binti ashura
Senior Member
- Jan 14, 2011
- 118
- 19
Ndugu zangu wana jf mpo juu, nashindwa kuwapa sifa ile itakayo watosha kwa kazi nzuri mnayoifanya. najuwa tumekuwa tukiandika lisala kuwa ndugu mgeni lasmi popote penye mafanikio hapakosi kuwa na matatizo, hivyo hata Jf haiwezi kosa matatizo kama vile watu kuleta habari za Udaku kwenye siasa au habari hii katika sehemu isiyohusika, pamoja na yote hayo watu wamekuwa wakielimishwa siku hadi siku. jambo lililonisukuma mie kuwamwagia sifa ni kwamba mie nilikuwa kijijini sana ambako magazeti na taarifa mbalimbali huwa zinachelewa sana lakini nimekuwa nikizipata kwa JF!. Jamani, wahenga wanasema mnyonge, mnyongeni lakini haki yake mpeni!. nawamwagia sifa JF!