Jerry Silaa kashindwa kazi?

unaelewa tofauti ya diwani na mbunge, jibu hili ukifafanua hoja za kushangaza za brigedia. Meya je? Unajua majukumu yake kulingana na hoja za brigedia, jamani tuweni na kiasi ndugu zangu, lawama tu hazitajenga, zknabomoa.... Kama mnahisi mna hoja mbona ratiba ya kumuona meya iko wazi, ugumu ni upi kumtembelea ofisini kwake!? Mbona hamueleweki?!!

Mwingine anasema figa hazidaidii, sasa ni kipi kinasaidia? Ama mnataka Silaa aelezee maendeleo ya kila mpiga kura binafsi, kama ni uchafu wa jiji wote nyie mnashiriki kuluchafua, kutupatupa machupa ya maji mamifuko ya salfeti hovyo unadhani jiji litapona!? Nani asiyejua kwamba hujuma ni kubwa mno katika huduma ya maji? Hivi ni wangapi wenu mna magari ya kusambaza maji? Tuweni wakweli, mbona mnamsakama hivyo Silaa? Kagusa maslahi yenu nini!!!!!!

Jerry nimeona umekuwa ukijibu hoja zilizo nyingi lakini mbona za Bregadia hujibu?.Au amekuchana live?
 
MTM,
Ahsante sana kwa kujitahidi kumjibu huyo hossama, ameonyesha ufinyu wa mawazo.

Tangu mwanzo nilisema wananchi tunataka kuona huduma za jamii zikiwa bora, sio kuambiwa maneno makavu yaliyoko kwenye makaratasi ofisini kwa meya.

Huyu hossama alivyo kiazi anaidharau JF wakati huo huo anaitumia kumkingia kifua meya ambaye amethubutu kuja hapa kufafanua mambo hata kama mambo mengine hayajayajibu, kitu ambacho naamini anajipanga atakuja kuyajibu kwa muda muafaka. Hawa ni wapambe nuksi ambao huwapotosha viongozi kwa kuwajaza maneno yasiyofaa na ya kuwapotosha.

Hossama tafuta mkate wa watoto wako (kama unao) kwa njia nyengine, sio hii ya kumpotosha meya.
 
Mimi ningependa kumuuliza Mheshimiwa swali basic tuu, nani aliyeruhusu kuwekwa kwa vizuizi kwa wapita njia kupita mbele ya jengo la ILO. Na jee manisipaa imewajengea Wananchi njia nyingine ya mbadala?
 
Tumia ID yako ya kawaida utasomeka tu.
Mbona una kiherehere sana kama panya buku!? Mjadala ufungwe kwa kushindwa kujibu hoja?
Kama unadhani ''kubwabwaja'' hapa JF haisaidii kitu, mbona jerry amekuja kujieleza hapa!

FYI Jerry atahojiwa tu, iwe JF, Mtaani ama FB.

Asikupe shida huyu jamaa ni mwandish wa habr.na ni mkristo,hili jina hapo ni zuga,aliwai gombea udiwani huko ... Kwao na kupigwa chini.
Kwaiyo anamtetea magamba mwenzie.
 
Mheshimiwa Meya,
Umenijibu hoja zangu katika post #83 ingawa huku tag ili kuweka majibu yako wazi lakini nimekuelewa.
Kwanza wewe ni kiongozi na unakutana na watu tofauti na wenye mitazamo tofauti.
Siku zote kiongozi hupaswa kuwa mvumilivu, mtulivu na mwelekezaji.
Nikifutailia hoja zako naona una jazba na hasira kana kwamba unashambuliwa.

Jambo moja linalokuweka hadharani kuliko watendaji wengine ni nafasi hiyo ukiwa msomi na kijana.
Mbiu ya viongozi vijana imepamba moto na wewe kama mmoja wao ni 'sample' ya kuthibitisha kama madai ya vijana kupewa nafasi za uongozi yana mamtiki au la. Kila unachokifanya ni 'template' ya kwanini vijana wanapaswa wapewe nafasi zaidi katika uongozi wa taifa

