Jihadhari na Utapeli wa Photo Point ya Mlimani City

Idimi

JF-Expert Member
Mar 18, 2007
14,970
10,462
Ndugu wana JF,
Sio lengo langu kuvurga biashara ya upigaji na usafishaji picha wa hawa ndugu wa Photo Point ya pale Mlimani City. Lengo tu ni kuwatahadharisha ndugu mnaoenda kupiga picha za matukio mbalimbali pale mahali (kama za Sendoff, Ubarikio, Harusi, birthdays na graduation). Kimsingi huduma hizi zinalipiwa bei kubwa na huambatana na ahadi za zawadi kemkem kama vile kuchapishiwa picha zako katika foronya, mito, vikombe, bakuli, sahani, fulana n.k.
Mnamo tarehe 10 ya mwezi Julai nilienda kupiga picha pale ofisini kwao Mlimani City. Gharama ya picha zile ilikuwa shilini 96,000, ikiwa ni kupiga na kusafisha picha 20 za ukubwa wa 5'x7' na moja ya ukubwa wa 12'x16' ambazo zingewekwa katika albamu pamoja na kuchapishiwa sahani moja yenye picha ya tukio.
Mpaka ninavyoongea hivi sasa albamu wanasema hawana, sahani na vikombe hawana, zimeisha, ilhali vimeshalipiwa katika package zao tulizolipia. Nikiwa katika harakati za kufuatilia picha zangu jana nikakutana na kundi la wateja wengine wenye malalamiko kama yangu wakidai kurejeshewa sehemu ya fedha zao walizolipia huduma.
Mpaka sasa sijajua mustakabali wa albamu na vitu vingine, kwa hiyo ndugu zangu mnaoenda kupiga picha pale Photo Point Mlimani City muwe makini na utapeli huu.
 
Mliandikishiana au ndio mali kauli,kama mliandikishiana au kama kuna sehemu pameandikwa ukipiga picha kadhaa wa kadhaa utapata vitu fulani basi mnahaki ya kudai hivyo vitu mlivyoahidiwa lakini kama hakuna kitu kama hicho basi hiyo imekula kwenu,na hapo ndio ujue biashara za washwahili zinavyoendeshwa kiswahili
 
Msiogope haijakula kwenu...nahisi jamaa wameishiwa stock tu! Fuatilieni na mtapata haki zenu. Tatizo jamaa walikuwa na uchu wa kukusanya fedhwa bila kuhakikisha kama huduma na bidhaa zao zinaendana na boom hiyo. Polen wandugu.

Kwa upande mwingine, Photo point ya Mlimani City ni moja kati ya sehemu wanapopiga picha za passport size kwa bei nafuu kuliko sehemu nyingine yeyote Dar. Picha nane za kiwango kizuri unapata kwa buku tatu tu. Bravo them!!
 
Hivi Tz hakuna wataalamu zaidi ya hao jamaa?. Zamani zile kupiga picha ilikuwa kama unakaa mkoani ni mpaka usubiri miezi mitatu au minne kupata picha zako. Leo hii kwa teknolojia ilivyo, unapost pics zako kwa wasafishaji, unachagua huduma uitakayo..na muda mfupi unapata kila kitu...ukiritimba huu wa kuwa wafanyabiashara ndio unaoleta shida..poleni sana.
 
Labda kama mashine yao imeharibika, lakini sahani nyingi zisokuwa na mauwa zinakubali picha ikiwa unavyo vifaa muafaka.
 
Ndugu Idimi,

Nadhani umetoa changamoto. Ila neno UTAPELI umeitumia visivyo. Tapeli ni yule anayekuzungusha bila SABABAU ya kueleweka. Makampuni makubwa tu mfano SIGARA kuna wakati Sigara ya Embassy ilikua haipo mtaani sembuse hao wajisiriamali wa Kizalendo???

Wa Tanzania tumezoea mpaka tuone WAGENI wana wekeza ndo tuone SAFI ila akiwekeza MZALENDO basi tatizo DOGO tu utaambiwa TAPELI, ANANYANYASA WAFANYAKAZI, HALIPI KODI n.k.

Wakati nakubaliana na wewe kuhusu kuishiwa na vifaaa (LABDA) na kutokupa taarifa mapema nadhani umefanya vizuri kuweka wazi ila KICHWA cha habari/taarifa ingekuwa kingine na sio UTAPELI.

Ila safi sana, wewe ni mteja mzuri..

