Recta
JF-Expert Member
- Dec 8, 2006
- 855
- 38
Nimemsikiliza huyo mtangazaji wa ITV aitwaye Gamba. Nadhani ana tatizo la upeo. Huyu, kama walivyo watangazaji wengi hapa nchini, wana upeo mdogo sana. Unahoji vipi suala la ahadi ya elimu bure wakati Chadema wamelifafanua hilo vizuri sana. Inaelekea huyu ana matatizo 'upstairs".
Nadhani anashindwa kuelewa kuwa, hakuna kitu kisichowezekana hasa nia ikiwepo. Kenya ambao hawana rasilimali nyingi kama Tanzania, wameweza kutoa subsidized education schemes. Sisi wengi wetu tulisoma bure hadi elimu ya juu. Inawezekanaje leo, ambapo wazazi wengi wanaweza kupeleka watoto wao shule za binafsi, serikali ishindwe kusomesha bure wote waliobaki? Hii ni kejeli kubwa sana kwa maendeleo ya nchi. Kama hii ya elimu bure kwa watoto haiwezekani, basi hakuna linalowezekana hata moja.
Kuna wanaouliza eti pesa zitatoka wapi. Swali gani hili? Pesa za magari, furniture za nyumba na ofisi za serikali, vitafunio na vitafunwa, safari zisizo na tija, marupurupu ya semina, warsha, kongamano na mikutano isiyo na tija zinatoka wapi? Mbona hizo ni rahisi kuzipata kuliko za kusomesha watoto wa Tanzania? Je, pesa za migodi, uwindaji, utalii, uvuvi, kilimo, kodi mbalimbali na nyinginezo (japokuwa kodi tu hawawezi kuikusanya zaidi ya 30%) zinakwenda wapi? Tuache kutaniana kwenye mambo serious. Gamba anajiunga na team ya wanaotia aibu. Kama hajui jinsi pesa itakaosemesha watoto wa Tanzania itatoka wapi, anabidi arudi shule upya.