JF Freestyle battle special thread

Thanks man wherever ur usinisahau mimi,
yeyote utakayekutana naye usisahau upo ukimwi,
Soma sana mwana usijali ugumu wa skim,
If am not reachabo napatikana www. yetu jamii,
Sala zidisha na tuombeane mazuri kwa imani.
In God willing tuonane kesho morning
Ushauri mwanana
Marefu kwa mapana
Hakika Nguli umenena
Mabaya niyaogope kama kinena
Machungu nisilete kwa tunayependana
Akili na uwezo tumepewa naye Maulana
Tukizitumia kwa hakika hatutobezana
Heshima ikiwepo matamu tutashirikishana
 
Vua gamba,
Ni kwamba unatamba? Kwa mashairi ya za viatu kamba?
Yasiyofika liyamba yasowekeka sambamba
Ni ubahili au huna staili?
Au huwezi kwenda na vibweka vyangu vilivyojaa kwa paili za maili?
Ustake nlete gharika, utaghafirika
Nakupa kipigo fika katika lugha ya mwafrika
We nenda kaibie, wakakusaidie
Kipigo pale pale mpaka wende ujifie
Jaribu kuleta vina vyenye usawia na uzito
Si mizani hafifu ya medani za kibitoz
Ntakukoa vikonzi, kwa vina vingi kama dozi za ponzi
Mpaka ulielie kama JD na machozi
Hatutaki gozigozi, nenda karudi kozi
Ustake kututisha kwa yako feki mapozi

Nilijua uko dhaifu kama my wife wa mtu flani
Hii gemu ya watu wazima umeifakamia kichwakichwa
Sasa ngoja uchinjwe kama kuku wa kitoweo
Usije kujilizaliza kama Pinda alivyolia

Ngebe na kelele nyingi sijui unadhani tunacheza ma-ready?
Unaleta pumba kama mpunga sijui ndio kuchanganyikiwa
Sasa kaa chonjo ili ukobolewe kama unga we sembe
Dogo maneno mengi wakati mbata na bong'oa nimekupiga
Mbele yangu huna neno ni bora ujiite Bubu ataka kusema
 
Jamii forums
Ni web tam
Kwa wenye akili timam
pia kwa dingi aunt hata binam
Lakini si kwa wanaharam

Weweeeeeeeee
Subirini nikalewe then nikirudi mtanitambua.
 
Jamii forums
Ni web tam
Kwa wenye akili timam
pia kwa dingi aunt hata binam
Lakini si kwa wanaharam

Weweeeeeeeee
Subirini nikalewe then nikirudi mtanitambua.

ohohooooooooo gang chomba
thats not they way we freestyle
c'mon man show me the real emirates spirit
where we really see you flowing
with lots of gang wannabee flows

reading at you name
thought you were the real gang'
but with such direct shot!
Da'aaamn man i see no place
for you to the end!!

Nothing but love bro'
 
Nilijua uko dhaifu kama my wife wa mtu flani
Hii gemu ya watu wazima umeifakamia kichwakichwa
Sasa ngoja uchinjwe kama kuku wa kitoweo
Usije kujilizaliza kama Pinda alivyolia

Ngebe na kelele nyingi sijui unadhani tunacheza ma-ready?
Unaleta pumba kama mpunga sijui ndio kuchanganyikiwa
Sasa kaa chonjo ili ukobolewe kama unga we sembe
Dogo maneno mengi wakati mbata na bong'oa nimekupiga
Mbele yangu huna neno ni bora ujiite Bubu ataka kusema

