Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,270
Naibu kamanda wa jeshi la Iran Jenerali Mas'ud Jazairi amesema kuwa Iran itajibu mashambulizi yoyote ya Israel dhidi ya vituo vya kuzalisha nishati ya nyuklia hapa nchini kwa kulenga kituo cha silaha za nyuklia cha Israel huko Dimona.
Jenerali Jazairi amesema kituo cha silaha za nyuklia cha Dimona ni shabaha rahisi kwa jeshi la Iran na kwamba iwapo utawala huo ghasibu utathubutu kushambulia Iran basi Tehran haitanyamaza kimya. Ameashiria pia vitisho na mipango ya Marekani ya kutekeleza mauaji ya kigaidi dhidi ya viongozi wa ngazi za juu wa jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu hapa nchini na kusisitiza kuwa majibu ya Iran yataitia majuto Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Siku chache zilizopita utawala ghasibu wa Israel ulisema kuwa unafikiria kushambulia vituo vya kuzalisha nishati ya nyuklia nchini Iran.
Jenerali Jazairi amesema kituo cha silaha za nyuklia cha Dimona ni shabaha rahisi kwa jeshi la Iran na kwamba iwapo utawala huo ghasibu utathubutu kushambulia Iran basi Tehran haitanyamaza kimya. Ameashiria pia vitisho na mipango ya Marekani ya kutekeleza mauaji ya kigaidi dhidi ya viongozi wa ngazi za juu wa jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu hapa nchini na kusisitiza kuwa majibu ya Iran yataitia majuto Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Siku chache zilizopita utawala ghasibu wa Israel ulisema kuwa unafikiria kushambulia vituo vya kuzalisha nishati ya nyuklia nchini Iran.