Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Wakati tunaendelea kutanua tafakari zetu kwa ukatili aliofanyiwa ndugu yetu. Macho yetu mawili tuyaelekeze kwa serikali huku tukiangalia mbele lakini kuna haja ya kuweka jicho la ziada kisogoni mwetu hata kama la bandia kwa ajili ya kutizama pande nyingine ambazo tunazisahau sana. Kwa mfano, siku hizi kuna makampuni ya ulinzi binafsi ambayo nayo hutumia silaha kama watumiavyo polisi. Tena huzibeba bila ya uficho, hawa nao wanaweza kukodiwa na kutumiwa kufanya tukio kama lililotokea. Ni vyema kwa nia njema ikiwa kweli tunamsaka adui huyu, ni budi tuweke eneo pana katika kutafuta njia ya kutufikisha walipo wauaji pasi na shaka.