Jerry Silaa kashindwa kazi?

Sasa kujifanya ana mipango kabambe kumbe naye ni timu moja na masaburi na iddi simba kwenye sakata la UDA?

ama kweli JF mnajua kuibua ishu
 
Nimewahi kukutana naye huyu kijana eti anafanya biashara ya madini kwenye ka ofisi kake pale kaliakoo wakati ule, nilisikia amekuwa meya nilifurahi sana, lakini kama hashughuliki na matatizo ya wananchi wake ataniudhi sasa hv
 
huyu dogo hakuna kitu anachofanya bana.....matatizo lukuki wanaface wana ilala......

....mpaka leo foleni hana jibu.....

...basi kama foleni atasingizia hana fund.....na suala la uchafu je?
 
WanaJF,

Wakati mwingine tuwe na kiasi katika kumlaumu ama kumpongwza mtu, naomba niwakumbushe kwamba system ya nchi hii ni ngumu sana na zaidi ni nyimi sana. Kuna wakati chadema walitamka kutokutambua matokeo yaliyompa urais JK na kwa maana ingine kutomtambua kabisa rais. Lakini mwisho wake ni JK yuleyule ndio mwenye final say hata kwenye kuweka mapesa kwenye mifuko ya maendeleo ya majimbo chini ya wabunge wote.

Silaa sikutegemea atafanya lolote la kushangaza ikiwa huko nyuma hakuna chochote kilichofanyika cha maana sana. Anashindwa kufanya mambo mengi kwa sababu nguvu yake haishindi system ma mkae mkijua ccm iko makini kuwakwamisha chadema katika kila jambo. Aibu tuliyovuna ya chadema kwenda ikulu kumshauri mtu wasiyemtambua inatosha kuonyesha kwamba Silaa hana cha kufanya hata awe anashinda vijiweni kwa sie akina choka mbaya.

Ndio nasema ni afadhali katiba yetu mpya, kama ni kweli itaandikwa, ipunguze madaraka ya rais ili pawepo na universal balance. Kama tutapoteza muda kutaka kujua Silaa kafanya nini kwa mwaka mmoja tu ihali hata serikali haiwezi kulipa mishahara kwa watumishi wake tutakuwa tutakuwa ni wavivu wa kufanya tafiti na kutoa mijadala.

Siku zote, hatutaweza kumpima mtu utendaji wake kwa kumvizia ama kumlinganisha na mwenzake, tunampima mtu kulingana na mipango mkakati yake na hali halisi. Hapa JF nishaona sana watu wanaanza kupoteza sifa ya u great thinkera na badala yake gossips zimekuwa ni sehemu ya mijadala yetu, tuwe wakweli, kama Silaa anauza sura basi ni sawa mwacheni auze sura kwani nyie mlikuwa wapi kumhoji wakati mnamchagua? Ama niulize hili, mlikuwa wapi kumdodosa kabla ya kukmasim madaraka hayo makubwa.

Mwisho napenda kuwashukuru wote mliochangia thread hii, na ni wakati huu sasa ambapo naitisha wote msitishe kuchangia kwa kuwa hakuna hoja nziti za kumlaumu mtu ndani ya mwaka mmoja. Kama mtu ataendelea kuchangia hoja hii ni sawa kwa kuwa katiba inaruhusu mawazo binafsi yasiyovunja sheria.

Nawatakia mwaka mpya wenye baraka na mafanikio, na kwa Silaa, nakuomba punguza kwenda kwenye kumbi za starehe na gari la umma wakati usio wa kazi, gari hilo ni nyenzo kwako katikz kufanyz kazi zako rasmi za umeya na sio mara Double Tree, mara mlimani city, mara rose garden, babu unajishushia.

Ni mimi,
Pangu Pakavu,
Nawasalimia.
 
WanaJF,


Wakati mwingine tuwe na kiasi katika kumlaumu ama kumpongwza mtu, naomba niwakumbushe kwamba system ya nchi hii ni ngumu sana na zaidi ni nyimi sana. Kuna wakati chadema walitamka kutokutambua matokeo yaliyompa urais JK na kwa maana ingine kutomtambua kabisa rais. Lakini mwisho wake ni JK yuleyule ndio mwenye final say hata kwenye kuweka mapesa kwenye mifuko ya maendeleo ya majimbo chini ya wabunge wote.

