KIBURUDISHO
JF-Expert Member
- Mar 28, 2011
- 1,002
- 274
WanaJF wenzangu mambo vp? natumai mu wazima.Kama mnakumbuka vizuri kwa siku kama tatu zilizopita niliwasilisha hapa mjengoni juu ya suala zima la upatikanaji wa chaneli zote za hapa tanzania kwa njia ya satelite zinavyosumbua.Hivyo leo nikalazimika kuwasiliana na wahusika wa IPP MEDIA idara ya ufundi moja kwa moja na ndipo wakanipatia jibu kuwa;Kwa woote wanaopokea matangazo yao kwa njia ya satelite ya INTELSAT906E kwa kutumia madish ya C-BAND ya ukubwa wa ft sita hawataweza kupokea matangazo yao hivyo wenye uwezo wa kupata matangazo yao ni wale tu wenye madish yenye ukubwa wa ft8 na inatokana na mkataba waliowekeana na hao wenye hiyo satelite kuwa mawimbi yao yanatakiwa yapatikane kwenye dish za ft8 tu wanasema hapo awali walikuwa wanafanya wizi tuu wa kupandisha signal na ndio maana sisi wenye madish ya ft6 tulikuwa tunawapata kwa hiyo kwa sasa hivi haiwezekani kwa sababu wao wenyewe wenye satelite ndio wanawacontrol.Sasa kilio changu ni kwa wale wenzangu na mimi ambao karibia woote nchi nzima tunatumia madish ya ft8,na kwa nini walifikia muafaka wa kuingia mkataba kama huo hali wakijua kipato cha watanzania walio wengi ni cha chini na hii sasa sii kwa IPP MEDIA tu ni kwa chaneli zote za bongo,Nawasilisha.