Unaogopa?
Wanavita Umsolopagaaz Makumazan na Umbopa!
Mashairi unakopa, unga unga bopa bopa?
Umechoka? huna cha kunena unafoka?
Unajiona umetoka kumbe bado umepotoka
Hujui unapokwenda wala kule unapotoka
Spidi ya Gulfstream huipati kwayo Foka
Usilete Mahoka, galasha jokeri joka
Nguvu za Coca, pangusa vyako vimoka
Huliwezi soka, uwanjani toka
Twache makocha tuchane vocha
We ndondocha dondoka mdondo
Ka mnywa gongo mbogo, aliyeshindia kipande cha muhogo
Kama Kublai Khan, ngomeyo naihusuru
Bila msululu wa suluhu kamwe siinusuru
Hii nyukilia, ila siyo kwa asali
Usiposikia utakutana na ajali
Chernobyl au Bhopal, rungu lake Umbopa
We acha kuropoka,
Bila vina wala mizani
Unachina kizani
Wewe dinner dizaini
Wala sina mpinzani
Mzuri ka hina kindani
Mi jogoo la Mikindani
nadhani unabaini, sisemi na shwaini
Tafuta mnazi ukwee, ugeme labda pombe
Kwani kwenye starehe ya vina nachukua kikombe
Hata uombe, uchinje ng'ombe utambike Njombe
Baki na bonge la donge, huku walia chonde chonde
Mswahili mahiri na staili sizoghairi
Mashairi hariri kamili kukudhalili
Napitisha sheria, inayokataza kulia
Nikikupiga panga usiweze kuugulia
Nakupa mitihani ya kughani kwenye fani
Usipofika kani huwezekani kuingia laini
Nakusimamisha kama huna leseni, nenda traffic stesheni
We mtoto tu waoga kwenye beseni
 
Unaogopa?
Wanavita Umsolopagaaz Makumazan na Umbopa!
Mashairi unakopa, unga unga bopa bopa?
Umechoka? huna cha kunena unafoka?
Unajiona umetoka kumbe bado umepotoka
Hujui unapokwenda wala kule unapotoka
Spidi ya Gulfstream huipati kwayo Foka
Usilete Mahoka, galasha jokeri joka
Nguvu za Coca, pangusa vyako vimoka
Huliwezi soka, uwanjani toka
Twache makocha tuchane vocha
We ndondocha dondoka mdondo
Ka mnywa gongo mbogo, aliyeshindia kipande cha muhogo
Kama Kublai Khan, ngomeyo naihusuru
Bila msululu wa suluhu kamwe siinusuru
Hii nyukilia, ila siyo kwa asali
Usiposikia utakutana na ajali
Chernobyl au Bhopal, rungu lake Umbopa
We acha kuropoka,
Bila vina wala mizani
Unachina kizani
Wewe dinner dizaini
Wala sina mpinzani
Mzuri ka hina kindani
Mi jogoo la Mikindani
nadhani unabaini, sisemi na shwaini
Tafuta mnazi ukwee, ugeme labda pombe
Kwani kwenye starehe ya vina nachukua kikombe
Hata uombe, uchinje ng'ombe utambike Njombe
Baki na bonge la donge, huku walia chonde chonde
Mswahili mahiri na staili sizoghairi
Mashairi hariri kamili kukudhalili
Napitisha sheria, inayokataza kulia
Nikikupiga panga usiweze kuugulia
Nakupa mitihani ya kughani kwenye fani
Usipofika kani huwezekani kuingia laini
Nakusimamisha kama huna leseni, nenda traffic stesheni
We mtoto tu waoga kwenye beseni
iko deep sana mazee
iko dip sana mazee
hii clip safi mazee
hii script kali mazee
 
iko deep sana mazee
iko dip sana mazee
hii clip safi mazee
hii script kali mazee

Toka historia mpaka tamthiliya
Simulizi simulia, tungo zizotulia
Hatua hatua mpaka watajua
Mwinyimkuu katua, vitu anafyatua
 
Toka historia mpaka tamthiliya
Simulizi simulia, tungo zizotulia
Hatua hatua mpaka watajua
Mwinyimkuu katua, vitu anafyatua

mhh,aahh, mhhh... maybe!
toka morning mazee nimeona platinum skills
Geoff, Nguli, Radical really got the skills
their flows, hotshots and style really got me going
Radical really got the avatar right
Geoff got the G spot right
Nguli really brought this stuff right