Silaa sikutegemea atafanya lolote la kushangaza ikiwa huko nyuma hakuna chochote kilichofanyika cha maana sana. Anashindwa kufanya mambo mengi kwa sababu nguvu yake haishindi system ma mkae mkijua ccm iko makini kuwakwamisha chadema katika kila jambo. Aibu tuliyovuna ya chadema kwenda ikulu kumshauri mtu wasiyemtambua inatosha kuonyesha kwamba Silaa hana cha kufanya hata awe anashinda vijiweni kwa sie akina choka mbaya.

Ndio nasema ni afadhali katiba yetu mpya, kama ni kweli itaandikwa, ipunguze madaraka ya rais ili pawepo na universal balance. Kama tutapoteza muda kutaka kujua Silaa kafanya nini kwa mwaka mmoja tu ihali hata serikali haiwezi kulipa mishahara kwa watumishi wake tutakuwa tutakuwa ni wavivu wa kufanya tafiti na kutoa mijadala.

Siku zote, hatutaweza kumpima mtu utendaji wake kwa kumvizia ama kumlinganisha na mwenzake, tunampima mtu kulingana na mipango mkakati yake na hali halisi. Hapa JF nishaona sana watu wanaanza kupoteza sifa ya u great thinkera na badala yake gossips zimekuwa ni sehemu ya mijadala yetu, tuwe wakweli, kama Silaa anauza sura basi ni sawa mwacheni auze sura kwani nyie mlikuwa wapi kumhoji wakati mnamchagua? Ama niulize hili, mlikuwa wapi kumdodosa kabla ya kukmasim madaraka hayo makubwa.

Mwisho napenda kuwashukuru wote mliochangia thread hii, na ni wakati huu sasa ambapo naitisha wote msitishe kuchangia kwa kuwa hakuna hoja nziti za kumlaumu mtu ndani ya mwaka mmoja. Kama mtu ataendelea kuchangia hoja hii ni sawa kwa kuwa katiba inaruhusu mawazo binafsi yasiyovunja sheria.

Nawatakia mwaka mpya wenye baraka na mafanikio, na kwa Silaa, nakuomba punguza kwenda kwenye kumbi za starehe na gari la umma wakati usio wa kazi, gari hilo ni nyenzo kwako katikz kufanyz kazi zako rasmi za umeya na sio mara Double Tree, mara mlimani city, mara rose garden, babu unajishushia.

Ni mimi,
Pangu Pakavu,
Nawasalimia.
acha kutufanya sote wajinga humu
No one is asking for much

alipokuwa anagombea umeya wa wa Ilala alijua kuwa anagombea umeya wa wilaya iliyotajiri kuliko zote tanzania

bila kusahau kuwa alitoa ahadi kem kem za uchaguzi

watu wanauliza program yake ya kuibadilisha ialala iko wapi?

je kashafanikiwa ninia?

je ana mipango gani siku za mbeleni?

is that too much to ask?
 
Hii thread ya Hossam aka pangu pakavu ameandika Jerry William Silaa mwenyewe.

Jerry mimi ni rafiki yako wa siku nyingi sana, wakati tunaogelea wote mto msimbazi na tunasoma wote Ukonga Primary School, kwa mwalimu Nyandindi, Ntilu, Buyobe, Best etc.

Jerry my friend you need to do more than what you are doing now, maisha ya ukonga hata kwenu Pugu yamekua magumu sana, just badilika na uwe makini kwenye mambo yako... Achana na mambo ya ujana, kama kipindi kile ulivyokua... Pls elewa now unatumikia umma!
 
Hii thread ya Hossam aka pangu pakavu ameandika Jerry William Silaa mwenyewe.

Jerry mimi ni rafiki yako wa siku nyingi sana, wakati tunaogelea wote mto msimbazi na tunasoma wote Ukonga Primary School, kwa mwalimu Nyandindi, Ntilu, Buyobe, Best etc.

