Jeshi la wananchi (kambi ya gongo la mboto) limeasi?

Lukolo

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
5,143
3,196
Katika namna ambayo inatia mashaka, kambi ya jeshi ya gongo la mboto imeendeleza mfululizo wa mauaji, ukatili, unyama na ubabe kwa wananchi wasio na hatia. Wakati wananchi wakiendelea kuugulia maumivu ya mabomu yanayoaminika kulipuliwa kwa makusudi na wanajeshi hao wa gongo la mboto, jana wanajeshi hao walitinga mitaani na kuanza kutembeza kichapo kwa raia wasio na hatia. Kwangu mimi, hii ni ishara kwamba wanajeshi hawa wa kambi ya jeshi ya gongo la mboto hawapo kwa ajili ya ulinzi wa wananchi bali wapo kwa ajili ya kuangamiza na kuteketeza wananchi wa maeneo ya jirani. Hii inanipa shaka pia kwamba wanajeshi hawa wanye hasira na wananchi, wanaweza kuyalipua tena mabomu yaliyobakia pale ghalani ili kuwamaliza kabisa wananchi walio karibu na kambi hii au wa Dar es salaam nzima kwa kuwa tumeambiwa yaliyobakia ni makubwa zaidi ya yaliyolipuka.

Kuna ushahidi mwingi wa kimazingira unaoonyesha kwamba mabomu ya gongo la mboto yalilipuliwa kwa makusudi ili kuwaua na kuwaangamiza watanzania wasio na hatia. Ushahidi mmojawapo ni kitendo cha wanajeshi hao kuhamisha familia zao mapema asubuhi kabla ya milipuko na kutokuwepo kwa wanajeshi wengine hapo kambini isipokuwa walinzi. Kama wanajeshi hawa walijua kungekuwa na milipuko hiyo, kwanini hawakuwatangazia wananchi ili wakae mbali na maeneo ya jeshi? Huu ni ushahidi tosha kwamba pana uasi hapa! Kwa mazingira ya ulipukaji wa mabomu, na kwa yale yaliyofanyika jana, ya wanajeshi kuwavamia raia wasio na hatia na kuwachapa, najiridhisha kwamba wanajeshi wa kambi hii wameshaasi, na hivyo siku si nyingi wanaweza kushika bunduki na kuingia mitaani kutuua kwa risasi baada ya jaribio la kutuua kwa mabomu kutokuzaa matunda yaliyotarajiwa.

Mwisho natoa wito kwa wakaazi wa gongo la mboto na maeneo ya jirani kuandaa maandamano ya kulipinga jeshi hili lililoasi na pia kumpinga Kikwete kwa kuwa ameshindwa kusoma alama za nyakati na kuchukua hatua.
 
Poleni inasikitisha sana sababu ya kutembeza kichapo ni nini?
Binafsi hata sijui, nilijikuta naingia tu kwenye mkumbo wa kichapo bila hata kuambiwa kwanini nachapwa. Jamaa walikuwa wanatoa kisago kile cha kuua kabisa. Ni bakola, ngumi, teke, vichwa and so on. Yaani utafikiri ndo tupo vitani kabisa. Ukionyesha kutaka kujibu wanasaidiana hata watatu kukushambulia. Hali ilikuwa ni mbaya, hawajali upo na nani, kama upo na mkeo unaweza kula kipigo wewe na mkeo au hata na babako au mamako. Kwakweli ni situation inayoudhi kwelikweli.
 
Duh poleni nimekwama hata kuandika najaribu kuhisi pengine waliowapiga ni wanajeshi wa nchi nyingine si unajua huwa mavazi yanafanana au wamepata wazimu . Katika hali ya kawaida huwezi kupiga mtu sembuse watu bila sababu . Nimekumbuka inawezekana wameamua kutumia njia hiyo kuishinikiza serikali iwaboreshee maslahi huku uraiani si huwa tunaandamana
 
Hii habari binafsi nimesimuliwa na mkazi wa g.mboto kwa njia ya simu "Ebwana kuna mwanajeshi kavamiwa na wananchi kapigwa kweli kisa eti wanasema wanajeshi walifanya makusudi kulipua mabomu" kiukweli nlifadhaishwa sana,gafla akapga simu tena "jamaa wamerudi wanagawa kpgo hapa nipo njian nakimbia" jamaa unapoleta hoja kama hiyo nivema utoe sababu zilizosababisha kuliko kuleta hoja ambazo zitatuwekea uadui na walinzi wa taifa letu! Kiukweli jamaa wanafany kazi ngumu mno,binafsi nimetokea mipakan 'hawalali kutulinda sisi' inaleta hasira unamlinda mtu tena kwa kujitolea then mnampga mmojawao What are we expecting?
 
