JF doctor's msaada jamani,maumivu ya tumbo na kutotoka maziwa kwa mama mtoto

DullyJr

JF-Expert Member
Apr 10, 2011
13,979
11,815
Habari zenu wakubwa.

Mke wangu kajifungua jana saa 4 asubuh tatizo toka ajifungue maziwa hayatoki yan mtoto hajanyonya mpaka dakika hii, mama mtoto anaumwa tumbo kama la uchungu, nisaidieni kujua dawa ya kuondoa au kupunguza maumivu ya tumbo, pia kusaidia maziwa yatoke kwani hayatoki kabisa na akijaribu kunyonya tumbo ndo linaanza kuuma!

Ahsanteni.
 
Nasubiri msaada wenu jamani kwani namuonea huruma mtoto analia sana yani hajanyonya toka azaliwe!
Mungu awazidishie
 
Mkuu Pole,
Mama ana uzito kiasi gani, urefu?
Mama alijifungulia wapi?
Mimba ya miezi mingapi?
- Je, alikuwa na tatizo lolote wakati wa ujauzito?
-Je, Mtoto alikuwa na tatizo lolote wakati wa kujifungua?
- Mama alipoteza fahamu, mara baada ya kujifungua?
-Kuna dawa zozote anazotumia za muda mrefu?
- Je, mama alikuwa ana tatizo lolote la siku za hedhi(kutokueleweka)?
 
Hongera kwa kupata mtoto.
Kuhusu tumbo sijajua shida iko wapi. Labda angerudi kwa gynae wake. Ila kuhusu maziwa kutoka kama hana vidonda vya tumbo mpe uji wa mahindi mwepesi wenye pilipili manga. Works like magic. Maziwa yataanza kutoka. Ale vizuri pia na kulala vya kutosha.
Kila la kheri. Mungu awatunze wote.
 
Well maumivu ya tumbo baada ya kujifungua nadhani ni kawaida hasa kwa mama aliyejifungua kwa operation, binafsiniliexperience hilo ni kwamba uterus inacontract kurudi kwenye normal size sasa na yale maumivu ya mshono ni balaa,yani ni exactly km uchungu,na poa maziwa kuchelewa kutoka inatokea, m mmoja alivocomment vitu vya moto hasa uji mwepesi wa pilipili manga mi niliunywa sanaaa maziwa yakaanza kutoka afta 4 days ila nilimwanzishia formula baada ya kuona yamegoma na mtt anasuffer.

Sasa basi,mtoto anapokua anajaribu kunyonya ili kustimulate yale maziwa yatoke hayo maumivu ya tumbo nayo yanazidi ni balaa.cha msingi apate pain killers atakazoandikiwa na dr na aendelee kumyonyesha mtt ivoivo hadi yatakapoanza kutoka.hongeren sana
 
Je amejifungua normal au c/section?maana binafsi I had my first born thru normal delivery sikuexperience hiyo kabisa,but with my second born thru c/section nilipata hiyo hali exactly as u explained.labda umcontact dr wake awape advise ila mi nilivumilia afta the first 3 days na hiyo hali ikapotea.
 
Mkuu Pole,
Mama ana uzito kiasi gani, urefu?
Mama alijifungulia wapi?
Mimba ya miezi mingapi?
- Je, alikuwa na tatizo lolote wakati wa ujauzito?
-Je, Mtoto alikuwa na tatizo lolote wakati wa kujifungua?
- Mama alipoteza fahamu, mara baada ya kujifungua?
-Kuna dawa zozote anazotumia za muda mrefu?
- Je, mama alikuwa ana tatizo lolote la siku za hedhi(kutokueleweka)?

mama mtoto ana 59kg
kajifungua hospitalini (palestina sinza)
mimba ya miezi9 na kajifungua kwa njia ya kawaida,
katika kipindi cha ujauzito kulikuwa hakuna tatizo zaidi ya yale ya kawaida tu kwa wajawazito wote
mtoto hana tatizo lolote zaidi ya hilo la kulia sana nafikiri kwasababu ya njaa
mama hatumii dawa zozote za muda mrefu
na pia hana tatizo la siku za hedhi
 