Inapotokea matarajio hayakidhi matokeo wanaokulaumu ni vijana wenzako kwa kuwa disappoint. Unachotakiwa ni wewe kuchukua maoni yao kama changamoto na kuyafanyia kazi. kuwadhihaki ni kauli ya kusikitisha sana na inaondoa hata matarajio kidogo waliyo nayo juu yako.
Ukiwa kama bado hujafika pale unapokusudia na kauli zako kama kiongozi zinabaki katika kumbu kumbu na huenda zikakuhukumu mahali usipotarajia. time will tell. Turejee kwenye hoja

Jerry;The point is mwaka mmoja si muda wa kutosha kuona "result"
Mwaka mmoja unatosha kwasababu hukuingia ofisini na kukuta ukumbi. Umekuta kila kitu zikiwemo sheria. Ulichotakiwa kufanya ni kuanza kurekebisha kile kibaya halafu unaweka mkakati wa mema.

Keenja anakumbukwa kwasababu uwepo wake ofisini ulitoa matokeo katika kipindi cha miezi mitatu. Nilikuwepo na nalifahamu vema hili. Hakufanya maajabu bali kusimamia na kuondoa uzembe. Badala ya kuwafukuza wafanya biashara kisutu katika korido, aliwaamuru watengeneze frame za kuweka bidhaa zao. period. Wapita njia wakawa na nafasi na wafanya biashara wakawa na nafasi.
Hili hakuhitaji miaka 5 kama unavyotaka iwe.

Keenja akakusanya mapato na ghafla tukaona pavement zinasakafiwa na kila mtu alijua ongezeko la mapato linatoa matunda yanayotarajiwa. Hakuhitaji miaka 5 wala kuandika sheria zilziopo kama uanavyodai.
Keenja ndani ya mwaka mmoja alirudiha nidhamu na Dar ikatajwa kama Jiji safi hata na wageni.

Tunapomuangalia Mzee Keenja na Kijana Silaa halafu tukasikiliza hoja zako, nashawishika kusema ujana tunaoupigia debe una walakini.
Kwanini ulalamike badala ya kusikiliza na kujifunza? kwanini usitumie usomi wako kutafuta suluhu?
Tajiri ni relative word, majukumu ya handeni na ilala hayaendani. Tuna mapato makubwa na majukumu makubwa vikevile
Nasema Handeni wana majukumu makubwa. Hawana miundo mbinu kama sewarage, maji safi, maji taka, nyumba n.k.
Jerry, huhitaji kujenga ghorofa 50 ili watu wajue unafanya kazi, unachotakiwa ni kufanya simple things in simple way in extra ordinary way. Unabahati hata serikali kuu ipo kwako, wewe unaongea na waziri hata rais tofauti na Meya wa Handeni.
Mapato yako ni chocheo la maendeleo sio kutafuta sababu kama 'relative word'. Ubunifu ndio unahitajika lakini kama umeamua kufanya kazi ' business as usual' kwa hoja ya Ogah, hewala
Kama unashindwa kuona umuhimu wa revenue kwa aina yoyote ya taasisi sintaweza kukuelewa
Najua umuhimu wake ndio maana nimesema kukusanya sio mafanikio ni wajibu wako from day one. Hata kama unakusanya bilioni 100 kwa siku, hazina maana kama bado Meya unaridhika maji yajae pamba house miaka 20 na wewe ukilijua hilo. Hatuhitaji kujua unafanya nini ofisini lakini tutahoji hivi Ilala kuna meya ikiwa sehemu kama Pamba house ameshindwa kuwasiliana na wahusika au idara zake na kutafuta suluhu. Pesa kwenye account ya jiji is not our problem, tunataka kuona hizo pesa unazi tranform vipi katika maisha ya wakazi wa Ilala
Wananchi wa halmashauri ya ilala wanamiliki 8% ya hisa DCB, ni benki yao. Na inamatawi mnne ilala anatoglo, tabata, ukonga na chanika. Nitajie bank nyingine yenye matawi manne ndani ya ilala
Ungefikiria kuongeza CRDB vijana, Lumumba na NMB ungekuwa na matawi zaidi. Sijasema kwanini bank ya watu wa Dar nimesema ongeza wigo. Tatizo hapa unacheza na karata ya kisiasa kujijengea uhalali lakini kiutendaji siasa haina nafasi. Let us hope wananchi wa Ilala wataridhika na hatua zako.
Narudia tena Ilala ni taasisi kubwa , mpango wa usafi ni document ya 20 pages na ina lot 6. Tano ni privatization na moja ni kutumia CBO za mitaa kufanya primary collection na malori ya halmashauri kufanya secondary collection. Na vilevile kutoa back up kwenye lot nyingine. Ndugu yangu sijui unatoka sekta gani lakini maeneo sensitive kama usafi 100% privatisation ni hatari
Sijasema privitization 100% nimesema kupunguza work load inabidi kuwe na privitization.
Kwa taarifa nimetoka sekta ya afya (public health) na nimewahi kufanya shughuli na taasisi kubwa za afya duniani. Kama ungekuwa msikivu huenda ungechota kitu. Pengine nikukumbushe kuwa unapozungumzia malori na ukusanyaji taka hujagusa tatizo, wapo mabwana afya, je unawatumia kama inavyopaswa? Unapoangalia suala la afya utagundua kuwa hakuna privitization 100% bali matumizi ya resource ulizo nazo na private sector. Angalia vitu in wider prism na jifunze kutoka kwa wengine pia
Ni vyema uwe upost na hizo picha za " kuzungukwa nao" unless unacoment kwenye jambo la mtu usiyemjua. Leadership ethic act 1995 inaeleza wazi na sijaona baya nilolifanya, ni vyema kama unalo uliweke watu waone. Usiaminishe watu kwa hearsays!
Sio mara moja umeonekana ukiwa nao na sihitaji kuweka picha.
Kuonekana ukiwa umezungukwa nao si tatizo wala hoja ni haki na sahihi.
Jerry, unaposoma kitu kama sheria halafu ukaacha busara ni tatizo kubwa. Wale ma-miss walio na vichanga vyao Amana hospitali sakafuni hawajui Leadership act ya 1995. Kama hutatumia busara kufahamu kuwa uonekanao wako unaweza kuzua maswali hilo sina hoja.