Jerry my friend you need to do more than what you are doing now, maisha ya ukonga hata kwenu Pugu yamekua magumu sana, just badilika na uwe makini kwenye mambo yako... Achana na mambo ya ujana, kama kipindi kile ulivyokua... Pls elewa now unatumikia umma!
Gotta love JF!
 
Najibu humu kwa mambo mawili, moja kuweka kumbukumbu sahihi, mbili kuwapa taarifa sahihi watu wanaovisit JF.

Kwanza ifahamike kuendesha halmashauri its beyond hata Mayoka anavyoweza kuimagine. Ni taasisi kubwa iliyoundwa na kuendeshwa kwa mujibu wa sheria, na si ukiwa meya unaweza ukaamka asubuhi na kuamua jambo au ukafukuza mtumishi au ukaajiri au ukaweka mkandarasi au kumfukuza anayeharibu.

Halmashauri ina zaidi ya watumishi 7000 watanzania, wakiwemo ndugu na rafiki wa Mayoka, ambao kila mtu asipojituma na ukizingatia kazi za serikali ni mtambuka anakwamisha maendeleo na kazi nyingine.

Kazi zimefanyika nyingi, Ingawa Hosam amejaribu kueleza tuliyoyafanya sekta ya afya bado naona wenye nia zao hawataki kuelewa.

Kiufupi tuna matatizo ya rasilimali fedha, mfumo wa sheria na muingiliano madaraka wa taasisi za umma na uyendaji mbovu wa watendaji wa halmashauri. Tumetumia muda mwingi kwenye kuongeza mapato na kupunguza matumizi maana mambo mengi yanajitaji fedha.

Mfano: Soko la Ilala lililokuwa linakusanua 3-4m kwa mwezi sasa tunakusanya 9-10m. Eventually mapato yameongezeka toka 16B 2010/2011 mpaka 26B 2011/2012. Tumepunguza matumizi toka dev 40% vs recurrent 60% mpaka Dev 60% vs recurrent 40% kwa maelekezo ya kila shilingi moja senti 60 zihamishiwe dev account bila kuchelewa tofauti na taasisi nyingine zinazotumia kwanza recurrent zikibaki ndio zinaenda dev.

Tumekuwa halmashauri ua kwanza kuanzisha mfumo wa kukusanya mapato kupitia Bank ka kuitumia benki ya wananchi wa Dar es salaam kupunguza mianya ya kuvuja mapato.

Tuta-install a computerized revenue collection system kuongeza tija. Tunafanya mabadiliko mengi ya sheria ili kuendana na wakati na sasa sheria mpya ya usafi iko functional na pamoja na kubadilisha utaratibu wa kupata na kusimamia makandarasi wa usafi tulitarget 1st January tunze lakini tumechelewa mpaka 1st March kutakuwa na mabadiliko makubwa.

Tumenunua malori 9 ya taka kuongeza nguvu. Tunanunua greda 2 na moja tulilonalo yutakuwa 1st council sio tu kumiliki greda zaidi ya moja bali matatu kwa ajili ya kuchonga njia za mitaani ambazo ni unpaved.

Tumekuwa council ya kwanza kukopa TIB kwa ajili ya ujenzi wa soko la kisutu ambalo litamilikiwa 100% na wana ilala na si mikataba ya JV ya kifisadi ambayo kila siku watu wanakuja ofisini kwangu kuomba. Yote haya yapo kwa internet ambapo picha mlioiona ni hii tu.

Kwa taarifa hii ilikuwa shear charity ball ya mwaka juzi ambayo ni jitihada za mjasiliamali mzawa kusaidia wenye shida. Pesa iliyopatikana hapa ilienda CCBRT kusaidia kina mama wenye fistula.

Mayoka jiulize ni lini umejitoa kwenye jamii. Humo humo ulikopata hizo picha zipo nikiwa na mke wangu na ndio maana nasema mazungumzo haya myapeleke FB maana profile zetu zipo wazi.

Halmashauri ni taasisi inayofanya marketing and PR na katika hilo meya huwezi kumwacha kila aliyetumia neno "kuuza sura" ameonyesha uwezo wake finyu wa kufahamu mambo, kama wanavyosema wanazuoni "intellectuals discuss issues not personality" najua ni ngumu mtu akijiangalia umri wake na achievement alizorecord kukubali failure, ila it doesn't make u a better person kwa kushambulia wengine.

