JIJI/MUNICIPAL/ Prof. Ana Tibaijuka Kuna Ruhusa Kufuga MAKAZI YA WATU

mgt software

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
13,767
7,115
Ni swali ambalo huwa najiuliza ni nani anayewajibika kukataza au kuruhusu mifugo kwenye Makazi ya watu, nikiwa mkazi wa eneo ambalo limetengwa na Serikali kwa ajili ya makazi ya watu, kumekuwepo na ukiukwaji wa Mipango miji, ikiwa ni pamoja na kuweka mifugo sehemu za makazi, utitili wa Maduka kwenye kuta za nyumba zao, ubadilishwaji matumizi ya Ardhi kufuatana na maombi ya ardhi. haya yanaendelea kutokea kwenye VIWANJA Vingi vya BUNJU BEACH Kwa MKANADA, baadhi wameleta mifugo kwenye viwanja vyao, mifugo hiyo inasababisha hasara zifuatazo:
1. Mmomonyoko wa Barabara kwani ni za bararbara za Vumbi.
2. Wakiachiwa wanakula Mimea ya watu kama Miti, maua na kuaribu kuta na mazingila kwa kuacha vinyesi ovyo.
3. Wanyama hawa wanapokuwa hawajapatiwa chakula usiku huwezi pata usingizi kwa kuwa wanapiga kelele sana ukizngatia chakula chao ni cha kutafutwa, hawana malisho, wananyama hao , ni nguruwe, Mbuzi Ngombe na Kondooo.
4. Kwa kuwa hawa wanyama hukojoa hovyo na niwachafu sana wanaweza kuleta magonjwa kama ifuatavyo-
maralia kwa sababu ya maji maji na unyevunyevu kuna mazalia yambu, Kipindu pindu kwa kuwa ni vinala wa kuleta INZI .
5. Wanaweza kusababisha uvunjifu wa Amani kwa kuwa wanaowafuga wanaona wana haki ya kufanya hivyo, wakati ambao hawafungi wanaona kero hivyo kuan mifarakano mingi sana mpaka majirani hawaongei kufuatana na wafugaji kuwa wakali wanapoambiwa au kudai haki ya uaribibu.

Mwisho naomba Mamlaka husika /Jiji/ ardhi waje bunju watuondolee mifugo ilik kukomesha tabia ya kuaribu Mazingira kwa makusudi na kusababisha uvunjivu wa amani
 
kwa bongo hii kijana hayo ni magumu kutekelezeka kabisa ninapoishi pia ni maeneo ya wafugaji nimepata kero sana nimepigizana kelele na jirani yangu nimechoka ukienda serikali ya mtaa wanaitisha kikao anapewa onyo ila onyo anapewa mwenye mifugo sio mifugo so tatizo linarudi pale pale kwani ngombe na mbuzi wakifunguliwa wanajua jalala langu lilipo wanakimbilia mbwa wake na wengine ivyo ivyo wametifuatifua mpaka kero nilipooona yanazidi nashukuru nimeweka fensi na geti sasa raha mstarehe ata paka aingii kwangu mana nimeweka mbwa yani ata akiwa juu ya ukuta mbwa wangu ataki ni ugomvi mpaka aondoke so kwa mtaji huu nakushauri utatue tatizomwenyewe kama mimi mkuu ukifatilia wanakwambia kwa mjini kuna idadi maalumu ya mifugo lakini wapi nafikiri serikali ingeweka sheria mtu kama anataka kufuga bac walishe sio waachie kutafuta malisho
 
Mama tiba sijui hata ameishia wapi manake ule mkwala aloingia nao nilidhani viwanja wazi vilivyovamiwa vingesharudishwa!
 