Nafaham unajitahidi kufanya kitu kinaitwa 'PR' swali ni kuwa unaifanya ikiwa na busara? Hili sihitaji mjadala kwasababu ni ushauri kwahiyo nisingependa tulijadili tena. Ninachosema ni kuwa hawa watu wanaosema unauza sura wana hoja zao hebu wasikilize halafu jiangalie.
 
Sawa tu kaka, ila ukweli daima unauma. Kubwabwaja kwenu hakutasaidia kitu, wewe kama mdogo X umesaidia nini mtaani kwako? Umeshiriki kikao gani cha maendeleo ukamwaga upupu wako? Mtu kamaliza mwaka mmoja tu maneno milioni hivi hamna kazi za kufanya? Mbona JK alimaliza miaka mitano akasema kwa muda wote huo alikuwa anasoma matatizo yenu, je mlikenua meno kuhoji hilo? Mkiambiwa ukweli mnahama key, do you real think mna point hapa zaidi ya kumwaga njegele tu!

Huyo mwingine anaibuka na ID, hivi mbona wewe unajiita X, hilo ndo jina lako, na ukweni kwako wanalitumia hilo?

Silaa kuja humu ni lazima kwa kuwa mnapotosha watu, mara huyu bia, yule ubunge, huyu uchafu, yaani hamna hata vipaumbele. Mtu anawaelimisha namna system ilivyo mbovu na namna anavyopigana lakini mpo tu, full ubishi, mnadhani sifa?

Mvuta bangi mwingine anaibuka na hoja eti mimi nilidisco udiwani, hivi tuelewe lipi sasa, mara oohh ni mkristo, sasa una maanisha nini? Mbona hamna hoja?

Jitahidini kutambua kazi za umeya na zile za ubunge then njooni tusemezane, Imenukiliwa nabik Issa aliwauliza wanafunzi wake 'enyi kizazi cha nyoka nitakaa na ninyi na kuwaelimisha na kuwajenga hata lini? Akamalizia na hii, 'enyi wanafki mnawezaje kuondoa kibanzi katika jicho la mwingine ilhali boriti limewajaa machoni penu!? Hivi hamuoni aibu!

Pangu Pakavu.

Asikupe shida huyu jamaa ni mwandish wa habr.na ni mkristo,hili jina hapo ni zuga,aliwai gombea udiwani huko ... Kwao na kupigwa chini.
Kwaiyo anamtetea magamba mwenzie.
 