Mfano UDA inamilikiwa na Halmashauri ya jiji na mimi ni meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, unaniingizaje huko.

Mwisho mimi ni kijana na kama binadamu mwengine nina haki ya kusocialize na sioni mahusiano na kazi za umma. Naamini wapenda maendeleo wamenielewa, as usual na karibisha comments and critics.
 
Halmashauri ni taasisi inayofanya marketing and PR na katika hilo meya huwezi kumwacha kila aliyetumia neno "kuuza sura" ameonyesha uwezo wake finyu wa kufahamu mambo, kama wanavyosema wanazuoni "intellectuals discuss issues not personality" najua ni ngumu mtu akijiangalia umri wake na achievement alizorecord kukubali failure, ila it doesnt make u a better person kwa kushambulia wengine.
Mfumo mbovu wa serikali inayoongozwa na chama chako ndio imefikisha watu wengi katika daraja la kushindwa maisha.

Ni janga kubwa kuliko unavyodhani na kukejeli jamii inayokata tamaa
 
Jerry pamoja na maelezo marefu uliyoandika, watu wanataka kuona vitu vikifanyika, si mipango ya kwenye makaratasi ambayo haitekelezeki.
Pili, utambue kwamba hapa JF ndio mwisho wa reli tunamkoma nyani giledi, huwezi kulinganisha JF na FB ambako kazi kubwa ni kusifiana looking good na blah blah.

Tunataka utakapomaliza muda wa utumishi wako kuwe na kitu cha kuonyesha kwamba uli accomplish. Huwezi kutuambia kuna ongezeko la mapato wakati huduma za kijamii bado ni za hovyo halafu utegemee tusikwambie ukweli, hiyo sahau.

Mwisho, umekuwa ukirudia mara kadhaa kauli ya kuonyesha ugumu wa kuendesha manispaa, hiyo inadhihirisha kazi imekushinda, kama sivyo tunataka kuona maendeleo on the ground si kwenye makaratasi tu!
 
Sawa Jerry umetoa statistic nzuri za 16B to 26B kama kawaida yenu magamba.

Lakini people ni 'TOMASO' wanataka waone physical issues.

Kwa mfano (hii ni kwa kukusaidia) ile barabara ya Mombasa-Mazizini-Moshi bar, inakuwa okay, hospital/dispensary ya Mongorandege inakua na equipment na reagents pamoja na personnel.

Jerry, acha bla bla, 1 day utakuja kuzomewa kama L. Masha! Kumbuka, siasa inahitaji watu makini! Afu nimekumbuka, unakumbuka tulipomaliza form IV Pugu afu ukataka usome V na VI in 1 year? Ikabidi uende Jitegemee, wakakuchomolea. Piga kazi, kama unataka kula bata, mwisho wa siku itakula kwako bro!
 
mfumo mbovu wa serikali inayoongozwa na chama chako ndio imefikisha watu wengi katika daraja la kushindwa maisha. ni janga kubwa kuliko unavyodhani na kukejeli jamii inayokata tamaa


mawaidha mazuri sana haya kwa jerry, kama hawezi kukuelewa na kuendeleza nyodo na dharau, atashughulikiwa muda muafaka ukifika.

Tunafahamu anajiandaa kuwania ubunge 2015 tunakusanya kuni za kumkaanga kuanzia JF hadi mitaani!
 
Mkuu Jerry Slaa,andika kwa aya ili hoja zako zisomeke vizuri na kwa urahisi.Hii siyo 'chuki',ni kuwekana sawa tu
 
mawaidha mazuri sana haya kwa jerry, kama hawezi kukuelewa na kuendeleza nyodo na dharau, atashughulikiwa muda muafaka ukifika.

Tunafahamu anajiandaa kuwania ubunge 2015 tunakusanya kuni za kumkaanga kuanzia JF hadi mitaani!
Anajiandaa kugombea jimbo gani? Wacha na miye nizichange nikagombee, maana bongo siasa ndiko kwenye ulaji!
 
Back
Top Bottom