JF EXCLUSIVE: DOWANS vs TANESCO, the saga continues!

May someone please explain what this is all about?
Coach Parcells, kwa kifupi,
1. Baada ya ICC kuitioza Tanesco walipe zile US$65m plus interest ambazo zinaitwa tozo za Dowans.
2. Tozo hiyo inapaswa isajiliwe na Mahakama Kuu hapa nchini ili iweze kuwa enforceble by lacal laws, yaani Tanesco wawajibike/kulazimishwa kulipa.
3. Kabla mahakama kuu haijatoa uamuzi wa kuisajili tozo hiyo, tayari kuna kesi nyingine 4 zimefunguliwa mahakama kuu kupinga kulipwa kwa tozo hiyo.
4. Hivyo uamuzi wa mahakama kuu kuisajili tozo hiyo unaweza kuchelewa mpaka Desemba 2011 au zaidi ili kuzosikiliza pingamizi hizo.
5. Ili mshitaki Dowans asizidi kupoteza haki zake, ameipandisha Tanesco kwenye mahakama ya Uingereza, akiomba mahakama hiyo kutoa uamuzi wa kukazia hukumu ya ICC, kwa kuiomba itoe kibali cha kuzishika mali za Tanesco zilizoko Uingereza au Jumuiya ya Ulaya ili mali hizo zitumike kama dhamana/security ya kuishinikiza Tanesco kulipo tozo husika.
6. Hiyo mahakama hiyo ya Uingereza imeitaka Tanesco kulipa Dola Milioni 5 zitumike kama security kusubiri uamuzi wa Mahakama kuu ya Tanzania kuisajili tozo ya Dowans.
7. Mahakama hiyo imeridia msimao wa mkataba ule ambao kwa ridhaa yao wenyewe waliamua uamuzi wa ICC ndio wa mwisho na haukutakiwa kupingwa wala kucheleweshwa.

My Take.
Wana bodi wenzangu, hii ni issue ya kisheria na sio kisiasa, nawashauri tupunguze kidogo politics kwenye masuala ya kisheria. Niliwahi kusisitiza, ule mkataba ni mkataba bomu, Tanesco walijifunga na hawana pa kutokea dawa ni kulipa tuu!.

Ila pia naungana na hoja za Tanesco kuwa wao hawalipi kwa vile aliyewaingiza kwenye mtego huo ni serikali, hivyo ni jukumu la serikali kulipa na sio Tanesco.

Nyerere angekuwa ni rais wa nchi hii, tungevunja uhusiano na ICC, tusingelipa chochote!, mitambo tungetaifisha!, hao wawekezaji wa ulaya wangefungasha virago vyao na kwenda makwao wakatengeneze dhahabu na gesi zao huko viwandani kwao. Wachina wangetuletea teknolojia ya kuichimba dhahabu yetu, gesi yetu na mafuta yetu huku faida asilimia 100%, ikibaki ni mali yetu, kuliko sasa wanavyochimba hawa maharamia kwa jina la waweklezaji, wakikomba asilimia 98% huku wakituachia asilimia 2% eti ndio royality!.

Lakini kwa vile siye yeye, waliopo wanaheshimu utawala wa sheria, wawekezaji ndio tunawanyenyekea na kuwalamba miguu, amini nawaambieni, Tozo tutalipa, tena sio Tanesco, bali serikali kwa kodi zetu!.
 
Nilikwisha sema kitambo humu humu JF siku za mwanzo kabisa wakati kesi imefunguliwa huko Paris kwamba njia pekee ya Tanesco kuokoka na mikataba hiyo na madudu yake (Malipo) ni kujitangaza imefilisika...(bankruptsy). Hao wanaotaka kufungua kesi ZAO dhidi ya Tanesco waendelee tu kizifungua na watakuwa wanapoteza resources zao bure kwa kuifungulia kampuni muflisi mashtaka...

Hebu niembieni jamani hivi ni kwa nini Tanesco wanang'ang'ania sana kuendelea kuwepo ili hali kila siku utasikia wanadhaminiwa na kodi zetu kupitia serikalini kuchukua mikopo ya kujiendesha...na kila siku utasikia habari za megawati hewa !!!

Kazi ya umeme imewashinda.. inafaa wakubali kwamba kazi hii ya uzalishaji hawaiwezi na kuachia manyanga na labda watanzania wataunda Tanesco nyingine itakayokuwa free na hizi legal issues na madudu mengine...

Yangu macho na hongera invisible kwa kutuhabarisha haya madudu mengine... lakini ukweli utabaki pale pale kwamba kila siku ukifungua JF na kuona habari za Tanesco hata kabla ya kuzisoma roho inaanza kudunda kwa kujua kwamba wanaongezewa mzigo mwingine wa malipo...
 
Nilikwisha sema kitambo humu humu JF siku za mwanzo kabisa wakati kesi imefunguliwa huko Paris kwamba njia pekee ya Tanesco kuokoka na mikataba hiyo na madudu yake (Malipo) ni kujitangaza imefilisika...(bankruptsy). Hao wanaotaka kufungua kesi ZAO dhidi ya Tanesco waendelee tu kizifungua na watakuwa wanapoteza resources zao bure kwa kuifungulia kampuni muflisi mashtaka...