Now k-rang'a, show me what you got dude
 
DISCLAIMER: MASHAIRI YOTE YATAKAYOPOSTIWA HAPA YATABAKIA MALI YA JAMII FORUM. COM.
Mimi nimeshayacopy, naenda kuyatumia,
Yameshaibiwa mangapi, na kesi hatujasikia,
Hivi Majani yu wapi, aje kunirekodia,
Nitamshirikisha Pape, we Nguli umefulia
 
Mabaya niyaogope kama kinena
Huyu wa Darisalamu, matusi anaandika,
Kuna watoto humu, kama Nguli na Paka,
Kwao matusi ni sumu, hayapaswi kusikika,
Usije pewa hukumu, na ban ya uhakika
 
ookk.. i know am new bt i know am cool..
tryna get the vibe n' soon i rule..
heard them say jesus walks bt didnt believe and thot them fools
now came too JF home of great thinkers, warn them niggas that am good
nahhh dont be scared.. hahaha am only playing witchu fools..
dont mean disrespect, n ddnt mean to be rude.....
the rap is crap only liked the thread dude..
 
who's this mporipori,
who goes by the name Nguli,
your freestlyles are zero, oh sifuri,

dont mess with me al break your nose,
and ruin your swaga aka pose,
am the best I suppose.

this is not my style but,
I couldn't resist,
you try so hard like you the best
but your s**t aint all that
huwezi kuamini, lakini
kwenye mic ni mkatili kama Idd Amin
hii mistari ilimkimbiza senti hamsini...............
 
Burn na Masanilo katika yetu fani mnaniabisha
Najua ni ngumu kuumiza kichwa JF tunatisha
Kuna wengi wataiga msiogope tutawashusha busha
Mmbanwa sana na baridi basi hameni huko Arusha
 
this is not my style but,
I couldn't resist,
you try so hard like you the best
but your s**t aint all that
huwezi kuamini, lakini
kwenye mic ni mkatili kama Idd Amin
hii mistari ilimkimbiza senti hamsini...............

"th best" why pick me nigga if u dont b'liv I am,
man control your charm, al control my calm,
You Idd Amin, natuma kwako salam,
kama Nyerere in 19-seventy nine, the old man frm Butiama,

will take you from your hide-out,
and bring you to your fall-down,
4ever all be wearing the crown.
 
Huyu wa Darisalamu, matusi anaandika,
Kuna watoto humu, kama Nguli na Paka,
Kwao matusi ni sumu, hayapaswi kusikika,
Usije pewa hukumu, na ban ya uhakika

Huh!
Hii kali tena!

Mi ni yenu kaka, ukweli naeleza
Sitaki kuyapika, majungu naeleza
Amri nimeshika, za Mungu Muweza
 
Huh!
Hii kali tena!

Mi ni yenu kaka, ukweli naeleza
Sitaki kuyapika, majungu naeleza
Amri nimeshika, za Mungu Muweza
hehehehe!
kaka tumekubali,kwamba wewe mkali
kaka una maadili,kaka hutaki shari
kaka reta habari,kaskazini aje baridi
kaka fanya bidii,kuwapa vijana maadili
 
ushauri mwanana
marefu kwa mapana
hakika nguli umenena
mabaya niyaogope kama kinena
machungu nisilete kwa tunayependana
akili na uwezo tumepewa naye maulana
tukizitumia kwa hakika hatutobezana
heshima ikiwepo matamu tutashirikishana
.......:d:d:d
 
hehehehe!
kaka tumekubali,kwamba wewe mkali
kaka una maadili,kaka hutaki shari
kaka reta habari,kaskazini aje baridi
kaka fanya bidii,kuwapa vijana maadili

Kaskazini baridi , ndugu zako tunaganda
hadi mvua zenye radi, Mola ndiye atulinda
tumezipanda saladi, ili njaa kuishinda
tumeiweka ahadi, wala hatutoipinda
kweli tutajitahidi, japo twavaa marinda!
 
Back
Top Bottom