Hata watu wake waliomchagua udiwani pugu guluka kwa lala walioathirika na mabomo ameshindwa kuwasaidia,nyumba zao walioahidiwa kujengewa unakwenda mwaka na zaidi
 
Hata watu wake waliomchagua udiwani pugu guluka kwa lala walioathirika na mabomo ameshindwa kuwasaidia,nyumba zao walioahidiwa kujengewa unakwenda mwaka na zaidi
 
Mimi naona ni Muda Muafaka wa Kumshauri Bwana Jerry Kuwa Muda wa Bla bla Umekwisha Tunataka Vitendo!! Kwa Ilala naona katika Dar es Salaam ndio sehemu inayoongoza kwa kero za kila aina!! Fikiria katikati ya jiji Hakuna utaratibu Wowote wa Utembeaji wa Miguu (Full Mkanganyiko), Uendeshaji magari (Ni kero ambayo kila mtu ameamua Kukaa kimya) na Ufanyaji wa Biashara (Hakuna utaratibu wa aina yoyote !! Mtu anauza magari = show room katika pedestrian road? Hii ni kwa jerry silaa tu!!) Sasa wewe ni meya wa ilala na Gari Kubwa ni nini cha maana unatufanyia? City centre kama Jalala!! Wake up my brother acha bla bla Hata kama umeiga kwenye Majiji ya wenzetu just make it to happen in Dar!! Yaani Huwa nadiriki kusema Dar es salaam "tunaishi kama mifugo" na mwisho wetu wa kufikiri umefika mwisho?
 
Sikujua kama kuna msemaji wangu.

Kwa taarifa jimbo la Ukonga nilishiriki kwa asilimia kubwa kuhakikisha linagawanywa na ningekuwa na nia ya ubunge ningegombea 2010.

Keep the revord clear, sigombei Ubunge 2015.

Mipasho.
Dogo kuwa makini unazungumza na watu tunaokujua in & out!
 
Hossama,
Nadhani umekuja JF kwa bahati mbaya na hujui ni kwanini unaishi.
Nilikuwa nakuona kwenye jukwaa la dini nikajua zimo lakini kwa jinsi unavyoandika hapa inaonekana hauna lolote unalolifahamu kuhusu uendeshaji wa manispaa pamoja na majuku ya diwani, meya pamoja na mbunge. Inaonekana hutambui njia za mawasiliano zipo nyingi kiasi gani. Jerry unayetaka asihojiwe kwenye mitandao anafahamu umuhimu wake na anaitumia, si JF tu bali twitter, fb n.k

Kama unadhani mwaka mmoja ni muda mfupi wa kupima utendaji wa mtu hujui ulitendalo, si ajabu umesema unashauriana na mkeo kabla hujaandika. Na kama haya unayoandika hapa ni mawazo ya watu wawili, mke na mume, najaribu kujiuliza ukiandika kwa akili yako mwenyewe utaandika utumbo kiasi gani?

Hossama kwakuwa wewe ni mzoefu zaidi wa jukwaa la dini na imani, nakushauri uendelee kujikita huko huko, soma Biblia kwa kumutanguliza Roho mtakatifu ili akuongoze kuielewa kweli itakayokuweka huru, vinginevyo utakuwa nabii wa uongo.
Sisi tutaendelea kumhoji Jerry kwakuwa ni diwani wetu na meya wa manispaa yetu. Tunalipa kodi ni lazima tuhoji matumizi yake.
 
Najibu humu kwa mambo mawili, moja kuweka kumbukumbu sahihi, mbili kuwapa taarifa sahihi watu wanaovisit JF.

Kwanza ifahamike kuendesha halmashauri its beyond hata Mayoka anavyoweza kuimagine. Ni taasisi kubwa iliyoundwa na kuendeshwa kwa mujibu wa sheria, na si ukiwa meya unaweza ukaamka asubuhi na kuamua jambo au ukafukuza mtumishi au ukaajiri au ukaweka mkandarasi au kumfukuza anayeharibu.

Halmashauri ina zaidi ya watumishi 7000 watanzania, wakiwemo ndugu na rafiki wa Mayoka, ambao kila mtu asipojituma na ukizingatia kazi za serikali ni mtambuka anakwamisha maendeleo na kazi nyingine.