Hebu niembieni jamani hivi ni kwa nini Tanesco wanang'ang'ania sana kuendelea kuwepo ili hali kila siku utasikia wanadhaminiwa na kodi zetu kupitia serikalini kuchukua mikopo ya kujiendesha...na kila siku utasikia habari za megawati hewa !!!

Kazi ya umeme imewashinda.. inafaa wakubali kwamba kazi hii ya uzalishaji hawaiwezi na kuachia manyanga na labda watanzania wataunda Tanesco nyingine itakayokuwa free na hizi legal issues na madudu mengine...

Yangu macho na hongera invisible kwa kutuhabarisha haya madudu mengine... lakini ukweli utabaki pale pale kwamba kila siku ukifungua JF na kuona habari za Tanesco hata kabla ya kuzisoma roho inaanza kudunda kwa kujua kwamba wanaongezewa mzigo mwingine wa malipo...
S.M.P2503, naomba tofautisha kesi za jina na madai, kesi ya madai huishia pale mdaiwa anapokuwa mufilisi, hata Tanesco ikitangaza kufilisika, assets za Tanesco zitawekwa kwenye attachment ili kulipa registered madeni. Sasa ukilinganisha tozo ya dowans na assets za Tanesco, hiyo tozo ni peanut!.
 
You should have at least laid out your understanding or what you think is the implied meaning of the quoted statements, because you could have taken them out of their legal context, msee.
Not necessarily, especially given the kind of legal language aka legalese applied here. The statements provided appear to be open to interpretation. That being said, you'll need to clarify as to the particular context(s) these statements allude to (according to you), and your own understanding of their legal meanings and/or consequences.

I haven't read the ruling in full yet, but I may help on what you're debating about. The provisions you have referred are clear. The agreement entered between Dowans and Tanesco states that "The decision of the arbitrator shall be final and binding upon the Parties." This clause is based on Tanzanian Arbitration Act 1996 which states that "the award to be made by the arbitrators or umpires shall be final and binding on the parties and the persons claiming under them respectively".

Now, this is a very very old law and is based on the Geneva Convention on the Enforcement of Foreign Judgments of 1927. I don't understand why we're still using using this outdated law. The Geneva Convention was replaced in 1958 by the New York Convention on the Recognition and enforcement of foreign Arbitral Awards. One of the things, the New York Convention did was to replace the word "final" in the Geneva Convention with the word "binding".

Even the ICC Rules which were used to arbitrate the DOWANS/TANESCO dispute states that "Every Award shall be binding on the parties." It does not say that it should be final. The UK Arbitration Act is also based on the new law. That is why the judge said that in this case, he will have to refer to the English old law because the agreement was made basing on the old law.

Just yesterday I was reading that although the New York Convention 1958 has replaced the Geneva Convention 1927, shockingly, there are still few countries which have arbitration laws based on the Geneva Convention. It did not come to my mind that Tanzania was among those few countries, because our Arbitration Act was passed in 1996.

Why we passed the Act based on the Geneva Convention 1927, instead of the New York Convention 1958 (a United Nations Convention), I don't know. If our Arbitration Act was based on the New York Convention, Dowans would not have been able to bring this action because the abitral award would have been binding but not final. The words "final" and "binding" have serious legal implications. That is why the new law replaced the former with the later. Seriously, using this 19th century's law is costing us.

This thread has serious legal implications, but unfortunately, it will be politicized if not yet. I hope our lawmakers will notice this and demand the law to be updated as soon as possible.
 
Na mitambo tunayo kwa jina la Symbion tunailipa. Huku tutalipa na huu upuuzi mwingine! Kuna namna ya kuanza upya Taifa hili?
 
  • Thanks
Reactions: Aza
dawa ni ubabe,kisheria hatuwezi,kama mkuu wetu wa nchi yupo tayari tuitaifishe kibabe na kuvunja mahusiano na hiyo mahakama full stop!
 
May someone please explain what this is all about?

IKO kisheria sana tungepata Mtaalam wa Lugha za kisheria atutafunie sisi wabeba zege maana shule zenyewe tumesoma St CCM, Chuo tumefundishwa na waadhiri walofail, wale wazuri wooote wako kwenye Siasa...
 
aisee safari kweli ni ndefu e mungu jaalia taifa hili
ni kweli mkuu hapa CCM sijui itatokajetokaje..kuna gemu wanachezeana wao kwa wao humo ndani.. kuhusu Chadema kwenye jambo kama hili kuwa wangefanya nini .. nina uhakika chama makini kama chadema kisingefanya uzembe wa kuingia kwenye janga kama hili .. na kama wangeingia katika hali kama hii basi ingebidi wafanye maamuzi magumu . ccm hawawezi kufanya maamuzi magumu sio kwamba hawataki au hawapendi .. ni kwamba hawawezi na yapo nje ya uwezo wao
 
Mkuu, CCM hapa itafanya nini kweli? Hawawezi kufanya lolote, pendekezo letu la awali la TANESCO kujitangaza mufilisi lilikuwa na maana japo lilipuuzwa!

