Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Jifunze namna ya kuwavumilia wengine!
Ukianza kutazama tabia na matendo ya watu ambao unakutana nao kwenye maisha yako ya kila siku kwa kujiuliza kile unachojifunza kutoka kwao utajikuta unaanza kuyatazama kwa jicho tofauti yale uliyokuwa ukiyaona hapo kabla kama maudhi au yenye kukatisha tamaa. Utaanza kuhisi ukipungukiwa na kiwango cha kukerwa, kuchanganywa na kubughudhiwa na vitendo na mapungufu ya wengine.
Kama tutawatazama wengine na matendo yao kama waalimu wetu tutajikuta tukiondoa hali fulani ya chuki na kukerwa ambayo huwa tunakuwa nayo pale mtu au watu wengine wanapofanya kinyume na matarajio yetu.
Muuguzi anapotutukana au anapotukaripia, badala ya kukasirika inabidi tujiulize tunachojifunza. Huenda tunajifunza kwamba ni hatari kwa mtu kuchagua kufanya kazi asiyoipenda.
Lakini pia huenda tunajifunza huruma, kuwahurumia wengine ambao wanafanya kazi ambazo siyo uchaguzi wao bali kwa sababu ya shida.
Basi linapo haribikia njiani, badala ya kukasirika inabidi tujiulize tunachojifunza. Huenda tunajifunza kuwa ni vizuri kuwa waangalifu tunapoamua kuchukua jukumu fulani kubwa maishani, au huenda tunajifunza kwamba tunaweza kujiandaa na kujiamini lakini mambo yakabadilika bila kutegemea au tunaweza kujifunza kwamba hakuna kitu kisichoweza kwenda kombo hata kama tukiamini kwa kiasi gani.
Mfanyabiashara tapeli anapotuuzia mali mbovu au zisizo zenyewe hatuna haja ya kukata tamaa na kuchanganyikiwa badala yake inabidi tujiulize tunachojifunza kutoka kwake. Huenda tumejifunza hatari ya mtu kujali fedha au maslahi yake zaidi kuliko kujali maisha na matarajio ya wengine. Huenda pia tumejifunza jinsi inavyouma pale tunapowadhulumu wengine.
Inapobidi kusimama kwenye foleni muda mrefu kusubiri huduma fulani, hatuna haja ya kukasirika na kuanza kujilauamu na kuwalaumu wengine. Badala yake inabidi tujiulize kile tunachojifunza katika tukio hilo. Huenda tunajifunza kuwa na subira maishani. Mara nyingi kusimama foleni ni kipimo kizuri sana cha kiwango cha subira aliyonayo mtu.Hii ni nafasi muhimu kwetu kujifunza subira na uvumilivu badala ya kukasirika na kukata tamaa.
Inawezekana wewe unayesoma hapa unaweza kuliona jambo hili kama kichekesho au lisilowezekana. Lakini ukweli ni kwamba sio kazi ngumu kuwavumilia wengine.
Ukianza kutazama tabia na matendo ya watu ambao unakutana nao kwenye maisha yako ya kila siku kwa kujiuliza kile unachojifunza kutoka kwao utajikuta unaanza kuyatazama kwa jicho tofauti yale uliyokuwa ukiyaona hapo kabla kama maudhi au yenye kukatisha tamaa. Utaanza kuhisi ukipungukiwa na kiwango cha kukerwa, kuchanganywa na kubughudhiwa na vitendo na mapungufu ya wengine.
Kama tutawatazama wengine na matendo yao kama waalimu wetu tutajikuta tukiondoa hali fulani ya chuki na kukerwa ambayo huwa tunakuwa nayo pale mtu au watu wengine wanapofanya kinyume na matarajio yetu.
Muuguzi anapotutukana au anapotukaripia, badala ya kukasirika inabidi tujiulize tunachojifunza. Huenda tunajifunza kwamba ni hatari kwa mtu kuchagua kufanya kazi asiyoipenda.
Lakini pia huenda tunajifunza huruma, kuwahurumia wengine ambao wanafanya kazi ambazo siyo uchaguzi wao bali kwa sababu ya shida.
Basi linapo haribikia njiani, badala ya kukasirika inabidi tujiulize tunachojifunza. Huenda tunajifunza kuwa ni vizuri kuwa waangalifu tunapoamua kuchukua jukumu fulani kubwa maishani, au huenda tunajifunza kwamba tunaweza kujiandaa na kujiamini lakini mambo yakabadilika bila kutegemea au tunaweza kujifunza kwamba hakuna kitu kisichoweza kwenda kombo hata kama tukiamini kwa kiasi gani.
Mfanyabiashara tapeli anapotuuzia mali mbovu au zisizo zenyewe hatuna haja ya kukata tamaa na kuchanganyikiwa badala yake inabidi tujiulize tunachojifunza kutoka kwake. Huenda tumejifunza hatari ya mtu kujali fedha au maslahi yake zaidi kuliko kujali maisha na matarajio ya wengine. Huenda pia tumejifunza jinsi inavyouma pale tunapowadhulumu wengine.
Inapobidi kusimama kwenye foleni muda mrefu kusubiri huduma fulani, hatuna haja ya kukasirika na kuanza kujilauamu na kuwalaumu wengine. Badala yake inabidi tujiulize kile tunachojifunza katika tukio hilo. Huenda tunajifunza kuwa na subira maishani. Mara nyingi kusimama foleni ni kipimo kizuri sana cha kiwango cha subira aliyonayo mtu.Hii ni nafasi muhimu kwetu kujifunza subira na uvumilivu badala ya kukasirika na kukata tamaa.
Inawezekana wewe unayesoma hapa unaweza kuliona jambo hili kama kichekesho au lisilowezekana. Lakini ukweli ni kwamba sio kazi ngumu kuwavumilia wengine.