Wako FP
 
Kuna uzembe pale. Mimi sikuchagua kuwekewa "border" kwenye picha zangu, lakini jamaa wakaniwekea. By default, picha inatakiwa isiwe na border unless umecheck alama ya vema ( √ ) kwenye sehemu ya border katika bahasha zao. Siku nyingine nililipia kusafisha picha kwa size ya 4x6 na ikaandikwa katika bahasha, nikatoka kidogo, niliporudi nikakuta zimesafishiwa kwa size ya 3x5, halafu eti wakasema tunaomba tugawane hasara!
 
na wewe una roho nyepesi kama kamasi, mlikubaliana biashara/service..........huenda jamaa kaharibikiwa mitambo au vifaa vimeisha......subiri daaaaaaaah
 
Yeah give them the benefit of the doubt! Mie ni mteja wa hiyo kampuni since wakiwa nachumba kimoja kule Mayfair; nyingi ya kumbukumbu za matukio ya maisha yangu Photo point wamenisidia kuyaweka ikiwa hata la ujio wa Junior! Issues zipo na si kitu cha kudumu.
Ila pia ni angalizo zuri kwa Photo point msituudhi wateja wenu kama hivi...............mwombeni radhi huyu jamaa!
 
haahhaaahaaha eti Vikombe saani vimeisha. Kumbe kuna vikombe na sahani spesho kwa ajili ya kazi kama hii. Nilidhaniunaweza kuweka picha kwenye kikombe au sahani yeyote.

Inawezekana kuna baadhi ya vifaa vyao vimeharibika na hawasemi ukweli wa tatizo halisi linalowakabili.
 
Neema Apson vipi tena photo point yako inachemka? labda wafanyakazi wako wanakuchezea hapo kukuharibia biashara.
Jamani kuna ingine ya Mayfair, Mikocheni mie niliwafurahia huduma zao ila ni picha tu na kusikilizwa kupata nilichotakaga
 
Pole sana ndugu lakini Jaribu kuuliza vizuri huenda wakakupa sababu maalum za ucheleweshwaji huo.Mimi sijawahi kuwatumia hao jamaa lakini nahadithiwa na watu kuwa Jamaa kazi zao ni nzuri so usikimbilie kuwaita matapeli tu huenda wana sababu iliyo nje ya uwezo wao Ingawaje Watanzania nao sometimes hawako wazi inawezekana wameishiwa bidhaa kwenye stock lakini haweki vitu wazi na badala yake wanakupa tarehe tu bila kukwambia nini hasa kinaendelea.
 
Hobi nyingine bana
Hivi mpaka leo mnapiga picha ili iweje. Nafuatilia matumizi ya picha hizo naona ni kupoteza kabisa pesa. Sawa! hata kuvuta sigara ndo ivo ivo
Ila poleni, mngeanza hayo mambo zamani msingefanya leo
 
ndugu wana jf,
sio lengo langu kuvurga biashara ya upigaji na usafishaji picha wa hawa ndugu wa photo point ya pale mlimani city. Lengo tu ni kuwatahadharisha ndugu mnaoenda kupiga picha za matukio mbalimbali pale mahali (kama za sendoff, ubarikio, harusi, birthdays na graduation). Kimsingi huduma hizi zinalipiwa bei kubwa na huambatana na ahadi za zawadi kemkem kama vile kuchapishiwa picha zako katika foronya, mito, vikombe, bakuli, sahani, fulana n.k.
Mnamo tarehe 10 ya mwezi julai nilienda kupiga picha pale ofisini kwao mlimani city. Gharama ya picha zile ilikuwa shilini 96,000, ikiwa ni kupiga na kusafisha picha 20 za ukubwa wa 5'x7' na moja ya ukubwa wa 12'x16' ambazo zingewekwa katika albamu pamoja na kuchapishiwa sahani moja yenye picha ya tukio.
Mpaka ninavyoongea hivi sasa albamu wanasema hawana, sahani na vikombe hawana, zimeisha, ilhali vimeshalipiwa katika package zao tulizolipia. Nikiwa katika harakati za kufuatilia picha zangu jana nikakutana na kundi la wateja wengine wenye malalamiko kama yangu wakidai kurejeshewa sehemu ya fedha zao walizolipia huduma.
Mpaka sasa sijajua mustakabali wa albamu na vitu vingine, kwa hiyo ndugu zangu mnaoenda kupiga picha pale photo point mlimani city muwe makini na utapeli huu.

ndugu nikusaidiesasa wahuni kama hao nenda nunua kitu angalia wameshachukua machine ya tra....fn..kama sio anzia nao huko huku ukidai madai yako...unajua nasikitika akuna kesi ya nyani kama ya madai nchii hii..ukiwapeleka mahakamani wanaishia kusema awana na watakulipa lini wanataja muda wanaotaka...hiyo ndio upupu wa nchi yetu else wapelekee comedy hao simple wakitoka kwenye tv walahi na kwambia wanakupigia wenyewepole mpwa
 
Endelea kumpa pole mama yetu mwambie ndio mwanzo wa ndoa hiyo ndoa si kufurahi tu hata majaribu ni moja na nafasi za ndoa ..polen wapendwa
 
neema apson vipi tena photo point yako inachemka? Labda wafanyakazi wako wanakuchezea hapo kukuharibia biashara.
Jamani kuna ingine ya mayfair, mikocheni mie niliwafurahia huduma zao ila ni picha tu na kusikilizwa kupata nilichotakaga

mmmhhh apson wale wale ama???
 
Back
Top Bottom