Kwa kweli swala la mifugo katika makazi inahuzunisha sana.... Jirani zangu wote wawili wanafuga Kuku wa Kisasa.... imagine walivyo na kelele, wanatoa harufu isiyofaa... yaani ni kero... Sema tu saa ingine unapotezea... Ila kweli serikali ingezingatia hili suala
 
Hivi Madaktali wa Mifugo wanasemaje, kuna Mifugo mingi haipatiwi madawa, chanjo na watu wanajifugia tu akuna uangalizi, je kukitokea mlipuko wa magonjwa nani wa kulaumiwa, je watu wa mazingira mpo wapi?, je kazi za watu wa mazingira ni kupigia kelele wenye viwanda na maotel tu au kujali afya za watu. Afya za watu ni pamoja na kuishi kwa Raha na Amani, unapotoka Kazini unakuja kupumzika sio kukutana na kero kazi zilivyohainisha, je utawala wa sheria ni upi kama wewe kila siku unagombana na jirani yako bila serikali kuwapa suruhu ya kudumu kw akutoa ONYO mbali mbali kuhusu Mifugo kwenye Makazi ya watu. Ifike hatua sasa tusiwe na uovyo, tufuatilie na tuzingatie usafi kwanza, kwa uozo huu wa serikali ndio Maana yanatokea haya ya Mwananyala, maana yanatokana na Mazoea yasiyozingatia uwajibikaji katika kazi ulioiomba .
 
Kwa kweli swala la mifugo katika makazi inahuzunisha sana.... Jirani zangu wote wawili wanafuga Kuku wa Kisasa.... imagine walivyo na kelele, wanatoa harufu isiyofaa... yaani ni kero... Sema tu saa ingine unapotezea... Ila kweli serikali ingezingatia hili suala

binamu we acha tu sizani kama unakaa maeneo kama ya kwetu uku kitunda na kipunguni utakoma kuringa mana ni mifugo kwa kwenda mbele ukamwambie mkurya mifugo yako inanikera yani cpati picha hyo vita itatulizwa na jeshi gani
 
Hivi Madaktali wa Mifugo wanasemaje, kuna Mifugo mingi haipatiwi madawa, chanjo na watu wanajifugia tu akuna uangalizi, je kukitokea mlipuko wa magonjwa nani wa kulaumiwa, je watu wa mazingira mpo wapi?, je kazi za watu wa mazingira ni kupigia kelele wenye viwanda na maotel tu au kujali afya za watu. Afya za watu ni pamoja na kuishi kwa Raha na Amani, unapotoka Kazini unakuja kupumzika sio kukutana na kero kazi zilivyohainisha, je utawala wa sheria ni upi kama wewe kila siku unagombana na jirani yako bila serikali kuwapa suruhu ya kudumu kw akutoa ONYO mbali mbali kuhusu Mifugo kwenye Makazi ya watu. Ifike hatua sasa tusiwe na uovyo, tufuatilie na tuzingatie usafi kwanza, kwa uozo huu wa serikali ndio Maana yanatokea haya ya Mwananyala, maana yanatokana na Mazoea yasiyozingatia uwajibikaji katika kazi ulioiomba .

kazi za mabwana afya ni kwenda kuonja vyakula mahotelini tena hoteli za maana kama vimeivya ukiwaona wanavitambi kwa kula vyakula vya bure yani haya ya mbwa ni kero maeneo mengi ila mm nitasemea eneo ninaloishi utakuta mtu ana mbwa 5-6 awafungwi na fensi ni barabarani mda wote mbwa wanaranda mara wamelala barabarani na ukipita akupishi labda uwe na gari usiku ikifika saa 3 ucku unaanza kufikiria pale nitapitaje awana matunzo wanajitafutia chakula wenyewe sio nyumba moja karibia kila nyumba ina mbwa du cjui tutafikaje kwa mfumo huu mfano kabla cjaweka fensi sikufuga mbwa maana sikutaka mbwa wangu awe kero kwa majirani nilipomaliza nilitafuta mbwa sio bora mbwa bali mbwa bora na nilipata kupitia hapa JF
 
