Mchekechoni
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 279
- 19
Kufuatia hotuba ya Amiri Jeshi Mkuu, JK, ya 28/02/2011, kuhusiana na maandamano ya cdm kanda ya ziwa chini ya viongozi wake wakuu, ni dhahiri kuwa polisi wamefyata mkia na kuacha maandamano hayo yasonge mbele bila kubugudhiwa. Hii inaashiria kuchepuka kwa jeshi hilo kutoka utii wake kwa mkuu wa nchi na kuachana na matakwa ya ccm kudhibiti cdm. Kesho waziri mkuu, Pinda anaenda bukoba kujaribu kufukia mashimo ya Dr.Slaa na Mbowe (bila shaka baada ya kupokea simu kali toka kwa JK akiwa safarini ulaya). Je atafanikiwa kuzima moto uliowashwa na cdm?