live hivii na ni almoast 5th months sasa.
Ninavyomuota ni anakuja kwangu, hunisalimia, kunikumbatia na kunibusu kisha huondoka zake akitabasamu na ni siku moja nilimuota amekaa kwa muda mrefuu sana tukipiga story, believe or not ukiniuliza story zenyewe sikumbuki ila tulikuwa palepale kitandani kwangu.
Marafiki na jamaa zangu wananiambia ni jini mahaba kanipenda, lakini je mbona hatu`do` kama inavyosemekana kuwa jini mahaba akikupenda mna`do` mpaka unakonda na kuchoka ile mbaya??
Msaada wenu wana JF kwa anayeweza kufahamu hii situation maana nishaanza kuwa na hofu sasa na siku hizi namuota hata mchana nikisinzia na nikisema ninywe pombe ili nisimuote, huja amekasirika na kunifokea kwa nini nalewa.