Kazi zimefanyika nyingi, Ingawa Hosam amejaribu kueleza tuliyoyafanya sekta ya afya bado naona wenye nia zao hawataki kuelewa.

Kiufupi tuna matatizo ya rasilimali fedha, mfumo wa sheria na muingiliano madaraka wa taasisi za umma na uyendaji mbovu wa watendaji wa halmashauri. Tumetumia muda mwingi kwenye kuongeza mapato na kupunguza matumizi maana mambo mengi yanajitaji fedha.

Mfano: Soko la Ilala lililokuwa linakusanua 3-4m kwa mwezi sasa tunakusanya 9-10m. Eventually mapato yameongezeka toka 16B 2010/2011 mpaka 26B 2011/2012. Tumepunguza matumizi toka dev 40% vs recurrent 60% mpaka Dev 60% vs recurrent 40% kwa maelekezo ya kila shilingi moja senti 60 zihamishiwe dev account bila kuchelewa tofauti na taasisi nyingine zinazotumia kwanza recurrent zikibaki ndio zinaenda dev.

Tumekuwa halmashauri ua kwanza kuanzisha mfumo wa kukusanya mapato kupitia Bank ka kuitumia benki ya wananchi wa Dar es salaam kupunguza mianya ya kuvuja mapato.

Tuta-install a computerized revenue collection system kuongeza tija. Tunafanya mabadiliko mengi ya sheria ili kuendana na wakati na sasa sheria mpya ya usafi iko functional na pamoja na kubadilisha utaratibu wa kupata na kusimamia makandarasi wa usafi tulitarget 1st January tunze lakini tumechelewa mpaka 1st March kutakuwa na mabadiliko makubwa.

Tumenunua malori 9 ya taka kuongeza nguvu. Tunanunua greda 2 na moja tulilonalo yutakuwa 1st council sio tu kumiliki greda zaidi ya moja bali matatu kwa ajili ya kuchonga njia za mitaani ambazo ni unpaved.

Tumekuwa council ya kwanza kukopa TIB kwa ajili ya ujenzi wa soko la kisutu ambalo litamilikiwa 100% na wana ilala na si mikataba ya JV ya kifisadi ambayo kila siku watu wanakuja ofisini kwangu kuomba. Yote haya yapo kwa internet ambapo picha mlioiona ni hii tu.

Kwa taarifa hii ilikuwa shear charity ball ya mwaka juzi ambayo ni jitihada za mjasiliamali mzawa kusaidia wenye shida. Pesa iliyopatikana hapa ilienda CCBRT kusaidia kina mama wenye fistula.

Mayoka jiulize ni lini umejitoa kwenye jamii. Humo humo ulikopata hizo picha zipo nikiwa na mke wangu na ndio maana nasema mazungumzo haya myapeleke FB maana profile zetu zipo wazi.

Halmashauri ni taasisi inayofanya marketing and PR na katika hilo meya huwezi kumwacha kila aliyetumia neno "kuuza sura" ameonyesha uwezo wake finyu wa kufahamu mambo, kama wanavyosema wanazuoni "intellectuals discuss issues not personality" najua ni ngumu mtu akijiangalia umri wake na achievement alizorecord kukubali failure, ila it doesn't make u a better person kwa kushambulia wengine.

Mfano UDA inamilikiwa na Halmashauri ya jiji na mimi ni meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, unaniingizaje huko.

Mwisho mimi ni kijana na kama binadamu mwengine nina haki ya kusocialize na sioni mahusiano na kazi za umma. Naamini wapenda maendeleo wamenielewa, as usual na karibisha comments and critics.

