Ambassador
JF-Expert Member
- Jun 2, 2008
- 933
- 75
Ni kawaida kwa wapenzi kuitana majina matamu matamu kama sweetie, honey, sugar, darling, etc. Mapenzi yakikolea na wapenzi kufikia hatua ya uchumba mbwembwe huongezeka. Kwa wengi wetu baada ya ndoa majina haya hubadilika kadiri muda unavyokwenda na matukio kubadili hali ya ndoa. Mfano baadhi huanza kuitana 'mme wangu' au 'mke wangu'. Wengine hutana Mr au Mrs. Baada ya kupata watoto majina ya mama fulani, sijui baba Mwamini (Lalingeni upo?) hushamiri.
Kuna rafiki yangu mmoja amegoma kabisa kuitwa jina la baba fulani na kudai kwamba yeye ana jina lake na mkewe amuite hilo. Hata yeye binafsi humuita mkewe kwa jina lake la kwanza licha ya kuwa wana watoto watatu sasa. Rafiki yangu mwingine alikuwa anaitana 'shemeji' na mkewe mpaka mtoto akawa anawaita shemeji!
Kuna madhara yoyote kumuita mkeo au mmeo kwa jina lake la kwanza mbele za watu hususan watoto wenu? Je jina lipi linafaa kumuita mmeo au mkeo naye ajifeel vizuri?
Kuna rafiki yangu mmoja amegoma kabisa kuitwa jina la baba fulani na kudai kwamba yeye ana jina lake na mkewe amuite hilo. Hata yeye binafsi humuita mkewe kwa jina lake la kwanza licha ya kuwa wana watoto watatu sasa. Rafiki yangu mwingine alikuwa anaitana 'shemeji' na mkewe mpaka mtoto akawa anawaita shemeji!
Kuna madhara yoyote kumuita mkeo au mmeo kwa jina lake la kwanza mbele za watu hususan watoto wenu? Je jina lipi linafaa kumuita mmeo au mkeo naye ajifeel vizuri?