Lukolo
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 5,143
- 3,196
Katika namna ambayo inatia mashaka, kambi ya jeshi ya gongo la mboto imeendeleza mfululizo wa mauaji, ukatili, unyama na ubabe kwa wananchi wasio na hatia. Wakati wananchi wakiendelea kuugulia maumivu ya mabomu yanayoaminika kulipuliwa kwa makusudi na wanajeshi hao wa gongo la mboto, jana wanajeshi hao walitinga mitaani na kuanza kutembeza kichapo kwa raia wasio na hatia. Kwangu mimi, hii ni ishara kwamba wanajeshi hawa wa kambi ya jeshi ya gongo la mboto hawapo kwa ajili ya ulinzi wa wananchi bali wapo kwa ajili ya kuangamiza na kuteketeza wananchi wa maeneo ya jirani. Hii inanipa shaka pia kwamba wanajeshi hawa wanye hasira na wananchi, wanaweza kuyalipua tena mabomu yaliyobakia pale ghalani ili kuwamaliza kabisa wananchi walio karibu na kambi hii au wa Dar es salaam nzima kwa kuwa tumeambiwa yaliyobakia ni makubwa zaidi ya yaliyolipuka.
Kuna ushahidi mwingi wa kimazingira unaoonyesha kwamba mabomu ya gongo la mboto yalilipuliwa kwa makusudi ili kuwaua na kuwaangamiza watanzania wasio na hatia. Ushahidi mmojawapo ni kitendo cha wanajeshi hao kuhamisha familia zao mapema asubuhi kabla ya milipuko na kutokuwepo kwa wanajeshi wengine hapo kambini isipokuwa walinzi. Kama wanajeshi hawa walijua kungekuwa na milipuko hiyo, kwanini hawakuwatangazia wananchi ili wakae mbali na maeneo ya jeshi? Huu ni ushahidi tosha kwamba pana uasi hapa! Kwa mazingira ya ulipukaji wa mabomu, na kwa yale yaliyofanyika jana, ya wanajeshi kuwavamia raia wasio na hatia na kuwachapa, najiridhisha kwamba wanajeshi wa kambi hii wameshaasi, na hivyo siku si nyingi wanaweza kushika bunduki na kuingia mitaani kutuua kwa risasi baada ya jaribio la kutuua kwa mabomu kutokuzaa matunda yaliyotarajiwa.
Mwisho natoa wito kwa wakaazi wa gongo la mboto na maeneo ya jirani kuandaa maandamano ya kulipinga jeshi hili lililoasi na pia kumpinga Kikwete kwa kuwa ameshindwa kusoma alama za nyakati na kuchukua hatua.
Kuna ushahidi mwingi wa kimazingira unaoonyesha kwamba mabomu ya gongo la mboto yalilipuliwa kwa makusudi ili kuwaua na kuwaangamiza watanzania wasio na hatia. Ushahidi mmojawapo ni kitendo cha wanajeshi hao kuhamisha familia zao mapema asubuhi kabla ya milipuko na kutokuwepo kwa wanajeshi wengine hapo kambini isipokuwa walinzi. Kama wanajeshi hawa walijua kungekuwa na milipuko hiyo, kwanini hawakuwatangazia wananchi ili wakae mbali na maeneo ya jeshi? Huu ni ushahidi tosha kwamba pana uasi hapa! Kwa mazingira ya ulipukaji wa mabomu, na kwa yale yaliyofanyika jana, ya wanajeshi kuwavamia raia wasio na hatia na kuwachapa, najiridhisha kwamba wanajeshi wa kambi hii wameshaasi, na hivyo siku si nyingi wanaweza kushika bunduki na kuingia mitaani kutuua kwa risasi baada ya jaribio la kutuua kwa mabomu kutokuzaa matunda yaliyotarajiwa.
Mwisho natoa wito kwa wakaazi wa gongo la mboto na maeneo ya jirani kuandaa maandamano ya kulipinga jeshi hili lililoasi na pia kumpinga Kikwete kwa kuwa ameshindwa kusoma alama za nyakati na kuchukua hatua.