Kama CHADEMA au hata CUF wanaweza kuwalaumu CCM kwa hili (la leo) basi watwambie the way forward (wangefanya nini wao katika hali kama hii)

Mkuu, umesahau kuwa CCM ndiyo waliileta Richmond na baadaye Dowans?? Hawawezi kukwepa lawama
 
Utadhani wakati wanaingia mkataba walikuwa wamelewa, hivi vitu ambavyo (kwa umakini) tungeweza kuvikwepa tumejiingiza kichwakichwa na waliofanya hivyo wapo mitaani wanadunda,tufike mahala uzembe wa namna uwe punished legally with heavy sentence ndio tutakaa sawa,ama sivyo tutaendelea kujionea vioja na rasilimsli zetu zinakwapuliwa mchana kweupe...
 
Hivi ruling ya High Court Tanzania ilishatolewa? Kama bado, halafu hawa matapeli wanaanzisha shauri jingine huko nje nadhani itakuwa ni sarakasi za kisheria!
Hawa Dowans wanafanya haya kwa kushirikiana na watanzania wenzetu, hapa dawa ni kuchapana bakora baadhi ya watu wakatafute hifadhi ya ukimbizi huko wanakoficha vijisenti vyao. Natamani ile sheria ya uhujumu uchumi ingefufuliwa kutoka makabrasha ya Hayati Sokoine, tusingeona upuuzi kama huu.
Kakalende, Matapeli wakati wote huwa wanaangalia upepo unavyoenda nakuhakikisha wamejiweka usawa wa kutopoteza walicho ki target , hii ni pamoja na kutumia vifungu vya sheria kuweka sawa mambo ili yawe kisheria zaidi kuliko kitapeli.
 
Hawa Dowans wanafanya haya kwa kushirikiana na watanzania wenzetu, hapa dawa ni kuchapana bakora baadhi ya watu wakatafute hifadhi ya ukimbizi huko wanakoficha vijisenti vyao.


Nadhani tulipofikia sasa, yumkini wananchi watasema enough is enough, ninaogopa kama watu watajichukulia sheria mkononi. Unalosema ni kweli kuwwa hawa jamaa ni watanzania wenzetu ambao''wameshiba kwa kutuibia na sasa wanatutapikia na mwisho watatufanyia kitu mbaya...' This is too much wasee!
 
Coach Parcells, kwa kifupi,

Nyerere angekuwa ni rais wa nchi hii, tungevunja uhusiano na ICC, tusingelipa chochote!, mitambo tungetaifisha!, hao wawekezaji wa ulaya wangefungasha virago vyao na kwenda makwao wakatengeneze dhahabu na gesi zao huko viwandani kwao. Wachina wangetuletea teknolojia ya kuichimba dhahabu yetu, gesi yetu na mafuta yetu huku faida asilimia 100%, ikibaki ni mali yetu, kuliko sasa wanavyochimba hawa maharamia kwa jina la waweklezaji, wakikomba asilimia 98% huku wakituachia asilimia 2% eti ndio royality!.

Lakini kwa vile siye yeye, waliopo wanaheshimu utawala wa sheria, wawekezaji ndio tunawanyenyekea na kuwalamba miguu, amini nawaambieni, Tozo tutalipa, tena sio Tanesco, bali serikali kwa kodi zetu!.

hili lingekua jambo murua hasa
shida inakuja kwamba hii ishu inawahusu haswa RA/EL ss nani aanze kumfunga mwezie
JK ana shida sana
 
dawa ni ubabe,kisheria hatuwezi,kama mkuu wetu wa nchi yupo tayari tuitaifishe kibabe na kuvunja mahusiano na hiyo mahakama full stop!

@MTAZAMO, nakubalina na wewe kabisa.Tukienda kwa mtindo wa kufuata sheria tutadumbukia kuzimu. Hapa solution ni kufanya 'street law' kwamba hatulipi hata cent moja, na kama ni kutaifaisha mali za TANESCO zilizoko Uingereza na sisi tufanye hivyo hivyo hapa - jino kwa jino, liwalo na liwe. Inabidi tujilipue na kuwa maskini jeuri vingenevyo tutakamuliwa damu!
 
Samahani wakubwa, kama tujuavyo umeme hakuna so tunatumia simu basi naomba taarifa ambazo zipo kwenye pdf mzifungue na mtuweke ili nasi tupate kuchangia, ni hayo tu.
 
nashindwa nifanye nini sijui nilie... sijui nicheke!!! serikali imejaa viongozi wazembe weye elimu za enzi za TANU hazipo updated ..... saa hizi hata huyo mwanasheria hakuusoma mkataba.. macho yote yalikuwa kwenye pesa
 
Back
Top Bottom