Ni swali ambalo huwa najiuliza ni nani anayewajibika kukataza au kuruhusu mifugo kwenye Makazi ya watu, nikiwa mkazi wa eneo ambalo limetengwa na Serikali kwa ajili ya makazi ya watu, kumekuwepo na ukiukwaji wa Mipango miji, ikiwa ni pamoja na kuweka mifugo sehemu za makazi, utitili wa Maduka kwenye kuta za nyumba zao, ubadilishwaji matumizi ya Ardhi kufuatana na maombi ya ardhi. haya yanaendelea kutokea kwenye VIWANJA Vingi vya BUNJU BEACH Kwa MKANADA, baadhi wameleta mifugo kwenye viwanja vyao, mifugo hiyo inasababisha hasara zifuatazo:
1. Mmomonyoko wa Barabara kwani ni za bararbara za Vumbi.
2. Wakiachiwa wanakula Mimea ya watu kama Miti, maua na kuaribu kuta na mazingila kwa kuacha vinyesi ovyo.
3. Wanyama hawa wanapokuwa hawajapatiwa chakula usiku huwezi pata usingizi kwa kuwa wanapiga kelele sana ukizngatia chakula chao ni cha kutafutwa, hawana malisho, wananyama hao , ni nguruwe, Mbuzi Ngombe na Kondooo.
4. Kwa kuwa hawa wanyama hukojoa hovyo na niwachafu sana wanaweza kuleta magonjwa kama ifuatavyo-
maralia kwa sababu ya maji maji na unyevunyevu kuna mazalia yambu, Kipindu pindu kwa kuwa ni vinala wa kuleta INZI .
5. Wanaweza kusababisha uvunjifu wa Amani kwa kuwa wanaowafuga wanaona wana haki ya kufanya hivyo, wakati ambao hawafungi wanaona kero hivyo kuan mifarakano mingi sana mpaka majirani hawaongei kufuatana na wafugaji kuwa wakali wanapoambiwa au kudai haki ya uaribibu.

Mwisho naomba Mamlaka husika /Jiji/ ardhi waje bunju watuondolee mifugo ilik kukomesha tabia ya kuaribu Mazingira kwa makusudi na kusababisha uvunjivu wa amani

nioneshe eneo lililotengwa kwa ajiri ya kufugia mifugo.
 
binamu we acha tu sizani kama unakaa maeneo kama ya kwetu uku kitunda na kipunguni utakoma kuringa mana ni mifugo kwa kwenda mbele ukamwambie mkurya mifugo yako inanikera yani cpati picha hyo vita itatulizwa na jeshi gani

Bahati mbaya ni kuwa wengine wanauchukua 'ukijiji' na wanakuja nao mjini. Angalia Mbezi beach kulivyo na majumba makubwa na mazuri na bado mabanda ya ng'ombe na mbuzi hayakosekani. Tena kuna wengine ni wasomi wazuri tu lakini kuweka mifugo nyumbani ni lazima.

Basi hao mapanya ukiwa na jirani mwenye mifugo! Hata ukijaribu kucontrol haiwezekani.

Afadhali hata Mzee Mengi aliwasema na kuwaaibisha Maprofesa wa Chuo Kikuu na hivi sasa ndiyo kidogo hicho Chuo kimerudi katika hadhi yake. Mwanzo wa miaka ya tisini ulikuwa unapishana na makundi ya mifugo pale Chuoni.
 
Bahati mbaya ni kuwa wengine wanauchukua 'ukijiji' na wanakuja nao mjini. Angalia Mbezi beach kulivyo na majumba makubwa na mazuri na bado mabanda ya ng'ombe na mbuzi hayakosekani. Tena kuna wengine ni wasomi wazuri tu lakini kuweka mifugo nyumbani ni lazima.

Basi hao mapanya ukiwa na jirani mwenye mifugo! Hata ukijaribu kucontrol haiwezekani.

Afadhali hata Mzee Mengi aliwasema na kuwaaibisha Maprofesa wa Chuo Kikuu na hivi sasa ndiyo kidogo hicho Chuo kimerudi katika hadhi yake. Mwanzo wa miaka ya tisini ulikuwa unapishana na makungi ya mifugo pale Chuoni.

mkuu hapo kwenye red umeongea yani majirani zangu wapo dar lakini wamebeba musoma sio akilini tu bali phiscaly kabisa mkuu mpaka kero
 
mkuu hapo kwenye red umeongea yani majirani zangu wapo dar lakini wamebeba musoma sio akilini tu bali phiscaly kabisa mkuu mpaka kero

Wengine ni wafitini tu... imagine mtu kaunganisha banda lake na ukuta wako.... upepo unakotokea ndo anatega banda pale... kisha manyoya anachomea pale pale.... kinyesi cha kuku anatupia hapo kwenye ukuta.... jamani... sometimes unaimba tu Mungu akupe busara za ziada
 
Back
Top Bottom