Hapo wote wamekosa busara raia na hao wanajeshi ila wanajeshi kwa walipaswa kuwa na busara zaidi ili la kupiga watu hovyo halijatulia hata kidogo
 
Katika namna ambayo inatia mashaka, kambi ya jeshi ya gongo la mboto imeendeleza mfululizo wa mauaji, ukatili, unyama na ubabe kwa wananchi wasio na hatia. Wakati wananchi wakiendelea kuugulia maumivu ya mabomu yanayoaminika kulipuliwa kwa makusudi na wanajeshi hao wa gongo la mboto, jana wanajeshi hao walitinga mitaani na kuanza kutembeza kichapo kwa raia wasio na hatia. Kwangu mimi, hii ni ishara kwamba wanajeshi hawa wa kambi ya jeshi ya gongo la mboto hawapo kwa ajili ya ulinzi wa wananchi bali wapo kwa ajili ya kuangamiza na kuteketeza wananchi wa maeneo ya jirani. Hii inanipa shaka pia kwamba wanajeshi hawa wanye hasira na wananchi, wanaweza kuyalipua tena mabomu yaliyobakia pale ghalani ili kuwamaliza kabisa wananchi walio karibu na kambi hii au wa Dar es salaam nzima kwa kuwa tumeambiwa yaliyobakia ni makubwa zaidi ya yaliyolipuka.

Kuna ushahidi mwingi wa kimazingira unaoonyesha kwamba mabomu ya gongo la mboto yalilipuliwa kwa makusudi ili kuwaua na kuwaangamiza watanzania wasio na hatia. Ushahidi mmojawapo ni kitendo cha wanajeshi hao kuhamisha familia zao mapema asubuhi kabla ya milipuko na kutokuwepo kwa wanajeshi wengine hapo kambini isipokuwa walinzi. Kama wanajeshi hawa walijua kungekuwa na milipuko hiyo, kwanini hawakuwatangazia wananchi ili wakae mbali na maeneo ya jeshi? Huu ni ushahidi tosha kwamba pana uasi hapa! Kwa mazingira ya ulipukaji wa mabomu, na kwa yale yaliyofanyika jana, ya wanajeshi kuwavamia raia wasio na hatia na kuwachapa, najiridhisha kwamba wanajeshi wa kambi hii wameshaasi, na hivyo siku si nyingi wanaweza kushika bunduki na kuingia mitaani kutuua kwa risasi baada ya jaribio la kutuua kwa mabomu kutokuzaa matunda yaliyotarajiwa.

Mwisho natoa wito kwa wakaazi wa gongo la mboto na maeneo ya jirani kuandaa maandamano ya kulipinga jeshi hili lililoasi na pia kumpinga Kikwete kwa kuwa ameshindwa kusoma alama za nyakati na kuchukua hatua.

hameni.
 
Hapo wote wamekosa busara raia na hao wanajeshi ila wanajeshi kwa walipaswa kuwa na busara zaidi ili la kupiga watu hovyo halijatulia hata kidogo

busara kivipi mkuu? mbwa umlishe then akutafune utafanyaje? ni kutafut rifle tu uachanishe roho na mwili wake. in that case walikuwa sahihi kutoa dozi ili watu wawe na heshima. jeshi siyo la kudharauliwa hata na mtu wala kiongozi wa nchi. kueni muyaone. msilete siasa na jeshi. uhuru uwe na mipaka ndugu zanguni. huwezi wadharau watu wanakulinda na wanarisk maisha kwa ajili yetu sisi. wakanyeni wadogo na watoto zenu wasipige walinzi wa jamhuri yetu. kuhamisha familia ilikuwa sikukuu watu wako outing. mwe!
 
Binafsi hata sijui, nilijikuta naingia tu kwenye mkumbo wa kichapo bila hata kuambiwa kwanini nachapwa. Jamaa walikuwa wanatoa kisago kile cha kuua kabisa. Ni bakola, ngumi, teke, vichwa and so on. Yaani utafikiri ndo tupo vitani kabisa. Ukionyesha kutaka kujibu wanasaidiana hata watatu kukushambulia. Hali ilikuwa ni mbaya, hawajali upo na nani, kama upo na mkeo unaweza kula kipigo wewe na mkeo au hata na babako au mamako. Kwakweli ni situation inayoudhi kwelikweli.
hivi hawezekani kufungua kesi....
 
Wewe unaishi dunia gani?

Ni jeshi gani duniani liliwahi kupigana nawananchi wake likashinda??
Jeshi hushinda vita kwa nguvu ya wananchi siyo bunduki.

Jeshi likidharau na kuanza kupiga hata kuua wananchi Safari yakumegeka kwake na hatimaye kusambaratika huwa imezaliwa.

busara kivipi mkuu? mbwa umlishe then akutafune utafanyaje? ni kutafut rifle tu uachanishe roho na mwili wake. in that case walikuwa sahihi kutoa dozi ili watu wawe na heshima. jeshi siyo la kudharauliwa hata na mtu wala kiongozi wa nchi. kueni muyaone. msilete siasa na jeshi. uhuru uwe na mipaka ndugu zanguni. huwezi wadharau watu wanakulinda na wanarisk maisha kwa ajili yetu sisi. wakanyeni wadogo na watoto zenu wasipige walinzi wa jamhuri yetu. kuhamisha familia ilikuwa sikukuu watu wako outing. mwe!
 