Kwa jibu hili sasa naona tutaenda sambamba,kwa kweli kijana huyu ni fisadi anayechipukia,ni rafiki mkubwa wa Riz 1 na ndiye aliye mpigia pande la umeya hapo na kuhusu suala la kuihusisha DCB katika masuala ya ukusanyaji wa mapato ya halmashauri ni dili ambalo ameingia na mkurugenzi wa Benki hiyo Mr Mkwawa kwa kifupi ni kwamba Mkwawa ambaye ni mtu wa madili na Jerry (fisadi anaye chipukia) mwanafunzi wa ufisadi toka kwa Masaburi na Makongoro Mahanga wamemuingiza Mweka hazina wa Manispaa kwanza kwa kumtisha (black mail)kujua madili yake hivyo wakitaka kumlinda itabidi akubaliane nao hivyo alipo ingia mkenge bila ya kumshirikisha mkurugenzi ambaye mpaka sasa yupo njia panda (maana huyo Mkurugenzi anataka astaafu vizuri hapo mwakani) baada yamakubaliano Mweka hazina (ndugu yake Luhanjo katibu mkuu mstaafu[ambaye Mkwawa naye ni wa hukohuko]) kwamba atapata mgao wake pamoja na kumalizia kumjengea gholofa lake ambalo halina maelezo. dili hilo limekwama kidogo TAMISEMI maana kuna mtu wanataka wamtengeneze akisaini tu Manispaa yote imebinafsishwa na makampuni ambayo tayari yanapiga jalamba kuchukua hizo tenda yanajulikana na niya hao hao waeshimiwa na jamaa zao .Huyu dogo aliposhika tu umeya alikataa kata kata kuingia ofisi aliyo toka meya wa Mwanzo Abuuy Jumaa kwa sababu anazo zijua yeye mwenyewe na kufanya ukarabati wa nguvu katika ofisi iliyo kuwa ya afya na masijala ya elimu na kuwafukuza waliokuwemo awali ukarabati ulio tumia mamilioni ya shilingi nje ya bajeti nahakuna aliye thubutu kuhoji. Huyu dogo ameikodishia Manispaa gari yake Toyota Land cruiser Hard top no.T 740 BCC kwa gharama kubwa ambazo zinaingia kila siku gari linatumiwa na idara ya Ujenzi lakini hakuna kazi yoyote linalo fanya yote hayo na mengine mengi ambayo nitakuwa nayatoa kwa awamu ni ukusanyaji wa fedha hizo kwa kujiandaa na Ubunge wa 2015 ambao ameahidiwa na Riz1 Eeh MUNGU iangalie Tanzania kwa jicho la huruma MUNGU Ibariki TANZANIA , MUNGU Ibariki AFRIKA!
 
Tatizo wapigakura wanataka wauza sura ndio maana walimchagua dogo, lakini hakuna chochote anachofanya mwulizeni amefanya nini kwenye maeneo ya Ukonga-Ulongoni na Mongo la Ndege? kama si kujaa mahandaki tu!
 
kwanza niseme tu kuwa nimefurahi kuona viongozi wetu (hasa Mayor Jerry) wakijibu hoja mbalimbali humu-laiti kama wangefanya hivyo na wenzako pia, waliomo humu JF.
Swali langu kwako mheshimiwa- hivi ni nini mpango wa kujenga barabara ya mombasa-moshbar kwa kiwango cha lami?! tafadhali nisaidie
nilisikiasikia bungeni mwaka jana lakini sikuelewa!!
 
Jana (22/1/2012) kasema walimu wwa shule tano za mwisho kwa uchafu waadhibiwe, inafaa tuanze naye huyu maana Dar ni Jiji chafu kuliko yote.................
 
huyu kazi yake kubwa ni kuuza nyago na mfano karimjee siku ile anakaa kwenye kiti cha kiongozi wa kambi mpaka akanyenyuliwa kwa nguvu aibu
 
mstahiki meya wa ilala, mbona ulianza kujibu maswali humu ndani vizuri?umekuwaje tena mbona huonekani kujibu hoja; tuna hamu ya kusiia majibu yako tulouliza
 
Wanajamvi,

Ukipata nafasi ya kukutana na meya wa manispaa ya Ilala Mstahiki Jerry Silaa Utamuuliza nini?!

Binafsi nitamuuliza kuhusu mgogoro wa Machinga complex na kukithiri kwa foleni na uchafu katika manispaa hiyo, kwako je? utamuuliza nini??


NB:

Am very serious kama hauna point ya msingi tafadhali usichakachue uzi huu!


jerry.jpg

 
Wakati yupo pale chuo nilimuona yupo yupo tu na wala hakuwa na influence yoyote alipoibukia nadhani ni mshangao wa wengi, kuwa mwanasiasa nadhani ni kama vile kuwa mcheza mpira ama filamu kila mtu atakujua!
 
Back
Top Bottom