Mbona hata yule mgombea wa jimbo la kigamboni ana uraia wa S. Africa lakini amepitishwa na chama? Alikimbia nchini baada ya kutumikia kifungo kwa muda, kisha akaona akakae mafichoni huko Kusini mwa africa, ila CCM wakimtaka mtu, ndiyo atakuwa, Bashe yeye mwenyewe anafahamu nini kina msibu, ajaribu kupambana kivyengine, c kupitia chaguzi za chama chake
Hapa umesema uongo wa waziwazi. Huyo mgombea wa CCM Kigamboni namfahamu binafsi, anaitwa Faustine Ndugulile, daktari bingwa. Huyu namfahamu sana na ndiye mgombea pekee huko CCM ninayemfahamu kiasi hicho kutokana na kufahamiana sana na mdogo wake na kuzoea nyumbani kwao tangu mdogo. Huyu ni mtanzania, mnyamwezi wa Tabora. Familia yao waliwahi kuishi Zimbabwe zamani ambako wazazi wake walifanya kazi. Hajawahi kutumikia kifungo chochote, uongo mtupu huu. Tena aliwahi kuwa mkurugenzi wa masuala ya udaktari wizara ya afya makao makuu, na mke wake ni profesa pale Muhimbili. Huko South Africa alikwenda kufanya kazi ya UN na wala hajatimka kama unavyodai. Usipende kukurupukia usiyoyajua.
Mimi siipendi CCM hata kidogo na wala sitaipigia kura, lakini siwezi kuvumilia mtu anapomtungia uongo hivi jamaa ninayemfahamu, haifai hata kidogo.