Hongera kwa kupata mtoto.
Kuhusu tumbo sijajua shida iko wapi. Labda angerudi kwa gynae wake. Ila kuhusu maziwa kutoka kama hana vidonda vya tumbo mpe uji wa mahindi mwepesi wenye pilipili manga. Works like magic. Maziwa yataanza kutoka. Ale vizuri pia na kulala vya kutosha.
Kila la kheri. Mungu awatunze wote.

kwanza nashukuru sana,
pia nikushukuru kwani nimemwanzishia huo uji mtoto amenyonya kidogo yameanza kutoka ila mama tumbo linamuuma mpaka anashndwa kunyonyesha
 
Je amejifungua normal au c/section?maana binafsi I had my first born thru normal delivery sikuexperience hiyo kabisa,but with my second born thru c/section nilipata hiyo hali exactly as u explained.labda umcontact dr wake awape advise ila mi nilivumilia afta the first 3 days na hiyo hali ikapotea.

kajifungua kwa njia ya kawaida tu!
Maziwa yameanza kutoka kdg ila mama anaumwa sana na tumbo.
Nashkuru kwa michango yenu ndugu zangu mbarikiwe sana
 
Mkuu lidaku, pole..

Habari njema mama kuendelea vizuri, ningeshauri mama kurudi hospitali, kuchunguzwa zaidi(kama kuna kuna shida yeyote. mfano kondo la nyuma kubaki, homa , n.k)

Mtoto:
Ni vizuri kuzingatia ushauri mliopewa na daktari..mf. Kumnyonyesha maziwa pekee kwa muda wa miezi 6, kupata chanjo, n.k.
 
Je amejifungua normal au c/section?maana binafsi I had my first born thru normal delivery sikuexperience hiyo kabisa,but with my second born thru c/section nilipata hiyo hali exactly as u explained.labda umcontact dr wake awape advise ila mi nilivumilia afta the first 3 days na hiyo hali ikapotea.

amejifungua kawaida tu,nashkuru sana kwa michango yenu
 
Mkuu lidaku, pole..

Habari njema mama kuendelea vizuri, ningeshauri mama kurudi hospitali, kuchunguzwa zaidi(kama kuna kuna shida yeyote. mfano kondo la nyuma kubaki, homa , n.k)

Mtoto:
Ni vizuri kuzingatia ushauri mliopewa na daktari..mf. Kumnyonyesha maziwa pekee kwa muda wa miezi 6, kupata chanjo, n.k.

nashkuru sana kwa mchango wako ndugu yangu ubarikiwe sana
 
nashkuru sana kwa mchango wako ndugu yangu ubarikiwe sana

Hongera sana mkuu, nadhani zingatia ushauri wa kitaalam hapo juu na pia maziwa ni let down reflex, mtoto anaponyonya ndio anasababisha chuchu kupata hisia na kupeleka habari kwa ubongo ili utengeneze maziwa zaidi, hivyo kikubwa mama aendelee kumweka mtoto kwenye chuchu aendelee kuvuta maziwa yatatoka tu hii ikiwa ni pamoja na mama kula na kupata vitu vvya maji maji mara kwa mara, supu, uji.

kingine ni kuwa tayari kisaikolojia, mama akiwa na msongo wa mawazo pia husababisha kushindwa kutoa maziwa, mafariji na mtie moyo asiwe na stess. Kuumwa tumbo hiyo inaiwa After pain, mtoto anapovuta nyonyo zaidi ya maziwa kutoka pia ubongo wa mama hutoa kichocheo kiitwacho Oxytocin ambacho kazi yake ni kusababisha kusinyaa/Contractions za mji wa uzazi, Uterus ili kuweza kurudi katika hali ya kawaida na hii husababisha tumbo kuuma.

kama hakuna damu insyotoka, uchafu wenye harufi, na maelezo mengine kama wenzangu walivyosema hapo juu hayo maumivu yataisha pole pole, kumbuka mtoto ananyonya maziwa ya mama tu kwa sasa hata maji usimpe, mungu awabariki sana
 
Uyo mama mtafutie pweza mkavu atamwaga mziwa kama bomba na kuhusu tumbo hii huwa ni kawaida uchungu unakua haujamaliza kuna dawa mimi nilimchukulia mke wangu dubai mara hii kajifungua juzi hajapata maumivu ya tumbo baada ya kujifungua zinaitwa ESPASMO CANULACE
 
Back
Top Bottom