Hii habari binafsi nimesimuliwa na mkazi wa g.mboto kwa njia ya simu "Ebwana kuna mwanajeshi kavamiwa na wananchi kapigwa kweli kisa eti wanasema wanajeshi walifanya makusudi kulipua mabomu" kiukweli nlifadhaishwa sana,gafla akapga simu tena "jamaa wamerudi wanagawa kpgo hapa nipo njian nakimbia" jamaa unapoleta hoja kama hiyo nivema utoe sababu zilizosababisha kuliko kuleta hoja ambazo zitatuwekea uadui na walinzi wa taifa letu! Kiukweli jamaa wanafany kazi ngumu mno,binafsi nimetokea mipakan 'hawalali kutulinda sisi' inaleta hasira unamlinda mtu tena kwa kujitolea then mnampga mmojawao What are we expecting?

kujitolea???kwani kazi ya ujeshi ni wito??vp hawalipwi hawa??
 
busara kivipi mkuu? mbwa umlishe then akutafune utafanyaje? ni kutafut rifle tu uachanishe roho na mwili wake. in that case walikuwa sahihi kutoa dozi ili watu wawe na heshima. jeshi siyo la kudharauliwa hata na mtu wala kiongozi wa nchi. kueni muyaone. msilete siasa na jeshi. uhuru uwe na mipaka ndugu zanguni. huwezi wadharau watu wanakulinda na wanarisk maisha kwa ajili yetu sisi. wakanyeni wadogo na watoto zenu wasipige walinzi wa jamhuri yetu. kuhamisha familia ilikuwa sikukuu watu wako outing. mwe!
we mwanajeshi acha kujustify ujinga wa wanajeshi kupiga raia. kuwa mjeshi siyo ndiyo iwe sifa kupiga watu
 
kwa kweli hili ni kosa kubwa mno alifai kufanywa na wanajeshi wetu ukizingatia tunaishi nao pamoja mitaani tunakunywa wote tunagombea madem wote leo wametulipulia mabomu watu wamekufa, nyumba zimeharibiwa leo wanatufata live kwa kichapo cha mbwa mwizi?
 
Sizinga,unaeshmika humu janvini..! Mtu anatoa uhai wake kukulinda ww na unafurahia utulivu,unaweza kumlipa kiasi gani mtu huyo!?

Mwanangu na uelewe kwamba,Jeshi ni samaki na sisi raia ni bahari mtoe samaki baharini hawezi kuishi
Na sisi tunatoa uhai wetu kuwalisha ni mgawao wa kazi tu.
Wanalinda nini! wakati mali za wananchi na nchi yenyewe inaibiwa na kubemendwa na mafisadi na matapeli wa kigeni wao wanaangalia tu na kuwapigia saluti.
Iko siku kitaeleweka tu.
 
busara kivipi mkuu? mbwa umlishe then akutafune utafanyaje? ni kutafut rifle tu uachanishe roho na mwili wake. in that case walikuwa sahihi kutoa dozi ili watu wawe na heshima. jeshi siyo la kudharauliwa hata na mtu wala kiongozi wa nchi. kueni muyaone. msilete siasa na jeshi. uhuru uwe na mipaka ndugu zanguni. huwezi wadharau watu wanakulinda na wanarisk maisha kwa ajili yetu sisi. wakanyeni wadogo na watoto zenu wasipige walinzi wa jamhuri yetu. kuhamisha familia ilikuwa sikukuu watu wako outing. mwe!

Sielewi hekima ya mfano wako anaelishwa ni nani kati ya raia na mwanajeshi (mbwa anaelishwa?)
Ni kweli hadi raisi wa nchi anawaogopa wanajeshi? maana yeye ni Amiri jeshi mkuu.
Hivyo basi Rais na wanajeshi lazima wawaogope na kuwaheshimu raia maana wao ndio walio waajiri.
KINYUME CHA HAPO WATAPAMBANA NA NGUVU YA UMMA.
 
Wanajeshi wakapimwe akili yawezekana wameathirika kisaikologia!
Na ninyi mliopewa kichapo mlishindwa kumkamata mmoja wao na kufa nae ka ushahidi????
 
Wanajeshi kupiga raia ni utovu wa nidhamu. Lakini kwa Tanzania hilo limekuwa gonjwa sugu. Raia wenapigwa sana na wanajeshi lakini mamlaka zinazohusika zinakaa kimya. Wanajeshi wanajiona wao ni untouchable katika nchi hii. Huwa wanachokoza raia kwenye mabaa, wakidundwa wanaenda kukusanya wenzao na kuleta maafa kwa raia hata wasio na hatia. Mie naomba niwakumbushe kama wamesahau. Kuna raia wengi sana wapepata mafunzo ya kijeshi na wana uwezo mkubwa sana kuliko hao wanajeshi feki waliopo sasa. Wasipojiheshimu watafundishwa adabu.

Halafu kujidai wanatulinda, mie sioni lilote wanalifanya. Wanatulinda na adui yupi? Wao wanatekeleza majukumu yao ya kazi kama wengine. Kama walimu, madaktari, polisi nk. Na mshahara wanalipwa kwa kodi zetu.

Wakiona kazi hiyo haiwafai waachane nayo.
 
Back
Top Bottom